Bunge la akina Mwigulu Nchemba na Lusinde ndo hili

Sir M.D.Andrew

JF-Expert Member
Jul 30, 2012
201
37
Kazi ya mabunge yote duniani kote ni kuisimamia serikali ktk shughuli zote za kila siku,inachukuliwa kuwa bunge ni chombo kitukufu kinachowaleta pamoja wananchi ktk kujadili mambo nyeti ya kitaifa pamoja na kupata majibu ya kero za wananchi kutoka kwa mkusanya kodi(serikali)ni kawaida kwa serikali za kihuni kuwaibia wananchi,tegemeo la wananchi inapoonekana serikali inaendeshwa kihuni huwa ni bunge,Swali la msingi hapa ni je,bunge nalo linapoendeshwa kihuni na likajaza wabunge wahuni,wananchi wapate msaada wapi? Inapotokea bunge linaongozwa kibabe kiitikadi,bunge kunuka rushwa je ni makosa kusema kuwa tanzania ni ya wahuni?Unapokuwa na bunge la akina LUSINDE,MAJI MAREFU,MWIGULU NCHEMBA,ADEN RAGE,CHENGE,Na kiongozi wao akawa MAKINDA unategemea nini?jibu ni rahisi-UHUNI.
 
Kwa kweli tuna hali ngumu sana jamani. Kwa staili hii hata serikali haiwezi kujitahidi kuboresha hali za kiuchumi maana hata Bunge haliiweki kiti moto kwa kukatisha na kuwazuia wanaohoji vitu vya maana. Halafu eti tunadhani tunaweza kushindana na wenzetu wa East Africa!!
Sijui nchi yetu itakuwa lini maana kwa sasa tu BAJETI ya Kenya ni Ksh1.4 trillion ($17 billion) kwa mwaka 2012/13 ukilinganisha na Mwaka jana ilipokuwa ni Ksh1.1 trillion ($12.9 billion), wakati sisi huku Tanzania ni TSh15 trillion (9.5 billion US$), Ikiwa imeongezeka kutoka Tsh 13 trillion (US$8.2 billion) mwaka jana.
Kwa haraka tu utaona ongezeko kwa Mwaka kwa Kenya ni karibia 4.1billion US$, sisi eti tumeongeza 1.3billion US$ mwaka. Tena bado tunategemea hiyo pesa karibu 40% kutoka kwa wahisani. Wakenya pesa inayotegemea kutoka nje katika bajeti ni 8% tu.

Kwani Wakenya wana nini hata sisi tushindwe...mbona kama vile sisi ndo tunautajiri wa asili kuliko wao!!??


BUNGE LISIPOKUWA MAKINI NCHI HAIWEZI KUJITAHIDI KUONGEZA MAPATO...TUTAENDELEA KUTEGEMEA NCHI ZA NJE TU...AGGHHH!!
 
Kwa kweli tuna hali ngumu sana jamani. Kwa staili hii hata serikali haiwezi kujitahidi kuboresha hali za kiuchumi maana hata Bunge haliiweki kiti moto kwa kukatisha na kuwazuia wanaohoji vitu vya maana. Halafu eti tunadhani tunaweza kushindana na wenzetu wa East Africa!!.......

Bunge linatia hata hasira. Wabunge wanachefua tu, They think like being there is an end in it self. Yaani juhudi zao ni kuingia bungeni, kupata allowance, kula na kulala, kuzomea akisema mwingine. Hata kama mbunge hajasikia vyema hoja iliyotolewa, akisikia wengine wanazomea, naye anajiunga kuzomea.

Mwanasheria akitukana, Naibu spika anasaidia kubisha kuwa siyo tusi, so, mimi sielewi actually tunakoenda, bunge limekuwa eti "... wewe ni rafiki yangu, tukitoka tutaongea kuhusu swali lako...", mfano Nchimbi leo amejibu hivyo.

Yamekuwa tena maswali ya kwenda kuongelea kwenye bar ? we need to hear what the Minister says towards the asked question(s)! Leo waulizaji wawili au zaidi wameombwa wakaongee na Nchimbi after 4:30! is that what we want to hear? kama wanamsifu Rais kwa kupita kuomba omba nje, HAWATAONA UBAYA WA KUSUPPORT BUDGET KWA ZAIDI YA 40% ZA KUOMBA OMBA, Mh! Let's wait and see.
 
hawa jamaa wapo madarakani kwa msaada wa nchi za magharibi zinazonyonya rasilimali..lakini wamkumbuke mobutu,sadam na wengineo walivyobadilikiwa
 
Back
Top Bottom