Bunge kupitisha azimio la kumpongeza Spika Ndugai na Serikali kutobadili Makao Makuu ya shughuli zake

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,442
3,352
Bunge la Tanzania leo linaendelea na shughuli zake katika Mkutano wa 19, Kikao cha 40 ambapo baadhi ya shughuli ni kupitisha maazimio mawili

Azimio la kwanza ni Kuitaka Serikali kutobadili Uamuzi wa Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi na Shughuli za Serikali

Azimio la pili ni Kumpongeza Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kwa mafanikio ya Bunge la 11

Azimio la kwanza la kuitaka Serikali kutobadili uamuzi wa Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu linakuja wakati ambao tayari shughuli nyingi za Serikali zimehamia Dodoma. Rais na Wizara zote tayari zimehamia Jijini Dodoma

EZ-NeyKWoAAqKQW.png
 
Bunge la Tanzania leo linaendelea na shunguli zake ikiwa ni Mkutano wa 19, Kikao cha 40 kinaendelea leo na baadhi ya shunguli ni kupitisha maazimio mawili

Azimio la kwanza ni Kuitaka Serikali kutobadili Uamuzi wa Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi na Shughuli za Serikali

Azimio la pili ni Kumpongeza Sipka wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kwa mafanikio ya Bunge la 11

Azimio la kwanza la kuitaka Serikali kutobadili uamuzi wa Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu linakuja wakati ambao tayari shughuli nyingi za Serikali zimehamia Dodoma. Rais na Wizara zote yatari zimehamia Jijini Dodoma
hilo la makao makuu natamani itungwe sheria kwamba hakuna kurudi tena dar......

katika mambo yote aliyofanya magufuli hili la kuhamishia shughuli za serikali dodoma kwa kweli kwangu ni bora kuliko hata madaraja na reli anazojenga!
 
They dont care! Hili ndio tatizo ambalo litaonekana sana awamu ijayo kwa sababu Chàto electoral Comission itajaza viazi wengi Dodoma wale wanaosifia.

Na hawaogopi wao kazi yao itakuwa sio kuwatumikia wananchi bali kusifu na kusifi
 
Haaa.. Wewe ulikuwa bado unafagia hapo ufipa ama?
Wenzio wameileta toka zamani hapa
 
Bora wangeleta hoja ya ujenzi wa daraja la mto wami ambamo hadi leo kuna maiti hajaopolewa humo
 
hilo la makao makuu natamani itungwe sheria kwamba hakuna kurudi tena dar......

katika mambo yote aliyofanya magufuli hili la kuhamishia shughuli za serikali dodoma kwa kweli kwangu ni bora kuliko hata madaraja na reli anazojenga!


Amini usiamini, hata ikitungwa hiyo sheria watakaoisaliti na kuivunja hiyo sheria wamo humohumo!!!
 
Back
Top Bottom