Bunge kielelezo cha ukuaji wa demokrasia -Sitta

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Bunge kielelezo cha ukuaji wa demokrasia -Sitta
Mwandishi Wetu
Daily News; Tuesday,September 16, 2008 @00:03

Spika wa Bunge, Samuel Sitta amesema Bunge litaendelea kuwa kielelezo cha ukuaji wa demokrasia nchini, hasa baada ya kuongezeka kwa kiwango kikubwa cha hamasa kwa wananchi kufuatilia uendeshaji wa shughuli za chombo hicho cha kutunga sheria.

Sitta alisema ongezeko la hamasa ya wananchi kufuatilia mijadala bungeni ni matokeo ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Bunge kwa kipindi cha mwaka 2008-2013 pamoja na mabadiliko ya Kanuni za Kudumu za Bunge.

Akitoa salamu zake kwa niaba ya wabunge nchini katika kuadhimisha Siku ya Demokrasia Duniani jana, Sitta alisema moja ya mabadiliko ambayo yamepanua upeo wa demokrasia ndani ya Bunge na kuwa mfano wa kuigwa na mabunge mengine ni utaratibu wa maswali ya papo kwa hapo ya Waziri Mkuu.

Alisema maswali hayo ya kila wiki katika kikao cha Alhamisi, Waziri Mkuu huulizwa maswali kadhaa ya moja kwa moja bila kuyaona ambapo majibu ya Waziri Mkuu hutoa picha ya namna serikali inavyoshughulikia kero na matatizo ya wananchi.

Sitta alisema hatua hiyo ni muhimu kwa ukuaji wa demokrasia ambapo nafasi ya upinzani imesaidia kuleta changamoto mpya katika mijadala bungeni na hotuba zenye changamoto, hivyo serikali kuwa makini katika kufuata misingi ya utawala bora na kurekebisha sheria zenye upungufu.

Spika alivipongeza vyombo vya habari ambavyo ni wadau wakuu wa demokrasia nchini kwa kuwa mstari wa mbele kukemea maovu na kuwataka wamiliki wa vyombo hivyo kuwaongezea ujuzi waandishi wa habari ili wafanye kazi yao vizuri zaidi na kutoa mchango katika kukua kwa demokrasia nchini.
 
Acha uwongo Sitta! Watanzania tulikuwa tunafuatilia kwa makini kabisa kikao bajeti la Bunge la Tanzania kilichokwisha wiki mbili zilizopita. Tuliyoyaona huku yametusikitisha wengi wetu tunaopenda maendeleo ya Tanzania. Kulikuwa na usanii wa hali ya juu na maamuzi ya kuwalinda mafisadi. Hakuna demokrasi yoyote ndani ya Bunge ni usanii tu na mambo ya kuhuzunisha.
 
Acha uwongo Sitta! Watanzania tulikuwa tunafuatilia kwa makini kabisa kikao bajeti la Bunge la Tanzania kilichokwisha wiki mbili zilizopita. Tuliyoyaona huku yametusikitisha wengi wetu tunaopenda maendeleo ya Tanzania. Kulikuwa na usanii wa hali ya juu na maamuzi ya kuwalinda mafisadi. Hakuna demokrasi yoyote ndani ya Bunge ni usanii tu na mambo ya kuhuzunisha.


Kwa maoni yenu (wewe na Kuhani) mnaona hakuna hatua yoyote iliyofikiwa? (Tuangalie toka 2005)
Naamini Sitta anafanya kazi katika mazingira magumu mno. Tumpe support kwa kile kidogo alichoweza kufanya au kusimamia katika mazingira haya, likiwemo la mabadiliko ya Kanuni za Kudumu za Bunge. Labda mniambie hilo ni swala dogo sana.

Hii haina maana ya kumpa green light kama ambavyo wengine wamejaribu kumpa Mwakyembe. We should watch his every move.


.
 
Tumsaidie alitenganishe BUNGE na SERIKALI. Liwe kama Mahakama ilivyo. Hakuna Jaji ambaye wakati huohuo ni Waziri.
 
Mimi naamini kwamba kuna mabadiriko makubwa yanayoendelea bungeni ktk awamu hii. Tumeona sheria mbovu na za kifisadi zikifutwa na mahakama kutokana na juhudi za baadhi ya wanaharakati (Sheria ya Takrima). Tumeona baadhi ya viongozi wetu serikalini wakiwajibishwa (Karamagi, Msabaha), au wakilazimishwa kujipima na kujivua madaraka waliyonayo (Lowassa). Tumebahatika kuona ujasili wa baadhi ya wabunge katika kuibua masuala bungeni (Richmond, EPA), na wakiamua kuwajibika bila kujali hatari, vitisho, onyo, na adhabu walizokuwa wakipata (Amina Chifupa, Anna Malecela, Zitto Kabwe, Wilbrood Slaa, Harrison Mwakyembe ...nk). Na hatimaye tumeona sheria nzuri ikipitshwa na wabunge wiki mbili zilizopitaya kutenganisha Bunge na Serikali. Sheria hii pia inalenga kuwaongezea wabunge mazingira mazuri ya kazi kwa kazi waliyopewa kikatiba na kuwaongezea kipato ili kuwapa fursa ya kufanya kazi vizuri zaidi. Kwa kipimo chochote kile hayo ni maendeleo makubwa kwa kweli.

Pamoja na hayo yote, kuna mengine yanayofanyika bungeni hivi sasa yanayotia mashakani maendeleo hayo tunayoyaona, na hasa yale ya kutenganisha bunge na serikali kama alivyosema WildCard. Wabunge hao hao tunaowasifia sasa wamejipanga kuleta muswaada wa Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (Constituency Development Fund (CDF)). Inasemekana kwamba mfuko huu utafadhili miradi ya maendeleo majimboni. Sote tunapenda maendeleo. Lakini, utekelezaji wa CDF utasimamiwa na kamati itakayoongozwa na Mbunge wa jimbo husika ambaye atakua mwenyekiti. Utekelezaji wa miradi siyo kazi ya mbunge na inatofautiana na madaraka aliyopewa kikatiba. Hata hivyo, msimamizi anapoingilia utekelazaji, anayemsimamia yeye ni nani?!

Uchaguzi 2010 unakaribia. Huu siyo mfumo wa kurudisha takrima kimya kimya kweli?! Kama kweli bunge ni kielelezo cha ukuaji wa demokrasia, mbona sasa wanataka kuturudisha nyuma?

Baadhi ya wanaharakati tumetoa msimamo wetu (attached), na kutoa tahadhari kwa wawakilishi wetu bungeni kuwa huko wanakotaka kuelekea siyo kuzuri. Tungependa kusikia maoni ya wana-JF na kuibua mjadala kuhusu suala hili.[/FONT][/FONT]
 

Attachments

  • Mfuko wa Majimbo Msimamo wa PF.doc
    362 KB · Views: 126
Kama mtakumbuka ndiye huyu huyu Sitta ambaye hakuona umuhimu wa kuijadili ripoti ya Richmond Bungeni kwa kuwa alikuwa kaalikwa katika chakula USA, na hivyo kuahirisha mpaka baada ya safari yake, wananchi na vyombo vya habari wakaja juu akabadilisha msimamo wake.

Yeye huyu huyu fisadi hakuona umuhimu wa kutafuta muda ili Ngeleja awakilishe recommendations za serikali kuhusiana na utata uliokuwapo kwenye umiliki wa mgodi wa Kiwira na pia hatua zitazochukuliwa dhidi ya mikataba ya madini ambayo Watanzania tumeipigia kelele kwamba haina maslahi yoyote kwa Watanzania. Wanaofaidika ni wageni na mashareholders wengi ambao pia ni wazungu. No, Sipo tayari kukubali uwongo wa Sitta.
 
Inawezekana ana narrow definition ya demokrasia, bunge linaloshindwa kuwakoromea executive mafisadi unaweza kuliita bunge la kidemokrasia? Unaweza kuita bunge la kidemokrasia linalowaadhibu wabunge wanaotumia haki yao kukemea ufisadi? very interesting 6. Unless ndio inaendelezwa ile kutuita wadanganyika.
 
Kama mtakumbuka ndiye huyu huyu Sitta ambaye hakuona umuhimu wa kuijadili ripoti ya Richmond Bungeni kwa kuwa alikuwa kaalikwa katika chakula USA, na hivyo kuahirisha mpaka baada ya safari yake, wananchi na vyombo vya habari wakaja juu akabadilisha msimamo wake.

Yeye huyu huyu fisadi hakuona umuhimu wa kutafuta muda ili Ngeleja awakilishe recommendations za serikali kuhusiana na utata uliokuwapo kwenye umiliki wa mgodi wa Kiwira na pia hatua zitazochukuliwa dhidi ya mikataba ya madini ambayo Watanzania tumeipigia kelele kwamba haina maslahi yoyote kwa Watanzania. Wanaofaidika ni wageni na mashareholders wengi ambao pia ni wazungu. No, Sipo tayari kukubali uwongo wa Sitta.


Si kwamba aliahirisha mpaka atakaporudi? Anyway, unapomnyooshea kidole Sitta mi ntakuacha uendelee kufanya hivyo. All I need to do is to take note.

Ila hapa Sitta anazungumzia ukuaji wa demokrasia, kwa maana ya kwamba kumekuwa na maboresho ukilinganisha ni miaka ya nyuma. Na pia, wewe umemlenga zaidi yeye (Sitta), wakati kinachotajwa ni BUNGE. Sijaona alichoongopa, sorry.



.
 


Si kwamba aliahirisha mpaka atakaporudi? Anyway, unapomnyooshea kidole Sitta mi ntakuacha uendelee kufanya hivyo. All I need to do is to take note.

Ila hapa Sitta anazungumzia ukuaji wa demokrasia, kwa maana ya kwamba kumekuwa na maboresho ukilinganisha ni miaka ya nyuma. Na pia, wewe umemlenga zaidi yeye (Sitta), wakati kinachotajwa ni BUNGE. Sijaona alichoongopa, sorry.



.

Sitta ndiyo spika wa Bunge kwa maneno mengine yeye ndiye msimamizi wa shughuli zote ndani ya Bunge. Anaposema kwamba kuna demokrasia ndani ya Bunge anajifagilia mwenyewe ili Watanzania tumuone kwamba ni mtendaji mzuri, kitu ambacho si kweli. Aliyasema hayo ya kuahirisha mjadala wa ripoti ya Richmond kwamba hauwezi kufanyika mpaka arudi USA. Alipoulizwa si kuna naibu spika akaonyesha kwamba Anna Makinda anaweza kuboronga, hivyo inabidi mjadala umsubiri yeye. Aliahirisha safari yake ya USA baada ya wananchi na wanahabari kuja juu kuhusiana na uamuzi wake. Tuliambiwa kikao cha bunge lililopita Bunge lingeweka moto, lakini hata cheche hatukuziona. Mafisadi bado wanapeta, hatujui kiasi gani kilichorudishwa na mafisadi, hatujui majina ya waliorudisha pesa hizo, hatujui ni nani mmiliki halali wa mgodi wa Kiwira, hatujui chochote kuhusu uchunguzi wa ufisadi wa Rada. Kwa kifupi hakuna jipya lolote tuliloliona kabla na baada ya kikao hicho.Hakuna demokrasi yoyote ile! Demokrasi lazima iambatane na results vinginevyo bado ni bunge uchwara tu.
 
Back
Top Bottom