Bunge jipya lina hali mbaya! Serikali itafanaje kuliokoa Bunge ili kuwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni?

Mkuu Drifter, kwanza asante kwa mchango wako, very objective, kiukweli tangu nimepandisha uzi huu, wewe ndio mtu wa kwanza kunielewa, kwasababu, kiukweli kabisa, hii jf ya sasa, tuna watu wachache sana, wenye kuweza kusoma bandiko na kisha kujiuliza what is the motive behind.

Chama cha Mapinduzi ni chama cha ukweli na haki, kiliasisiwa na Mwalimu Nyerere, mpenda haki na mtenda haki. Baada ya Mwalimu, CCM ilipitia mageuzi na kuishiwa kuhodhiwa na wenye fedha, hivyo kuzalisha kada kubwa ya makada wa CCM ambao ni makada maslahi, na kwenye uchaguzi, wanakuwa wako tayari kutumia mbinu zozote kushinda uchaguzi. JPM alipoingia, amekuja kuibadili CCM kuirudisha ile CCM ya Nyerere. Sasa ndani ya makada wa CCM, kuna makada wa aina mbili, kuna "CCM Die Hard", hawa ndio wanaotaka kuhakikisha CCM inaupondaponda upinzani na kushinda kwa asilimia 99.9% kwa kutumia mbinu zozote.

Tupo sisi makada "Modern CCM" ambao kutokana na good track ya kazi nzuri ya JPM, CCM innashinda kwa mshindi mzuri safi na clear victory, kushinda kwa haki bila kufanya figisu figisu zozote.

Kwa vile Bunge letu ni Bunge la vyama vingi, mimi naamini kuna baadhi ya wana CCM very genuine, hakupenda kuona baadhi ya wapinzani wakishindwa akiwemo mtu kama Zitto!. Lakini kutokana na wapinzani kukataliwa na wananchi, ili Bunge lichangamke, zile kamati 2 za oversight committee, PAC na LAAC, lazima ziongozwe na wabunge wa upinzania ambao ni vichwa vya ukweli, kwenye hao wabunge wote sijaona watu wa kalibre hiyo ndio maana kila siku, tunamuomba Mwenyekiti wetu, JPM, katika zile nafasi zake 10, awateua wapinzani 4, Zitto, JJ Mnyika, Mbatia na kale kabinti Queen Sendiga.

Ili CCM itawale vizuri inahitaji Upinzani makini, ndio maana kila uchao, naibalasa Chadema humu na ACT Zanzibar, waache ujinga wa kususa. Ili kusasa kwa akili ni kususa kama kwa kususa huko utaachieve something, lakini kususa tuu for the sake of kususa, huku you won't achieve anything huu ni ujinga!.

Karibu tena.
P
Swali kwako Pasco utawaleta vipi bungeni wapinga maendeleo?

Pili ukiweka gunzi katikati ya betri tochi itawaka?

Mimi nadhani ni vizuri miaka hii mitano aachiwe Magufuli peke yake na wabunge wake bila gunzi ili tuone maajabu ya maendeleo na tuone kweli wapinzani walikuwa ni kikwazo cha maendeleo.

Natalajia kuiona Mtera kama Oslo Norway
 
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali, Bunge letu jipya linalokwenda kuundwa hivi karibuni baada ya uchaguzi Mkuu, lina hali mbaya sana ya kuwa liko kwenye hati hati ya kutokuwepo kwa kambi rasmi ya upinzani Bungeni.

Swali ni Jee NEC, Rais Dr. Mwinyi na Rais Dr. Magufuli wataingia huruma na kuokoa jahazi kwa kuliokoa Bunge letu la JMT ili liweze kuwa na kambi rasmi ya upinzani Bungeni?.

Declaration of Interest
Japo mimi ni kada wa chama cha siasa, na uchaguzi umekwisha, sasa narejea kwenye zile safu zangu za " Kwa Maslahi ya Taifa", ambazo zinatanguliza uzalendo kwa maslahi ya taifa letu Tanzania, hivyo nakuomba unisome with clear conscious kama mnamsoma Mtanzania mwingine yoyote, lakini kama tayari umeisha ni lebo mimi ni kada na kujiambia kila ninachoandika ni kwa maslahi ya chama changu na sio maslahi ya taifa, nakushauri uishie hapa, maana hata ukiendelea kunisoma with pre conceived opinion, hautaweza kuiona rationale ya bandiko hili.

Na kwa vile hili ndilo bandiko langu la kwanza Jukwaa la Siasa baada ya Uchaguzi, naomba kuchukua fursa hii kumpongeza Rais, Dr. John Pombe Joseph Magufuli kwa ushindi wa kishindo, nakipongeza Chama changu CCM, na kupongeza wote waliodhinda.

Japo ni lengo la kila mwana CCM, kuona chama chake kinashinda viti vyote na kata zote, ila pia kuna baadhi ya wana CCM, ambao ni makada wazalendo zaidi, wamefurahishwa na ushindi wa kishindo wa CCM, ila pia ni wazalendo zaidi kwa nchi kuliko chama, tungependa kuona wapinzani makini wachache wakiingia Bungeni ili kujenga ile dhana ya Bunge la vyama vingi. Hivyo kushindwa kwa mtu kama Zitto ni masikitiko kwa wana CCM wazalendo wengi wa type yangu!. Tunapenda Bunge la CCM, lakini pia lenye mwamko na msisimko wa challenges za upinzani.

Hivyo kwenye kushangilia ushindi, nawasihi viongozi wetu na wana CCM wazalendo wenzangu, tushangilie kwa kiasi, tusiwatambie upinzani, tusiwakejeli, kuwatukana wala kuwabeza, kwasababu nao ni Watanzania wenzetu na wamechaguliwa na Watanzania, ila kura zao hazikutosha, hivyo kwenye hotuba zetu, tupunguze kujimwambafy na badala yake tuongeze humility na kuhutubia hotuba za upendo ku heal na sio za ku hurts ili kuliponya taifa na machungu ya kushindwa na kuliunganisha taifa tuwe na upendo, umoja, mshikamano na ushirikiano kuijenga nchi yetu.

Wapinzani
Asiyekubali kushindwa sio mshindani, uchaguzi umekwisha, aliyeshinda ameshinda kwa haki na kihalali, aliyeshindwa ameshindwa kwa haki na kihalali, kwa kutumia kanuni ya " the end justifies the means", tukubali matokeo, kazi sasa ibaki ni moja tuu, kuijenga nchi yetu kwa kutoa kila aina ya ushirikiano kwa washindi.

Vitabu vya dini zote vinafundisha Wananchi kutii mamlaka halali. Baada ya uchaguzi kumalizika na rais kupatikana na kuapishwa, kile kitendo cha kuapishwa ni kumhalalisha rasmi hivyo baada ya rais Magufuli kuapishwa, sasa yeye ni mamlaka halali, ndiye rais wa JMT, ni rais wa Watanzania wote, waliomchagua, wasio mchagua, hata ambao hawakupiga kura, rais Magufuli ndiye rais wa nchi, tutii mamlaka halali.

Baada ya kuapishwa na kuanza kazi, hakuna kitu kinachoitwa kususa, kutokubali matokeo au kutomtambua rais, huko ni kujifurahisha tuu, kwa sababu tayari rais yupo na ana exist, umtambue, usimtambue, yeye ndio rais wako na yupo kwa ajili yako. Unaweza usimpende, unaweza usimkubali, lakini huwezi kutomtambua!. Hivyo viongozi wa upinzani acheni hadaa za kuwahadaa wafuasi wenu kuwa hamumtambui rais. Rais ni mtu mwenye status of duality.

1. Rais Magufuli ni mtu, ni binadamu, unaweza usimpende, usimkubali na ukakataa kutambua ushindi wake, that is human, kama humpendi mtu, hakuna anayeweza kukulazimisha umpende au umkubali, hilo una uhuru nalo.

2. Rais Magufuli ni Taasisi ya urais, president institution, hii ni mamlaka, hakuna choice ya kuipenda, kuikubali au kuitambua, ipo kisheria hivyo ni lazima uiheshimu, na kuitii mamlaka hii, it's not a matter of choice, its an obligation, ni lazima kuitii mamlaka na usipotii, mamlaka inakushughulikia, ndio maana hata sheria, kutokujua jambo fulani ni kosa kisheria, is not an excuse sheria isi act on you, hivyo hakuna kitu kinachoitwa kutokumtambua rais.

Huo ulikuwa ni utangulizi tuu kuwekana sawa, mada ya leo ni hii.
Kufuatia poor performance ya vyama vya upinzani kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, kwa Watanzania kuvikataa na badala yake kukichagua CCM pekee, but 4!, idadi hiyo haiwezi kutimiza akidi inayotakiwa kuweza kuunda kambi rasmi ya upinzani Bungeni.

Ibara ya 14 ya Kanuni za Bunge zinaeleza
2) Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda Kambi Rasmi ya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabunge wote.
(3) Chama cha Upinzani hakitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni, isipokuwa tu kama kina idadi ya Wabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabunge wote.

Idadi ya Wabunge wote wa Bunge la JMT ni 357, hivyo asilimia 12.5% ni wabunge 44.

Kwa matokeo ya uchaguzi huu, hata baada ya allocation ya wabunge wa viti maalum, idadi hiyo haiwezi kufikiwa, hivyo Bunge lijalo, lina hati hati ya kutokuwa na kambi ya upinzani Bungeni, kambi hii ikikosekana, maana yake, hakutakuwa na serikali kivuli, hivyo bajeti za serikali tuu zitawasilishwa bila maoni ya kambi ya upinzani, jambo ambalo is not healthy kwa Bunge la vyama vingi.

Watu watatu pekee wenye uwezo wa kuokoa jahazi hili, ni
1. Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ikubali kutoa nafasi ya upendeleo kwa viti maalum vya upinzani hata kama hawakukidhi vingezo.
Mfano, maadam sifa ya kupata viti maalum ni chama kupata asilimia 10 ya kura zote, then Tume inaweza kuamua, wale wagombea urais wote waliopata kura zaidi ya asilimia 10%, wote waingie Bungeni.

2. Rais wa Zanzibar, anazo nafasi 10 za uteuzi wa wawakilishi, katika nafasi hizo zote 10, ateue wawakilishi 10 wa vyama vya upinzani, kati ya hao 10, wawakilishi 5, waingie kwenye GNU, na wawakilishi 5 waingie kwenye Bunge la JMT toka Baraza la Wawakilishi. This is a very big sacrifice to make.

3. Rais wa JMT, Dr. John Pombe Joseph Magufuli, na yeye ana nafasi zake za uteuzi wa wabunge 10. Usually lengo la uteuzi huu ni ili rais aweze kupata watu wa kutosha kumsaidia, kwa kuwa mawaziri, lakini kwa line up ya walioshinda CCM, kuna line up ya kushibisha mawaziri wote, na bado akabakiwa na reserve team inayoweza kuunda Baraza la Mawaziri la akiba.

Hivyo kama rais Magufuli akiingia huruma, akaamua kuliokoa Bunge letu tukufu, then na yeye ateue angalau wabunge 6 wa upinzani kuingia Bungeni kwenda kuimarisha upinzani, na rais Magufuli anaweza kuitumia kete hii kupiga ndege wawili kwa jiwe moja.
1. Kuuokoa Upinzani 2. To heal the nation from the election wounds ambazo to some ni very painful na kuna watu wako very bitter!.

Kwa ushauri wangu, napendekeza rais Magufuli awateue hawa wafuatao
1. Tundu Lissu- aligombea nae
2. Zitto Kabwe - Most Interactive MP
3. James Mbatia- Very Compromising
4. Prof Haruna Lipumba - Good Puppeteer
5. JJ.MNYIKA- Mjengaji hoja mzuri
Nafasi tano zilizobaki ni za wanawake, tunamuomba Magufuli amuangazie yule Queen Sendiga miongoni mwa wanawake hao.

Hili likifanyika, litatibu makovu ya uchaguzi Mkuu huu, na kuingiza vichwa vya upinzani ambavyo vitalichangamsha Bunge letu na kuliongezea msisimko.

Hili lusipofanyika, Bunge la chama kimoja, bila any challenges, japo litaharakisha maendeleo bila upinzani, litakosa msisimko na lita bore!.

Kwa kumalizia, namalizia kwa lile swali la msingi, kuwa Bunge jipya lina hali mbaya liko kwenye hati hati ya kutokuwepo kambi rasmi ya upinzani Bungeni.

Swali ni Jee NEC, Rais Dr. Mwinyi na Rais Dr. Magufuli wataingia huruma kuliokoa Bunge letu la JMT ili liweze kuwa na kambi rasmi ya upinzani Bungeni?.

Jibu la swali hili, litapatikana ndani ya kipindi cha wiki moja kuanzia Jumatatu Ijayo.

Nawatakia Jumamosi Njema

Paskali
Rejea za Bunge la Chama Kimoja



AS a Tanzanian foremost : hata bunge lililo pita sikuweza kuona policy alternative zikiwekwa na sisi Wapinzani hata katika maeneo japo ya wizara kivuli nne tuu, acha kusema katika kila wizara kivuli.

This time tuongeze nguvu ya kuimarisha upinzani katika utendaji kazi wake ili waweze kutoa michango yenye uzito kwenye public policy alternative.
 
Makovu kutoka kwa nani? Nani aliwatia vidonda? Pili upinzani walicheleweshaje maendeleo? Ili bungen hoja ipite huamliwa na kura sasa upinzani walichelewesha vipi? Je mbona hayo maendeleo hayakuonekana 1992- ambapo ni ccm watupu
 
Eti NEC iteuwe..Hivi kuna ibara ipi inayoipa mamlaka NEC kuteua yenyewe wabunge?
 
Wanabodi,
Kwa ushauri wangu, napendekeza rais awateue hawa wafuatao
1. Freeman Mbowe- M/Kiti chama kikuu cha upinzani
2. Tundu Lissu- aligombea nae
3. Zitto Kabwe - Most Interactive MP
4. James Mbatia- Very Compromising
5. Prof Haruna Lipumba - Good Puppeteer
6. JJ.MNYIKA- Mjengaji hoja mzuri
Nafasi tano zilizobaki ni za wanawake, tunamuomba Magufuli amuangazie yule Queen Sendiga miongoni mwa wanawake hao.

Hili likifanyika, litatibu makovu ya uchaguzi Mkuu huu, na kuingiza vichwa vya upinzani ambavyo vitalichangamsha Bunge letu na kuliongezea msisimko.

Hili lusipofanyika, Bunge la chama kimoja, bila any challenges, japo litaharakisha maendeleo bila upinzani, litakosa msisimko na lita bore!

Paskali
Rejea za Bunge la Chama Kimoja

1. Uchaguzi 2020 - Japo ni mchungu 'Kumesa' lakini ndio ukweli wenyewe; watakaorudi Bungeni ni 'wa kijani', kubali kataa. Mwenye masikio na asikie!

2. Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je, tunarejea nchi ya chama kimoja?

3. The Economist: Rais Magufuli ametangaza kufuta Upinzani ifikapo 2020 na kuirudisha Tanzania kuwa Nchi ya chama Kimoja
Maadam Mama kaonyesha nia Njema na dhamira Njema, kwenye kulitibu taifa hili, Mnaonaje tukimshauri:, kama ikimpendeza, afanye na hili, na kwa vile saa hizi nafasi zimeisha jazwa anaweza to create at least 2, Mbowe na Zitto, wakaingia!.
Hili mnalionaje?.
P
 
Maadam Mama kaonyesha nia Njema na dhamira Njema, kwenye kulitibu taifa hili, Mnaonaje tukimshauri:, kama ikimpendeza, afanye na hili, na kwa vile saa hizi nafasi zimeisha jazwa anaweza to create at least 2, Mbowe na Zitto, wakaingia!.
Hili mnalionaje?.
P
Waendelee kupindisha Sheria na Katiba?

Haya basi "Akipendezwa"

Wataua Upinzani.
 
Maadam Mama kaonyesha dhamira Njema, ikimpendeza, afanye na hili, na kwa vile saa hizi nafasi zimeisha jazwa anaweza to create at least 2, Mbowe na Zitto, wakaingia!.
Hili mnalionaje?.
P
Awatoe kwanza wale 19 wasio na chama, na wasitetewe wana kesi ipo mahakamani, ile kesi ni ya uongo, ilitengenezwa makusudi ili kuchelewesha suala lao lakini kimsingi hawana haki yoyote, kwani wao hawana tofauti yoyote na wasaliti waliowatangulia wakashughulikiwa kwa taratibu zile zile na chama chao.
 
Awatoe kwanza wale 19 wasio na chama, na wasitetewe wana kesi ipo mahakamani, ile kesi ni ya uongo, ilitengenezwa makusudi ili kuchelewesha suala lao lakini kimsingi hawana haki yoyote, kwani wao hawana tofauti yoyote na wasaliti waliowatangulia wakashughulikiwa kwa taratibu zile zile na chama chao.
Hawezi kuingilia muhimili mwingine kule bungeni Samia hahusiki totally hata hivyo kesi ipo mahakamani japo mahakama yenyewe niyaccm lakini ngoja tuone
 
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali, Bunge letu jipya linalokwenda kuundwa hivi karibuni baada ya uchaguzi Mkuu, lina hali mbaya sana ya kuwa liko kwenye hati hati ya kutokuwepo kwa kambi rasmi ya upinzani Bungeni.

Swali ni Jee NEC, Rais Dr. Mwinyi na Rais Dr. Magufuli wataingia huruma na kuokoa jahazi kwa kuliokoa Bunge letu la JMT ili liweze kuwa na kambi rasmi ya upinzani Bungeni?.

Kwa ushauri wangu, napendekeza rais Magufuli awateue hawa wafuatao
1. Freeman Mbowe- M/Kiti chama kikuu cha upinzani
2. Tundu Lissu- aligombea nae
3. Zitto Kabwe - Most Interactive MP
4. James Mbatia- Very Compromising
5. Prof Haruna Lipumba - Good Puppeteer
6. JJ.MNYIKA- Mjengaji hoja mzuri
Nafasi tano zilizobaki ni za wanawake, tunamuomba Magufuli amuangazie yule Queen Sendiga miongoni mwa wanawake hao.

Hili likifanyika, litatibu makovu ya uchaguzi Mkuu huu, na kuingiza vichwa vya upinzani ambavyo vitalichangamsha Bunge letu na kuliongezea msisimko.

Hili lusipofanyika, Bunge la chama kimoja, bila any challenges, japo litaharakisha maendeleo bila upinzani, litakosa msisimko na lita bore!.
Just imagine vichwa hivi vingekuwa Bungeni leo kungetokea nini kwenye kupitishwa kwa mkataba huu?.

Kati ya mboga ambazo mboga kidogo, unakula ugali mkubwa, ni mboga ya mpenda!. Bunge linapokuwa mlenda, mambo ndio kama hivyo!.
P
 
Wanabodi,

Japo ni lengo la kila mwana CCM, kuona chama chake kinashinda viti vyote na kata zote, ila pia kuna baadhi ya wana CCM, tunaojiita "CCM Contemporary" ambao ni makada wazalendo zaidi kwa nchi kuliko kwa chama, wamefurahishwa na ushindi wa kishindo wa CCM, ila pia ni wazalendo zaidi kwa nchi kuliko chama, tungependa kuona wapinzani makini wachache wakiingia Bungeni ili kuleta a balance of power na kujenga ile dhana ya Bunge la vyama vingi. Hivyo kushindwa kwa mtu kama Zitto ni masikitiko kwa wana CCM wazalendo wengi wa type yangu!. Tunapenda Bunge la CCM, lakini pia lenye mwamko na msisimko wa challenges za upinzani.

1. Kuuokoa Upinzani 2. To heal the nation from the election wounds ambazo to some ni very painful na kuna watu wako very bitter!.

Hili likifanyika, litatibu makovu ya uchaguzi Mkuu huu, na kuingiza vichwa vya upinzani ambavyo vitalichangamsha Bunge letu na kuliongezea msisimko.

Hili lusipofanyika, Bunge la chama kimoja, bila any challenges, japo litaharakisha maendeleo bila upinzani, litakosa msisimko na lita bore!.

Paskali
Sikujua kama kulikuwa kuna vikao vya bunge vikiendelea..

Nimeshangaa sana kumbe kuna bunge, tena kubwa kabisa kuelekea bajeti.

Inashangaza sana.

Hata zile clips kutoka bungeni siku hizi hazipo tena.
Karibu, Bunge jipya lina hali mbaya! Serikali itafanaje kuliokoa Bunge ili kuwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni?
P
 
Back
Top Bottom