Bunge huru la wana JamiiForums: Tathmini ya maisha ya watanzania mwaka 2013!

UNDENIABLE

JF-Expert Member
Feb 26, 2013
2,326
1,314
Salaam waheshimiwa wabunge(wawakilishi wa watanzania)!

Waheshimiwa!
Mjadala huu naleta mbele ya BUNGE HURU LA WANAJAMIIFORUM. Hivyo yeyote atakayechangia au atakayesoma comments namwomba ajivishe cheo cha ubunge(uwakilishi wa watanzania).

Waheshimiwa wabunge!
Yamebaki takribani siku 4 tu tumalize huu mwaka wa 2013 na kuingia mwaka mwingine mpya 2014. Tukiwa kama wadau muhimu sana wa maisha ya taifa la tanzania, naombeni tufanye tathmini fupi fupi sana(tusichoshane na mithread mireeeeefu) kuhusu hali ya maisha ya watanzania mwaka 2013, na pia vipi dalili za mwaka 2014. Tusiache kugusa elimu, afya, uchumi(purchasing power), historia, siasa kwa ujumla wake, utendaji wa serikali ya Tanzania na maendeleo ya watanzania kwa ujumla wake.

Kwenye hii thread usimtaje member(mbunge) mwenzako kama mkuu, bali jivishe/mvishe uheshimiwa. Kwa mfano mimi nitatajwa mh UNDENIABLE badala ya mkuu UNDENIABLE

NB:
Tuweke uchadema na uccm pembeni. Tanzania kwanza vyama baadaye!

Ahsanteni , naomba kuwasilisha
UNDENIABLE

CC: Mzee Mwanakijiji, Pasco



MODS NAOMBENI ILE MICHANGO MIZURI KUTOKA KWA MEMBERS(WABUNGE) ZIUNGANISHWE ZIWE JUU HUKU MWANZONI MWA THREAD. AHSANTENI SANA.
Invisible, @
Paw

Bunge hili litahairishwa tarehe 31.12.2013 saa 6:00 usiku


TAHADHARI:
HURUHISIWI KULETA MAMBO YA CHIT CHAT KWENYE HUU UZI. HAPA NI JUKWAA LA SIASA SIO CHIT CHAT


Kuelekea tathmini ya mwaka 2014. Naomba mnitumie PM kwa yeyote anaetaka kuwa mbunge wa jimbo fulani na chama chake, ama waziri wa wizara fulani. Ahsanteni sana!
 
Mheshimiwa hatuwezi kuweka vyama pembeni kwani kuna vyama ndio vinazidi kutuangamiza kila kukicha hivyo turuhusu tu wa bunge wa vyama vyote tuwawakilishe wananchi wenzetu la sivyo itakuw ngumu kuweka chama kama CCM pembeni kwenye janga hili la Taifa ndg mheshimiwa
 
hali imekuwa ngumu kweli kwa wananchi,maboresho ya huduma mbalimbali za jamii yamefanyika kwa kiwango cha chini ya asilimia 50,huku elimu kwa wanafunzi ikizidi kudorora,tatizo mishahara hewa likishindikana kumalizwa lakini kwa watu kama wabunge hali ni nzuri sana na ya neema kubwa kweli kweli asanteni sana waheshimiwa,hizi sikukuu zimekwangua fedha yote,lkn nafikiri vikao haviko mbali toka sasa
 
Mh: Mimi nalia na swala upandishwaji bei ya bidhaa kiholela bila kujali ongezeko la kipato cha Mtanzania wa kawaida, na tofauti kubwa iliyopo kwa walionacho na wasionacho. Kimsingi serikali tunapoelekea 2014 ingalie mfumo rasilimali ambazo zitapelekea mtanzania wa chini kufaidika na kumpa unafuu wa maisha. Tuombe aman na utulivu na upendo kwa wote bila kuangalia dini, kabila na itikadi za kichama. Nawasilisha
 
Mheshimiwa hatuwezi kuweka vyama pembeni kwani kuna vyama ndio vinazidi kutuangamiza kila kukicha hivyo turuhusu tu wa bunge wa vyama vyote tuwawakilishe wananchi wenzetu la sivyo itakuw ngumu kuweka chama kama CCM pembeni kwenye janga hili la Taifa ndg mheshimiwa
Mh zipuwaa hoja yako imesikilizwa. Endelea mh!
 
Ndugu waheshimiwa tabia za vijana wa kitanzania kubadili wasichana kama nguo ikome na kwa upande wa wasichana kubadili wanaume kama nguo ikome.itungwe sheria iwapo mvulana atakapokutana kimwili na mwanamke basi huyo atakuwa ni mke halali na yeyote atakayebainika anatembea nje ya ndoa apewe adhabu ya miaka 7 jela na viboko 10,vitano akiwa anaingia na vitano akiwa anatoka ili akawaonyeshe watoto wake.
 
hali imekuwa ngumu kweli kwa wananchi,maboresho ya huduma mbalimbali za jamii yamefanyika kwa kiwango cha chini ya asilimia 50,huku elimu kwa wanafunzi ikizidi kudorora,tatizo mishahara hewa likishindikana kumalizwa lakini kwa watu kama wabunge hali ni nzuri sana na ya neema kubwa kweli kweli asanteni sana waheshimiwa,hizi sikukuu zimekwangua fedha yote,lkn nafikiri vikao haviko mbali toka sasa
Mh upo live ujue. Wapiga kura wako wanakutazama na kukusikiliza!
 
hali imekuwa ngumu kweli kwa wananchi,maboresho ya huduma mbalimbali za jamii yamefanyika kwa kiwango cha chini ya asilimia 50,huku elimu kwa wanafunzi ikizidi kudorora,tatizo mishahara hewa likishindikana kumalizwa lakini kwa watu kama wabunge hali ni nzuri sana na ya neema kubwa kweli kweli asanteni sana waheshimiwa,hizi sikukuu zimekwangua fedha yote,lkn nafikiri vikao haviko mbali toka sasa
Mh niggas vikao vya wabunge ni posho ya kawaida tu kama wafanyakazi kwenye taasisi zingne. Wapiga kura wasijeelewa vibaya!
 
Ndugu waheshimiwa tabia za vijana wa kitanzania kubadili wasichana kama nguo ikome na kwa upande wa wasichana kubadili wanaume kama nguo ikome.itungwe sheria iwapo mvulana atakapokutana kimwili na mwanamke basi huyo atakuwa ni mke halali na yeyote atakayebainika anatembea nje ya ndoa apewe adhabu ya miaka 7 jela na viboko 10,vitano akiwa anaingia na vitano akiwa anatoka ili akawaonyeshe watoto wake.
Mh chimbuvu naamini viongozi wa serikali wataliangalia hili
 
Mheshimiwa, wewe ni mdau kwa namna moja ama nyingine! Please wakilisha watanzania wenzako!


Mheshimiwa UNDENIABLE kwa kweli hali si nzuri hata kidogo kwa wanainchi wa wilaya yangu binafsi. Nikigusa upande wa elimu kidogo tu nakwambia Mh ya kwamba huko ni majanga makubwa yatatarajiwa huku tunakoelekea jamani. Shule za kata ni mzigo mkubwa kwa Taifa letu tulipendalo ambalo tunalitarajia kuwa na viongozi bora hapo baadae.
 
Last edited by a moderator:
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom