Bunge huru la wana JamiiForums: Tathmini ya maisha ya watanzania mwaka 2013!

Salaam waheshimiwa wabunge(wawakilishi wa watanzania)!

Waheshimiwa!
Mjadala huu naleta mbele ya BUNGE HURU LA WANAJAMIIFORUM. Hivyo yeyote atakayechangia au atakayesoma comments namwomba ajivishe cheo cha ubunge(uwakilishi wa watanzania).

Waheshimiwa wabunge!
Yamebaki takribani siku 4 tu tumalize huu mwaka wa 2013 na kuingia mwaka mwingine mpya 2014. Tukiwa kama wadau muhimu sana wa maisha ya taifa la tanzania, naombeni tufanye tathmini fupi fupi sana(tusichoshane na mithread mireeeeefu) kuhusu hali ya maisha ya watanzania mwaka 2013, na pia vipi dalili za mwaka 2014. Tusiache kugusa elimu, afya, uchumi(purchasing power), historia, siasa kwa ujumla wake, utendaji wa serikali ya Tanzania na maendeleo ya watanzania kwa ujumla wake.

Kwenye hii thread usimtaje member(mbunge) mwenzako kama mkuu, bali jivishe/mvishe uheshimiwa. Kwa mfano mimi nitatajwa mh UNDENIABLE badala ya mkuu UNDENIABLE

NB:
Tuweke uchadema na uccm pembeni. Tanzania kwanza vyama baadaye!
Kwenye hii thread usimtaje member(mbunge) mwenzako kama mkuu, bali jivishe/mvishe uheshimiwa. Kwa mfano mimi nitatajwa mh UNDENIABLE na sio mkuu UNDENIABLE

Ahsanteni , naomba kuwasilisha
UNDENIABLE

CC: Mzee Mwanakijiji, Pasco

Mh Spika
nashukuru kwa kunipa nafasi nami niseme machache juu ya nini kimejiri 2013 na nini tutegemee 2014.
Mh Spika,yapo mengi mazuri yamefanyika kwa mwaka huu tunaouaga 2013 na kwa mwonekano wa kawaida yataendelea kufanyika ama kutendeka mwaka ujao wa 2014,kama ulivyosema tusichoshane,lakini kiukweli,Nchi yetu inaonyesha kusonga mbele hususani ktk nyanja mbalimbali
1.barabara zinaendelea kupitika na asilimia 78 ya mikoa yetu imeungwanisha kwa rami,
2.Ktk mji wetu mkuu wa kibiashara msongamano wa magari unaendelea kutibiwa kwa kuwepo kwa train na barabara ya magari yaendayo kwa kasi inaonekana kukamilika na angarau tumeonyeshwa basi la mfano wake
3.Mh Spika,kwa sisi wa maeneo ya mito na mabonde,tunaendelea kushukuru baada ya kuona daraja la mto kilombero likifanyiwa kazi na hii itatusaidia sana kupitisha mipunga yetu na kuifikisha sokoni kwa haraka
4.tumeona mkonga wa Taifa,nao umekamilika ingawaje matumizi yake bado hayajaleta unafuu ktk bei za upigaji simu na mitandao,lakini Mh Spika nadhani mwaka 2014 mambo yatakuwa mazuri.
naomba nimalizie dakika zangu 3 zilizobaki kwa kusema kutoa angalizo langu kwa kiti
1.kiti kisimamie haki na kama inawezekana basi haya mapungufu yalionekana mwaka huu tunaoumaliza yasijirudie tena mwaka ujao,
2.tunategemea mwaka ujao,hakutakuwa na operation tokomeza,kuferi kwa vijana wetu hususani hawa wa darasa la 14 na pia mwaka 2014 hatutegemea kupata habari ya wanafunzi wasiojuwa kusoma kupatikana wakiwa kidato cah kwanza,hii ni aibu kwa bunge na kwa kiti pia.
3.tunagemea kuona uwajibikaji zaidi mwaka 2014,hususani kwa serikali,viongozi na wananchi kwa ujumla na mwisho kabisa
4,Mh Spika,ninge penda kuona AZIMIO LA ARUSHA likirudishwa 2014 na kama upo uwezekano mambo yake yawekwe ktk katiba,hii itasaidia sana kuwabana viongozi wanaoficha pesa nje ya Tanzania,viongozi wanaofanya biashara na kujilimbikizia mali na wala rushwa watabanwa kama azimio hili litalejeshwa.
Naomba nisiwachoshe,kwani namwona Mh Pasco kanyoosha kiganya chake juu,nadhani mwenzangu ataongelea zaidi mafanaikio ya KATIBA MPYA kwani hili ni swala nyeti sana na kiukweli sisi kama wabunge ni lazima tujipongeze kwa kulisimamia hili,kwani tumejitahidi kupita kwa wapiga kura wetu na tuliwahamasihsa na kuwapa elimu juu ya katiba na mungu akipenda mwaka 2014 tunaweza kupata katiba mpya.
Naona kengere inagonga kuashiria muda wangu kuisha,nashukuru kwa kunipa nafasi Mh SPIKA
 
Watz tumevurugwa na wanasiasa, sio wafanyakaz wala watendaji serikalin wote wanafanya kaz kisiasa zaidi, hii ndo sababu huduma zote za jamii hapa kwetu ni mbovu. Nashauri ndg watz wenzangu swala la siasa tuwaachie akina mbowe,jk na akina lipumba cc tuchape kazi kwa mujibu wa maadili ya kazi husika.
 
Mh. spika nashukuru kwa kupewa nafasi. Kero kubwa kwangu ni suala la sekta ya elimu kuchezewa na kutothaminiwa. Mara standardization, mara division 5, waalimu kutolipwa stahiki zao. Naomba wizara hii imulikwe.
 
mh! spika mijadala kama hii ni afya katika jamii yetu. naomba kuwe na wabunge wa vyama na majimbo ili watu waeleze kilichofanyika ktk maeneo yao na wale wa upnzan waweze kuikosoa serikal. jinsi ya kuapata hao wabunge/wawakilsh watu wanaweza kujiandkisha ktk forum kwa ID zao vyama na majimbo yao.
 
mh Spika mimi ni mbunge wa kanda ya ziwa moja ya mambo ambayo wananchi wa kanda ya ziwa wangependa sana serikali ilifanye ikibidi hata kwa dharura ni kuimarisha/kujenga upya reli ya kati ili ikiwezekana kuwe na route za kila siku Mwanza-dar, dr-mwanza na kama itawezekana pia uwepo mtandao wa reli utakao unganisha mikoa yote ya tanzania bara tunataka haya kwa sababu ukosefu wa reli umesababisha kupanda kwa kiasi kikubwa kwa gharama za maisha mathalani gharama ya kusafirisha mzigo kwa reli ni kidogo sana ukilinganisha na kisafirisha mzigo huo huo kwa kutumia malori takribanibinafikia mara mbili yake. Mh Spika bidhaa zinapanda sana kwa sababu ya usafirishaji kuwa ghari sana suluhisho la hili tatizo ni ujenzi wa reli mpya kabisaa hii itatusaidia pia katika kutunza barabara pesa ambayo tungetumia kukarabati barabara tungeipeleka kwenye afya au elimu
 
mh! spika mijadala kama hii ni afya katika jamii yetu. naomba kuwe na wabunge wa vyama na majimbo ili watu waeleze kilichofanyika ktk maeneo yao na wale wa upnzan waweze kuikosoa serikal. jinsi ya kuapata hao wabunge/wawakilsh watu wanaweza kujiandkisha ktk forum kwa ID zao vyama na majimbo yao.
Mh tawa wazo zuri sana. Uongozi wa bunge huru la jf litazingatia mapema sana iwezekanavyo. Ahsante sana
 
Kwakweli mh spika kuna waheshimiwa wana taka kuharibu vijana kwa kutaka kuhalilisha gongo.

Naomba muongozo wako ikiwezekana waziri Rose Mayemba ajiuzulu.
 
Last edited by a moderator:
Sasa mh., mimi nimtake mh. raisi ajitahidi kutusaidia kutekeleza ahadi alizozitoa kwa wananchi 2010,kuna hospitali ya rufaa na kuletwa kwa meli mpya mapema sana ili inisaidie mimi kuendelea kuwa mbunge wa pale kwani kuna kijana wa vidole 2 anaonekana kuninyima usingizi na anakubalika sana jimboni mpaka kwa mke wangu, eehe! ukizingatia nilishaapa kuondoka kwa ridhaa yangu.

Naamini mh.rais kupitia kwa 'wapigwe tu' amenisikia
 
Mh. spika nashukuru kwa kupewa nafasi. Kero kubwa kwangu ni suala la sekta ya elimu kuchezewa na kutothaminiwa. Mara standardization, mara division 5, waalimu kutolipwa stahiki zao. Naomba wizara hii imulikwe.
Mh githeri bila shaka hili litazingatiwa na viongozi wahusika katika wizara
 
Me nalia na hali ngumu ya maisha bei za mahitaji zinaongeka kila mwaka,wakati kamshahara kangu kako pale pale,na huku nakamuliwa kodi kama kawa hii hali imesababisha mpaka mpaka ugomvi ndani ya nyumba,
hivi sasa nimeanza kubuni njia ya kujipatia kipato kwa style nyingine kabisa ntaianza tarehe 4 mwezi ujao.
 
Vipi tutakayoongea humu tutalindwa kwa sheria gani maana lazima tuwe na Kinga
 
Mheshimiwa Mwenyekiti mimi naomba watanzania Tuache UVIVU na tuchangamkiew FURSA. Mfano huko Tabora sasa nasikia kuna mafuriko wanachi watumie Fursa hiyo kufanya biashara ya Uvuvi wa MIGEBUKA na KAMBALE kwa wingi.

Pia Nasikia kuna kilio cha ongezeko la Bei ya Umeme. Watu wasilie ni wakati sasa wakutumia Vishoka kwa wingi na Kujichukulia Umeme wa Bure kutoka Tanesco kwani hili ni Shirika lao la UMMA na ni KODI zao hizi.

Mheshimiwa mimi naishia hapa nawatakia Waheshimiwa wengine Sikukuu njema za Mwaka mpya ila nawakumbushe tena kuwa Kila Changamoto na matatizo wayageuze kuwa Fursa na sio Kulialia.
 
Mh Spika
nashukuru kwa kunipa nafasi nami niseme machache juu ya nini kimejiri 2013 na nini tutegemee 2014.
Mh Spika,yapo mengi mazuri yamefanyika kwa mwaka huu tunaouaga 2013 na kwa mwonekano wa kawaida yataendelea kufanyika ama kutendeka mwaka ujao wa 2014,kama ulivyosema tusichoshane,lakini kiukweli,Nchi yetu inaonyesha kusonga mbele hususani ktk nyanja mbalimbali
1.barabara zinaendelea kupitika na asilimia 78 ya mikoa yetu imeungwanisha kwa rami,
2.Ktk mji wetu mkuu wa kibiashara msongamano wa magari unaendelea kutibiwa kwa kuwepo kwa train na barabara ya magari yaendayo kwa kasi inaonekana kukamilika na angarau tumeonyeshwa basi la mfano wake
3.Mh Spika,kwa sisi wa maeneo ya mito na mabonde,tunaendelea kushukuru baada ya kuona daraja la mto kilombero likifanyiwa kazi na hii itatusaidia sana kupitisha mipunga yetu na kuifikisha sokoni kwa haraka
4.tumeona mkonga wa Taifa,nao umekamilika ingawaje matumizi yake bado hayajaleta unafuu ktk bei za upigaji simu na mitandao,lakini Mh Spika nadhani mwaka 2014 mambo yatakuwa mazuri.
naomba nimalizie dakika zangu 3 zilizobaki kwa kusema kutoa angalizo langu kwa kiti
1.kiti kisimamie haki na kama inawezekana basi haya mapungufu yalionekana mwaka huu tunaoumaliza yasijirudie tena mwaka ujao,
2.tunategemea mwaka ujao,hakutakuwa na operation tokomeza,kuferi kwa vijana wetu hususani hawa wa darasa la 14 na pia mwaka 2014 hatutegemea kupata habari ya wanafunzi wasiojuwa kusoma kupatikana wakiwa kidato cah kwanza,hii ni aibu kwa bunge na kwa kiti pia.
3.tunagemea kuona uwajibikaji zaidi mwaka 2014,hususani kwa serikali,viongozi na wananchi kwa ujumla na mwisho kabisa
4,Mh Spika,ninge penda kuona AZIMIO LA ARUSHA likirudishwa 2014 na kama upo uwezekano mambo yake yawekwe ktk katiba,hii itasaidia sana kuwabana viongozi wanaoficha pesa nje ya Tanzania,viongozi wanaofanya biashara na kujilimbikizia mali na wala rushwa watabanwa kama azimio hili litalejeshwa.
Naomba nisiwachoshe,kwani namwona Mh Pasco kanyoosha kiganya chake juu,nadhani mwenzangu ataongelea zaidi mafanaikio ya KATIBA MPYA kwani hili ni swala nyeti sana na kiukweli sisi kama wabunge ni lazima tujipongeze kwa kulisimamia hili,kwani tumejitahidi kupita kwa wapiga kura wetu na tuliwahamasihsa na kuwapa elimu juu ya katiba na mungu akipenda mwaka 2014 tunaweza kupata katiba mpya.
Naona kengere inagonga kuashiria muda wangu kuisha,nashukuru kwa kunipa nafasi Mh SPIKA

Pa pa pa pa pa pa pa pa pa pa pa
 
mh! spika mijadala kama hii ni afya katika jamii yetu. naomba kuwe na wabunge wa vyama na majimbo ili watu waeleze kilichofanyika ktk maeneo yao na wale wa upnzan waweze kuikosoa serikal. jinsi ya kuapata hao wabunge/wawakilsh watu wanaweza kujiandkisha ktk forum kwa ID zao vyama na majimbo yao.

Hahha! Kwa jinsi ni ijuavyo JF CCM humu watakuwa wapinzani.
 
Mheshimiwa UNDENIABLE kwa kweli hali si nzuri hata kidogo kwa wanainchi wa wilaya yangu binafsi. Nikigusa upande wa elimu kidogo tu nakwambia Mh ya kwamba huko ni majanga makubwa yatatarajiwa huku tunakoelekea jamani. Shule za kata ni mzigo mkubwa kwa Taifa letu tulipendalo ambalo tunalitarajia kuwa na viongozi bora hapo baadae.
Ahsante sana mh liverpoolfc
 
Mh spika natumia kanuni ya 68 A naomba kwa ruhusa yako niisome,mbunge anaweza kusimama muda wowote na kuomba mwongozo,Mh engmtolera achukue posho yangu ya leo
 
Last edited by a moderator:
Mheshimiwa Mwenyekiti mimi naomba watanzania Tuache UVIVU na tuchangamkiew FURSA. Mfano huko Tabora sasa nasikia kuna mafuriko wanachi watumie Fursa hiyo kufanya biashara ya Uvuvi wa MIGEBUKA na KAMBALE kwa wingi.

Pia Nasikia kuna kilio cha ongezeko la Bei ya Umeme. Watu wasilie ni wakati sasa wakutumia Vishoka kwa wingi na Kujichukulia Umeme wa Bure kutoka Tanesco kwani hili ni Shirika lao la UMMA na ni KODI zao hizi.

Mheshimiwa mimi naishia hapa nawatakia Waheshimiwa wengine Sikukuu njema za Mwaka mpya ila nawakumbushe tena kuwa Kila Changamoto na matatizo wayageuze kuwa Fursa na sio Kulialia.
Mh kibanga ampiga mkoloni umeanza vizuri lakini sasa unaharibu. Kaa chini mh!
 
Mheshimiwa wananchi wangu wa jimbo la Segerea wana matatizo mengi sana,la kwanza hawana soko maana eneo lao la kujenga soko,mimi nilibadilisha matumiza na kujenga nyumba yangu,mh.wananchi wangu hawana maji kabisa na mengine mengi,serikali iangalie namna ya kuwasaidia.
 
Back
Top Bottom