Bundi aingia ndani ya ukumbi wa Bunge leo asubuhi

japo kuomba kifo kwa mtu sio poa ila ndugai akiumwa nusu kaputi hata miaka 2 itakuwa powa

ajifunze maana ile kuugua mara ya 1 hakupata funzo.
 
Amepita pitaje?? Kwenye nyufa au kwenye kuta??..
Ila kama mdau hapo alivyoelezea, bundi kisayansi wako very sensitive to the smell of dead cells..
Wanasayansi wa wanyama na ndege kupitia vipindi kama Nat Geo Wild wanafanya tafiti deep sana za hawa viumbe wanaotuzunguka na kwa kweli kuna vitu vingi sana muhimu vya kujifunza kupitia wanyama, ndege na hata wadudu.. Natamani tungeweza kuipata hiyo sayansi na vifaa kupata maarifa yaliyo wazi lakini yote kheri..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna kitu kitatokea .

Job Ndugai anaweweseka.
Kulingana na mila katika jamii nyingi za Kiafrika Ndege na Wanyama kama BUNDI au KAKAKUONA hawezi kuonekana ndani ya nyumba au nje ya nyumba kusitokea tukio lolote....huo ni ukweli. Achilia mbali IMANI za Kibinadamu lakini pia kuna ASILI(NATURE) ya viumbe fulani fulani huwa wana namna ya ku-detect kimaumbile matukio fulani kiumbele kuna jambo litatokea...!!!

Mwaka 2004 wakti Tsunami ilipopiga pwani ya SUMATRA unaambiwa hakuna BUNDI wala ndege au mnyama yeyote aliyeangamia isipokuwa wanadamu pekee...!!!Reason: Bundi na ndege wengine walikuwa wame-sense kwa kutumia INSTICT ya kwamba kuna janga linakuja. Lakini pia Uchawi na Ushirikina upo phivo Ndugai aache kujipa moyo kuwa hakuna kitu lazima iko namna kama siyo leo, basi ni kesho au mtondogoo lazima kutokeee kitu...!!
 
Tumepoteza sana ndugu zetu kwa imani kama hizo. Familia ikiwa na mgonjwa na kisha kumuona Bundi basi inakata tamaa badala ya kumpeleka mgonjwa hospitali.
Siyo imani wala nini...inawezekana wazazi wangu walimpeleka hospitali lakini alizidiwa tuu.
 
Unafahamu ni kwa nini Bundi alikaa muda wote huo hapo nyumbani kwenu? Kwa vyovyote vile, Mdogo wako alikuwa mgonjwa sana na hivi alikuwa anatoa Harufu ambayo ninyi haikuwa rahisi kui-detect lakini kwa kuwa Bundi ni very sensitive to smell, basi yeye alikuwa hapo akivizia mawindo akihisi sehemu hiyo kuna mzoga. Vinginevyo,Bundi hana uhusiano wowote na kufariki kwa Mdogo wako.

Kama Bundi ndiye alikuwa anahusika na kifo cha mdogo wenu, ni kwa nini akae hapo wiki nzima? Kama ana uwezo Wa kumchukua mtu au kumfanya afe,kwa nini asubirie muda wote huo?
Mkuu huwa naheshimu sana michango yako humu ila hapa umejibu kijinga na kipuuzi, huwa mimi binafsi siamini sana haya mambo ila nakumbuka nikiwa kijana mdogo bundi alikuja kwetu akakaa juu ya mti kwa siku mbili mfululizo babu yetu kipindi hicho akasema ile sio dalili nzuri.
Siku mbili baadae kaka yetu mkubwa aliyekua safarini Mwanza alipata ajali akafariki. Mambo mengine usijifanye mjuaji waachie wengine na tamaduni zao.
 
Amepita pitaje?? Kwenye nyufa au kwenye kuta??..
Ila kama mdau hapo alivyoelezea, bundi kisayansi wako very sensitive to the smell of dead cells..
Wanasayansi wa wanyama na ndege kupitia vipindi kama Nat Geo Wild wanafanya tafiti deep sana za hawa viumbe wanaotuzunguka na kwa kweli kuna vitu vingi sana muhimu vya kujifunza kupitia wanyama, ndege na hata wadudu.. Natamani tungeweza kuipata hiyo sayansi na vifaa kupata maarifa yaliyo wazi lakini yote kheri..

Sent using Jamii Forums mobile app
We ndio sasa unataka kuwatisha watu zaidi ya kuwafariji. Unataka kumaanisha kuwa tayari ameletwa hapo mjengoni na harufu ya kifo? Ni nani humo bungeni aliyekwisha kuwa na dead cells? Ili ikiwezekana awahishwe India??!!
 
Na akienda tena Apollo lazima arudi ndani ya box kama biscuit

Sent using Jamii Forums mobile app

Hivi huyu Matonya Ndugai anavyo wa-harrass kina Tundu Lissu, Zitto Kabwe, Halima Mdee, Esther Bulaya,kina Mbowe na Esther Matiko kwa maelekezo ya Jiwe ataendelea kubaki salama tu siku zote...????Nakumbuka ule wimbo wa..''Njiwa peleka Salaam. This time ni zamu ya ''Bundi kupeleka salaamu maalum''
 
Nakumbuka japo huwa siamini sana ila hizi mambo zipo...nakumbuka wakat fulan miaka ya 90 hivi kuna siku bundi alikuja akakaa juu ya paa la nyumba usiku kucha akilia. Asubuhi tukaletewa taharifa shemej yetu amefariki...dah! Hizi mambo zipo jamani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bundi ni kawaida yake kurandaranda usiku, lakini mchana si kawaida yake. inampasa mheshimiwa kama ameamua kuamini ushirikina, basi aamini kuwa wa mchana ndio tatizo kuliko wa usiku, maana si kawaida ya bundi kuonekana akirandaranda mchana.
 
Mimi nafikiri kuna kitu bundi anahisi ambacho sisi binadamu hatukioni.
Yeah ndio ilivyo ...wataalamu wanasema kwamba anauwezo mkubwa " wakugundua wakunusa kiasi kwamba never zake huwa zinampatia taarifa Kwamba kiumbe fulani kimepunguza chembe chembe hai mwilini na Muda sio mrefu kitakufa ...so bundi huwa anaenda mpaka karibu na makazi ya hicho kiumbe akitumaini kwamba kikifa anaweza kujipatia mzoga .... kuna thread ambayo imewahi kueleza kwakina kuhusu hilo humu .....

Ila sio kweli kwamba kila wakati ambao bundi huwa anaonekana basi patakuwepo na kiumbe ambacho kitafikwa na umauti

Sent using Jamii Forums mobile app
 
bundi ni ndege anaye ishi kwa kufanya shughuli zake za asili usiku na mchana huwa analala.hivyo huenda hapo bungeni ndiyo makazi yake au ndiyo katafuta makaz


Ni mambo ya kujidhalilisha sana. Mtu kama Ndugai,Spika anayeongoza wasomi Wa kuanzia Darasa la Saba hadi viwango vya PhD na yeye akiwa msomi Mwenye Degree mbili, badala ya kuwaelimisha wabunge kwamba huyo ni ndege kama Njiwa, Popo na kadhalika, yeye anawatoa hofu wabunge kwa kuwaambia kwamba Bundi huyo angalikuja maeneo hayo usiku ndio wangalipaswa kuwa na hofu lakini sio huyo Wa mchana!

Hivi kwa uelewa kama huo,Ndugai anafahamu maana ya kuwa Spika? Kuwa Spika maana yake sio kufahamu tu Kanuni za Binge na Kuunda Kamati za Bunge bali inabidi pia uelewa wake juu ya mambo mengine(General Affairs) uwe mpana sana ama sawa na Wabunge au Zaidi ya wale anaowaongoza.
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom