Bunda: Kundi la Fisi lavamia msiba na kujeruhi waombolezaji

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,500
9,279
Picha

WATU wawili wamenusurika kifo baada ya kushambuliwa na wanyama aina ya fisi wasiojulikana idadi yao baada ya kuvamia kwenye mji uliokuwa na msiba Kijiji cha Kasahunga wilayani Bunda mkoani Mara.

Kwa mujibu wa Daktari wa Hospitali ya Misheni Kibara, Dk Samwel Paul, ambako majeruhi David Robert amelazwa, alithibitisha kupokea majeruhi huyo aliyejeruhiwa sehemu mbalimbali ikiwamo mikono yake.

Naye Muuguzi wa Kituo cha Afya Kasahunga aliyefahamika kwa jina moja la Happy ambako majeruhi mmoja amelazwa, alimtaja majeruhi huyo kuwa ni Elizabeth Mgeta (60), na amejeruhiwa mkono mmoja.

Mashuhuda wa tukio hilo lililotokea saa sita usiku wa kuamkia jana, walidai fisi hao walivamia msibani hapo na kuanza kushambulia waombolezaji waliokuwa wamekaa nje wakisubiri kulala baada ya ibada kuisha.

Katika hatua nyingine, wavuvi wanne wamekufa maji kutokana na mtumbi wao waliokuwa wanavulia samaki kutoboka na kuzama katika ziwa Victoria, eneo la mwalo wa Kibara katika Wilaya ya Bunda mkoani Mara.

Taarifa ya Polisi Mkoa wa Mara ilieleza kuwa mvuvi Doto Mfungo (18) ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Kenkombyo wilayani Bunda alinusurika kifo baada ya kushikilia mtumbwi huo na kupiga kelele za kuomba msaada, ambako wananchi walifika katika eneo hilo na kumuokoa.

Wavuvi waliokufa maji ni Kabenjulilo Magere (17), Godluck Yohana (15), Kaitila Julius (19) na Philipo James (17) ambaye alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kenkombyo aliyefaulu mtihani wa darasa la saba mwaka huu, ambao wote ni wakazi wa Kijiji cha Kenkombyo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Juma Ndaki alithibitisha kutokea kwa tukio hilo usiku wa kuamkia jana saa 7:30. Dakitari wa Hospitali ya Misheni ya Kibara wilayani Bunda, Dk Samwel Paul na muuguzi mmoja wa hospitali hiyo Nurie Mabele, wamethibitisha wavuvi hao kufa maji.
 
Pole zao majeruhi waliovamiwa na mbiti. Hawa watoto kwenye mitumbwi waache kuajiriwa. Sisi tulikija goziba miaka ya nyuma niliishukuru serikali ya halimashauri ya mleba. Maana walitupiliwa mbali kwenda ziwani waliokuwa under 18
 
Pole zao majeruhi waliovamiwa na mbiti. Hawa watoto kwenye mitumbwi waache kuajiriwa. Sisi tulikija goziba miaka ya nyuma niliishukuru serikali ya halimashauri ya mleba. Maana walitupiliwa mbali kwenda ziwani waliokuwa under 18

Goziba nasikia iko kisiwa kuna biashara sana mkuu ..maana mara nyingi zile mitumbwi unakuta zinapakia vitu vingi semitrailer kwa semitrailer
 
Wavuvi waliokufa maji ni Kabenjulilo Magere (17), Godluck Yohana (15), Kaitila Julius (19) na Philipo James (17) ambaye alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kenkombyo aliyefaulu mtihani wa darasa la saba mwaka huu, ambao wote ni wakazi wa Kijiji cha Kenkombyo.

Gone too young aisee, wapumzike kwa amani.
 
Fisi ni hatari aisee akiona weak point anamaliza kazi dk sifuri.. hawajui kuwinda so huwa wanavizia sana wanyonge
Mimi kuna siku gari lilizama kwenye mchanga karibu na Inyonga basi ikabidi nitetembee hadi Kijiji kimoja karibu na Inyonga kwenda kutafuta makoleo

Niliondoka hapo nikijua kuwa kile kijiji hakiko mbali sana kwa hiyo saa12 na nusu nikaaza kutembea kumbuka hiyo ilikuwa 2013 nilitembea huku giza likiingia nikaanza kusikia milio ya fisi lakini sikuwa na wasiwasi

Hofu yangu ilikuwa zaidi kwenye Simba kwa sababu Bastola haiwezi kunisaidia iwapo Simba wangetokea ila nilikuwa najua sauti ya Bastola tu ingewakimbiza nilifika kijijini saa2 za usiku nikapata watu na Majembe ila nikaona si busara kurudi tukasubiri lifti majira ya saa 4 za usiku ikapita Scania ya Bariadi tukapanda mpaka kwenye tukio nikaitoa gari pale hadi Inyohga mjini

Fisi nilikuwa nawachukulia kama wanyama waoga.
 
Kuna mbwa mmoja dume aling'atwaga na fisi mapumbu yote akaondoka nayo aiseee.. By then i was 9 yrs in 1994 nakumbuka hadi leo Arusha huko sisahau.. Ila aliponaga na kuishi hana mapumbu, daah
Daah maskin walimgeuza hanithi 😅😅
 
Maeneo Kama haya ndo wanatakiwa waishi kina Mshana Jr huku mijini na jf wanatutisha tu waende huko wakatishane na fisi vamizi😎
 
Mimi kuna siku gari lilizama kwenye mchanga karibu na Inyonga basi ikabidi nitetembee hadi Kijiji kimoja karibu na Inyonga kwenda kutafuta makoleo

Niliondoka hapo nikijua kuwa kile kijiji hakiko mbali sana kwa hiyo saa12 na nusu nikaaza kutembea kumbuka hiyo ilikuwa 2013 nilitembea huku giza likiingia nikaanza kusikia milio ya fisi lakini sikuwa na wasiwasi

Hofu yangu ilikuwa zaidi kwenye Simba kwa sababu Bastola haiwezi kunisaidia iwapo Simba wangetokea ila nilikuwa najua sauti ya Bastola tu ingewakimbiza nilifika kijijini saa2 za usiku nikapata watu na Majembe ila nikaona si busara kurudi tukasubiri lifti majira ya saa 4 za usiku ikapita Scania ya Bariadi tukapanda mpaka kwenye tukio nikaitoa gari pale hadi Inyohga mjini

Fisi nilikuwa nawachukulia kama wanyama waoga.
Fisi ni very stubborn ving'ang'anizi haswa na hawaogopi kuumia hawatambui hii ni hatari hadi mmoja wao afe ndo wanaona kumbe hii kweli ni hatari
 
Fisi ni very stubborn ving'ang'anizi haswa na hawaogopi kuumia hawatambui hii ni hatari hadi mmoja wao afe ndo wanaona kumbe hii kweli ni hatari
Lakini kumbuka tochi kali inamkimbiza fisi wa kawaida
Ila kwenye nchi zenye Vita fisi wakishazoea kula nyama ya maiti za Binadamu kama ilivyokuwa South Sudan labda hao.
 
Back
Top Bottom