Bulyanhulu: Wachimbaji wadogo wapigwa mabomu walipotaka kuchimba karibu na mgodi wa ACACIA

Hii imetokea siku ya leo asubuhi ambapo baadhi ya wananchi kwenda kuchimba katika eneo la NAMBA 2 ambalo lipo karibu na mgodi wa ACACIA Bulyanhulu wilayani Kahama.

Mamia ya vijana,wazee na akina mama walionekana kumiminika katika eneo hilo na kuanza kuchimba huku wakiimba nyimbo za kumsifu Rais Magufuli kwa maamuzi aliyoyachukua dhidi ya ACACIA! Wananchi hao walisikika wakisema "Haiwezekani kila sie tunapogundua tunafukuzwa eti ni eneo la ACACIA, kumbe nae hana leseni kama sisi, asante Magufuli"!

Wakati wakiendelea na kuchimba gari za POLISI zipatazo tatu zikiwapo na gari za ACACIA zilifika katika eneo hilo na kuanza kupiga mabomu hali ilisababisha na kutawanyika kwa wachimbaji hao.

Kwa mujibu wa polisi wanadai hawaruhusu mtu kuchimba katika eneo hilo kwani ni eneo la mwekezaji!
Huo uchokozi wapigwe tu wananchi wetu wanadanganywa na wenye uwezo wa kukata leseni ili ionekane mwekezaji kawaonea leseni yake ifutwe
 
Nimecheka sana hii ishu,safi sana wananchi huo ndo uzalendo..

Pale kuna mvamizi na sio mwekezaji,
wawaache wananchi wachimbe dhahabu
 
Jana Magu alikua anatafuta public sympath..... na ndio maana ACACIA haitaguswa kamwe na ndio maana wao ACACIA wataendelea kuchimba na kusafirisha dhahabu kama kawaida
 
da huyu siwametutangazia hau lesen wala hajasajiliwa ? Au hatukusikia jana aseee
 
Mwekezaji asiye na leseni..
Km hana leseni ilikuwaje kuwaje mpaka anachimba dhahabu?
Siyo km natetea lkn huu uchafu umebarikiwa na viongozi wa ccm. Acacia itachimba dhahabu siku zote. Wakitaka kukomesha huu upuuzi. Wavunje mikataba.
Hii ni hatari, niliona ujinga wa ccm ktk kula rambi rambi
 
mbona team .......siioni uwanjani hapa? njooni bwana mnachungulia tu na kusepa?
 
Kiukwelii me nahisii anachofanyaa Mzee baba nikurusha rushaa vijimatekee lakini ukwelii anaujuaa yeye mwenyewe na mikatabaa yakee na hao watuu ambayo anaisomea uvunguni mwa kitandaa kwa aibuu. Hao majamaa wanajiamini sababu kilaa kituu wanachoo na walikubalianaa semaa Mzee baba anaonaa geree kwambaa wanafaidii wakat watangulizi wake walikubalii tenaa kwa mikatabaa ya nje ya nchii na bataa refuu. Abonge nao taratibu wakishindwana atumie nguvu kama nikulipishwa tulipeee na hasaraa tupatee yaishee lakini anachofanyaa sahivii watoto wamjini tunaitaa vunga la motemaa nae anatafutaa gap afetue chake atuliee. Haiwezekan wametuibia alafuu unataka majadiliano nawezi wa rasilimal zetu waendeleee kukamuaa tu.
 
Back
Top Bottom