Bulaya,Mdee na wabunge wote wa upinzani msifikirie kabisa suala la kuomba radhi

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Ni wazi wote tunafahamu kuwa hata mtu alieshitakiwa kwa kosa la kuua, kabla ya kuhukumiwa Mahakama hujiridhisha kwanza kama mtuhumiwa ameua kwa kukusudia au laa.

Mimi sio mwanasheria ila sidhani mtu aliemua mwenzake kwa kumpiga na kitu kizito baada ya kutukanwa, kudhalilishwa,n.k anaweza kuhukumiwa kwa kosa la kuua kwa kukusudia kwani ni wazi mtu huyu alikuwa provoked na kwa hasira ndio akajikuta ametenda kosa la mauji.

Tukija kwa wabunge wa upinzani, utaona kabisa mazingira ni haya hayo kwani wanakuwa provoked, tena pengine kwa makusudi, na wabunge wa chama tawala au kutotendewa hakin na kiti ndio kunapelekea wao kukosa uvumilivu na kuonekana wakorofi.

Kwa mtazano wangu,kutokana na mazingira haya ya wao kuchokozwa na wanaowachokoza kutochukuliwa hatua ikiwemo na kiti kutowatendea haki wanayoyafanya ni sahihi kabisa kwasababu hawana namna nyingine ya kupinga huu uonevu na hiyo ndio silaha pekee walionayo maana hawana nguvu kwenye vyombo vyote vya maamuzi vilivyotawaliwa na watu wa chama kimoja hivyo hawana njia mbadala zaidi ya hiyo.

Kwasababu hiyo,nawashauri wabunge waliofungiwa na wabunge wote wa upunzani kutoona haja ya kuoomba rahi bali wachukulie kuwa wako katika mpambano ya kutafuta haki na usawa ndani ya Bunge.

Jambo lingine wanalopaswa kutambua ni kuwa kuomba radhi ni kukiri makosa(kukubali huu uonevu) na zaidi ni kuhalalisha huu uonevu na pia ni kuwapa nguvu wale wanaowachokaza kwa makusudi.

Mandela alikaa jela kwa miaka 27,Lema amekaa mahabusu kwa muda wa miezi 4,yinyi kifungo cha nje cha mwaka mmoja ndio kitawashinda?

Kutokuwepo Bungeni hakuwazuia kuwatumika wananchi wenu kwa asilimia mia moja hivyo pambaneni mkiwa hata nje ya Bunge kuliko uonyonge wa kuomba radhi wakati mule ndani ni wazi hamna haki.
 
Tutaendela kulia milele ikiwa bado katiba ambayo ndio kiongozi mama..iko outdated..
 
Tutaendela kulia milele ikiwa bado katiba ambayo ndio kiongozi mama..iko outdated..
Eti unaonewa alafu tena unaomba radhi!

Unaona kabisa ulikuwa unampigania mwenzako ambae ni wazi alikuwa anaonewa alafu eti uje uombe radhi!!

Hii sio sawa kabisa.
 
Back
Top Bottom