sajo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 2,993
- 5,211
Tarehe 17 Disemba 2020, Mahakama ya Rufaa ya Tanzania katika kikao chake ilichoketi Bukoba, imebatilisha hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania katika kesi ya Mauaji Namba 56 ya 2018 kuwa Mwalimu RESPICIUS PATRICK @ MTANZANGIRA anyongwe mpaka kufa kwa kusababisha kifo cha mwanafunzi SPERIUS EDWARD, aliyedaiwa kufariki dunia kwa kipigo cha viboko.
Mahakama hiyo imebatilisha hukumu hiyo kupitia uamuzi ilioutoa katika Rufaa ya Jinai Namba 70 ya 2019 kwa kuona kuwa wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo, Kifungu namba 265 na kifungu namba 298(1) vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 ya Sheria za Tanzania havikufuatwa ipasavyo na hivyo kufanya mchakato mzima wa usikilizwaji wa kesi kuwa batili.
Vifungu hivyo vinaitaka mahakama Kuu inaposikiliza mashauri ya jinai kuwa na washauri wa mahakama wasiopungua wawili watakaotoa msaada wa kufikia maamuzi katika kesi hiyo kupitia maoni yao (washauri) kwa jaji anayesikiliza kesi. Mahakama ya Rufaa imekubali kuwa wakati wa kusikiliza kesi hiyo, mahakama Kuu chini ya Jaji Mlacha ilikuwa na washauri watatu wa mahakama lakini washauri hawa ambao sio wataalamu wa sheria (lay persons) hawakuelezwa ipasavyo maana ya kesi hiyo na hivyo wakatoa ushauri pasipo kuwa na uelewa wa walichokishauri. Jaji Mwandambo alieleza kuwa, ukiukwaji wa masharti ya vifungu hivyo (hasa cha 295(1)) uliwanyima washauri hao wa mahakama nafasi ya kusikilizwa na kutoa ushauri na hivyo kuifanya kesi hiyo kuwa kama iliyosikilizwa pasipo usaidizi wa washauri wa mahakama jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Mahakama ya Rufaa ya Tanzania baada ya kubaini mapungufu hayo, ikitumia mamlaka iliyopewa kisheria chini ya kifungu cha 4 cha Sheria ya Mamlaka ya Kirufani (AJA) Sura ya 141 Rejeo la 2019 ya kufanya marejeo (Review) kwa kesi mbalimbali, imeibatilisha hukumu hiyo na kuamuru usikilizwaji upya wa kesi hiyo mbele ya Jaji mwingine pamoja na washauri wengine wa mahakama. Hata hivyo, Mahakama hiyo imesema kuwa usikilizwaji huo upya wa kesi hiyo, hautamhusiha mwalimu HERIETH GERALD ambaye aliachiwa huru na Mahakama Kuu ya Tanzania kupitia hukumu ya hesi hiyo ya Mauaji Namba 56 ya 2018. Mwalimu Respicius ataendelewa kushikiliwa wakati akisubiri usikilizwaji upya wa kesi yake. Rufaa hii ilikuwa ikiendeshwa na wakili Remidiues Mbekomize akishirikiana na wakili Aneth Lwiza walimuwakilisha Mrufani na upande wa Serikali uliwakilishwa na mwanasheria mwandamizi wa Serikali, Ngole.
Rejea hapa Respicius Patrick @ Mtanzangira vs Republic (Criminal Appeal No.70 of 2019) [2020] TZCA 1908; (17 December 2020) | Tanzania Legal Information Institute kwa nakala ya uamuzi wa Mahakama ya Rufaa katika Rufaa ya Jinai namba 70 ya 2019
Pia soma hapa Bukoba: Mahakama Kuu yamhukumu kunyongwa hadi kufa Mwalimu aliyemuua mwanafunzi kwa kipigo kwa tafsiri nzuri isiyo rasmi ya Hukumu kwa lugha ya Kiswahili
Mahakama hiyo imebatilisha hukumu hiyo kupitia uamuzi ilioutoa katika Rufaa ya Jinai Namba 70 ya 2019 kwa kuona kuwa wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo, Kifungu namba 265 na kifungu namba 298(1) vya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 ya Sheria za Tanzania havikufuatwa ipasavyo na hivyo kufanya mchakato mzima wa usikilizwaji wa kesi kuwa batili.
Vifungu hivyo vinaitaka mahakama Kuu inaposikiliza mashauri ya jinai kuwa na washauri wa mahakama wasiopungua wawili watakaotoa msaada wa kufikia maamuzi katika kesi hiyo kupitia maoni yao (washauri) kwa jaji anayesikiliza kesi. Mahakama ya Rufaa imekubali kuwa wakati wa kusikiliza kesi hiyo, mahakama Kuu chini ya Jaji Mlacha ilikuwa na washauri watatu wa mahakama lakini washauri hawa ambao sio wataalamu wa sheria (lay persons) hawakuelezwa ipasavyo maana ya kesi hiyo na hivyo wakatoa ushauri pasipo kuwa na uelewa wa walichokishauri. Jaji Mwandambo alieleza kuwa, ukiukwaji wa masharti ya vifungu hivyo (hasa cha 295(1)) uliwanyima washauri hao wa mahakama nafasi ya kusikilizwa na kutoa ushauri na hivyo kuifanya kesi hiyo kuwa kama iliyosikilizwa pasipo usaidizi wa washauri wa mahakama jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Mahakama ya Rufaa ya Tanzania baada ya kubaini mapungufu hayo, ikitumia mamlaka iliyopewa kisheria chini ya kifungu cha 4 cha Sheria ya Mamlaka ya Kirufani (AJA) Sura ya 141 Rejeo la 2019 ya kufanya marejeo (Review) kwa kesi mbalimbali, imeibatilisha hukumu hiyo na kuamuru usikilizwaji upya wa kesi hiyo mbele ya Jaji mwingine pamoja na washauri wengine wa mahakama. Hata hivyo, Mahakama hiyo imesema kuwa usikilizwaji huo upya wa kesi hiyo, hautamhusiha mwalimu HERIETH GERALD ambaye aliachiwa huru na Mahakama Kuu ya Tanzania kupitia hukumu ya hesi hiyo ya Mauaji Namba 56 ya 2018. Mwalimu Respicius ataendelewa kushikiliwa wakati akisubiri usikilizwaji upya wa kesi yake. Rufaa hii ilikuwa ikiendeshwa na wakili Remidiues Mbekomize akishirikiana na wakili Aneth Lwiza walimuwakilisha Mrufani na upande wa Serikali uliwakilishwa na mwanasheria mwandamizi wa Serikali, Ngole.
Rejea hapa Respicius Patrick @ Mtanzangira vs Republic (Criminal Appeal No.70 of 2019) [2020] TZCA 1908; (17 December 2020) | Tanzania Legal Information Institute kwa nakala ya uamuzi wa Mahakama ya Rufaa katika Rufaa ya Jinai namba 70 ya 2019
Pia soma hapa Bukoba: Mahakama Kuu yamhukumu kunyongwa hadi kufa Mwalimu aliyemuua mwanafunzi kwa kipigo kwa tafsiri nzuri isiyo rasmi ya Hukumu kwa lugha ya Kiswahili