figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,491
- 54,884
BWANA harusi aliyekimbiwa na bibi harusi, Omary Mohamed, amesema baada ya tukio hilo amelazimika kudai fedha zake za mahari ili aweze kuendelea na maisha yake.
Akizungumza na MTANZANIA jana, Omary alisema kwa sasa hawezi kusema lolote zaidi ya kusubiri kulipwa fedha zake madai ambayo ameyawasilisha kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kilungule Manispaa ya Ubungo.
“Kwa sasa hatua ninayosubiri ni kulipwa fedha zangu. Na muda huu nipo nyumbani kwangu Buguruni Mtaa wa Ghana, lakini unanihoji badala hata kunitumia hata hela ya kahawa,” alisema kwa kifupi Omary.
Kauli ya bwana harusi huyo inatokana na tukio lililotokea juzi baada ya bibi harusi mtarajiwa aliyefahamika kwa jina la Asha Mohamed mkazi wa Kilungule Wilaya ya Ubungo kumkimbia bwana harusi na mshenga wake wakiwa wamepigwa butwaa.
Tukio hilo lilitokea saa 7 mchana jana ambapo bwana harusi mtarajiwa aliachwa …..
Akizungumza na MTANZANIA jana, Omary alisema kwa sasa hawezi kusema lolote zaidi ya kusubiri kulipwa fedha zake madai ambayo ameyawasilisha kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kilungule Manispaa ya Ubungo.
“Kwa sasa hatua ninayosubiri ni kulipwa fedha zangu. Na muda huu nipo nyumbani kwangu Buguruni Mtaa wa Ghana, lakini unanihoji badala hata kunitumia hata hela ya kahawa,” alisema kwa kifupi Omary.
Kauli ya bwana harusi huyo inatokana na tukio lililotokea juzi baada ya bibi harusi mtarajiwa aliyefahamika kwa jina la Asha Mohamed mkazi wa Kilungule Wilaya ya Ubungo kumkimbia bwana harusi na mshenga wake wakiwa wamepigwa butwaa.
Tukio hilo lilitokea saa 7 mchana jana ambapo bwana harusi mtarajiwa aliachwa …..