mwalimally
Member
- Apr 23, 2010
- 21
- 1
Nimetumiwa email na mdada mmoja akitaka nione kwa jinsi gani sisi wanaume tunawaumiza wake zetu. Yeye ameipata kutoka katika blogu moja ya kitanzania. Wadau tumshauri huyu dada katika hili lililomsibu.........
Mimi ni mdada wa miaka 28 nimeolewa na ndoa yangu ina mwaka 1. Nilianza kuishi na huyu mume wangu kabla ya kufunga ndoa ila kwa wakati huo tayari alikuwa ameshajitambulisha na mipango ya mahari na ndoa ilikuwa inaendelea.
Dada hii siku sitaisahahu maishani mwangu, ilikuwa wiki 2 kabla ya mahari nilipogundua mume wangu anatembea na housegirl wetu ambae alikua akitusaidia kazi ndogo ndogo pale tunapokwenda kazini.
Iliniuma sana nilipombana msichana akaniambia ukweli wote na kuniomba msamaha. Nilimsamehe ila nikamwambia aondoke ili inisaidie kusahau machungu na kuniwezesha kuendelea na mipango ya kufunga ndoa.
Nilitamani kusitisha mipango yote lakini ningewezaje kuiambia familia yangu ambao tayari walikuwa busy na maandalizi ya mahari na vikao vya harusi? tuliongea na mume wangu na akaniomba msamaha nikamsamehe nikijua atajirekebisha na kama ni ujana labda ataacha tukishaoana.
Tulifunga ndoa salama na maisha yakaendelea kama kawaida bila tatizo. Baada ya miezi 6 nikagundua mume wangu ana mwanamke mwingine this time sio yule house girl tena ila alikuwa ni binti umri wa mdogo wangu wa mwisho ambaye amezaliwa 1988!! Sikuona haja ya kugombana na mtoto mdogo kama huyu ila nilimpigia simu nikaongea nae friendly tu nikijifanya kama ni dada wa bwana wake (mume wangu).
Baada ya kujua kila kitu ndio nikamwambi yule binti kwamba HUYO BWANA WAKE NI MUME WANGU WA NDOA. Yule msichana alishtuka na kuniomba tuonane ili ahakikishe, kweli nilikwenda hadi kwao na picha za harusi ndio binti na mama yake wakaamini.
Akaniomba msamaha kwamba yeye hakujua kwa sababu huyo mwanaume alimwambia yeye ni bachelor na pia hakumtajia jina la ukweli na alikua akivua Pete kila wanapoonana. Baada ya wiki moja mume wangu aligundua nimeonana na mwanamke wake na aliponiuliza sikumficha nilimueleza ukweli na nilivosikitishwa na hiyo tabia.
Kwa mara nyingine aliniomba msamaha kama kawaida yetu wanawake, nilimsamehe ili kuiokoa ndoa yetu changa. Maisha yakaendelea ila haikupita hata miezi 3 nikaona mwenzangu amebadilika tabia, kuyachunguza zaidi nikagundua kwamba bado wanaendelea na yule msichana na worse enough ameanzisha mahusiano mengine na ex-girlfriend wa rafiki yake.
Dada hapo ndio nimezidi kuchanganyikiwa naiona ndoa chungu! Sikuishia hapo nikaamua kuongea nae kwamba tabia anayofanya sijaipenda this time alikuwa mkali na kusema kwamba nisimuingilie kwenye life style yake kwasababu kila kitu amenipa na mimi ndio mke wake hao vimada niwaache kama walivyo.
Dada ni kweli huyu mwanaume amenipa kila kitu hadi gari la kifahari ameninunulia na pesa za matumizi sio tatizo kwake yaani nakula ninachotaka navaa ninachotaka lakini tatizo langu kubwa sio pesa wala chakula na wala sio wivu kama wengi watavodhania bali sina uhakika kama huyu mwanaume ananipenda kweli au la??
Pia mwenzangu haogopi magonjwa na kila nikijaribu kuongea nae kuhusu magonjwa hanielewi, je nifanyeje?? naogopa kupeleka hili swala kwa wazazi nahisi kama ni mapema mno kuanza vikao vya mashitaka ukizingatia ndio kwanza tuna mwaka mmoja na bado nampenda mume wangu ila simuamini tena.
nisaidieni nifanye nini?
ni mimi dada B wa DSM.
Mimi ni mdada wa miaka 28 nimeolewa na ndoa yangu ina mwaka 1. Nilianza kuishi na huyu mume wangu kabla ya kufunga ndoa ila kwa wakati huo tayari alikuwa ameshajitambulisha na mipango ya mahari na ndoa ilikuwa inaendelea.
Dada hii siku sitaisahahu maishani mwangu, ilikuwa wiki 2 kabla ya mahari nilipogundua mume wangu anatembea na housegirl wetu ambae alikua akitusaidia kazi ndogo ndogo pale tunapokwenda kazini.
Iliniuma sana nilipombana msichana akaniambia ukweli wote na kuniomba msamaha. Nilimsamehe ila nikamwambia aondoke ili inisaidie kusahau machungu na kuniwezesha kuendelea na mipango ya kufunga ndoa.
Nilitamani kusitisha mipango yote lakini ningewezaje kuiambia familia yangu ambao tayari walikuwa busy na maandalizi ya mahari na vikao vya harusi? tuliongea na mume wangu na akaniomba msamaha nikamsamehe nikijua atajirekebisha na kama ni ujana labda ataacha tukishaoana.
Tulifunga ndoa salama na maisha yakaendelea kama kawaida bila tatizo. Baada ya miezi 6 nikagundua mume wangu ana mwanamke mwingine this time sio yule house girl tena ila alikuwa ni binti umri wa mdogo wangu wa mwisho ambaye amezaliwa 1988!! Sikuona haja ya kugombana na mtoto mdogo kama huyu ila nilimpigia simu nikaongea nae friendly tu nikijifanya kama ni dada wa bwana wake (mume wangu).
Baada ya kujua kila kitu ndio nikamwambi yule binti kwamba HUYO BWANA WAKE NI MUME WANGU WA NDOA. Yule msichana alishtuka na kuniomba tuonane ili ahakikishe, kweli nilikwenda hadi kwao na picha za harusi ndio binti na mama yake wakaamini.
Akaniomba msamaha kwamba yeye hakujua kwa sababu huyo mwanaume alimwambia yeye ni bachelor na pia hakumtajia jina la ukweli na alikua akivua Pete kila wanapoonana. Baada ya wiki moja mume wangu aligundua nimeonana na mwanamke wake na aliponiuliza sikumficha nilimueleza ukweli na nilivosikitishwa na hiyo tabia.
Kwa mara nyingine aliniomba msamaha kama kawaida yetu wanawake, nilimsamehe ili kuiokoa ndoa yetu changa. Maisha yakaendelea ila haikupita hata miezi 3 nikaona mwenzangu amebadilika tabia, kuyachunguza zaidi nikagundua kwamba bado wanaendelea na yule msichana na worse enough ameanzisha mahusiano mengine na ex-girlfriend wa rafiki yake.
Dada hapo ndio nimezidi kuchanganyikiwa naiona ndoa chungu! Sikuishia hapo nikaamua kuongea nae kwamba tabia anayofanya sijaipenda this time alikuwa mkali na kusema kwamba nisimuingilie kwenye life style yake kwasababu kila kitu amenipa na mimi ndio mke wake hao vimada niwaache kama walivyo.
Dada ni kweli huyu mwanaume amenipa kila kitu hadi gari la kifahari ameninunulia na pesa za matumizi sio tatizo kwake yaani nakula ninachotaka navaa ninachotaka lakini tatizo langu kubwa sio pesa wala chakula na wala sio wivu kama wengi watavodhania bali sina uhakika kama huyu mwanaume ananipenda kweli au la??
Pia mwenzangu haogopi magonjwa na kila nikijaribu kuongea nae kuhusu magonjwa hanielewi, je nifanyeje?? naogopa kupeleka hili swala kwa wazazi nahisi kama ni mapema mno kuanza vikao vya mashitaka ukizingatia ndio kwanza tuna mwaka mmoja na bado nampenda mume wangu ila simuamini tena.
nisaidieni nifanye nini?
ni mimi dada B wa DSM.