Haaaaa.....
Kaaa nae tu, kama mtoto wako!!!! Wacha fikra za kumfukuza.... Cijuw umefikiriaje??? Naaapa kwa Mungu na kukuombea tena kwa Yesu na Mohammad (SAW) usirudie tena hayo mawazo....
Usimfukuze hata kidogo.
Huyu ni kaka yako, na yanayomsibu ni mtihani tu, mmetoka tumbo moja, jifikirie ingekuwa ni wewe badala ya yeye ungependa kufukuzwa na kunyanyaswa? Inabidi umuenzi na kumheshimu na mapungufu yake yote.
Utamfukuza leo hujui ya kesho.
Huyu ni kaka yangu kabisa, mama mmoja baba mmoja. Ana miaka 38 na kabla ya kuzaliwa mimi, walizaliwa kaka na dada zangu wengine 2, hivyo mimi ni mdogo wake wa 3, na hapo unaweza kujua tumepishana umri kiasi gani!
Haileweki. Alimaliza form akafeli. Wazazi walimlazimisha shule akakataa kata kata. Akawa anashinda anazurura na kufanya kazi za udalali huku akiishi kwa sisi wadogo zake. Alikuwa anakaa kwa kaka zangu mwanzo, akawa na tabia za ulevi wa kupindukia na kuiba vitu vidgo vidogo na kusumbua shemeji zake. Tumemkalisha vikao na kumuonya kashindwa kubadili tabia.
Kila mtu alimchoka tukaamua kumuacha na kuanza kuishi maisha kama chokoraa! Nilimuonea huruma, nikamchukua akae nyumbani kwangu. Nilijaribu kumfungulia miradi ikafa kwa maana ni muhongaji mzuri wa wanawake! Nilimpa hela aenda driving, na kupata leseni ili nifanyie mpango kazini kwangu akala hela zote na leseni hakupata. Niliamua kumtafutia leseni kwa juhudi zangu na kumpeleka akawe dereva kwenye kampuni moja kubwa ya kusafirisha mizigo, akaishia kutumia magari kubebea vimwana. Akafukuzwa kazi
Sasa kaanza tabia ya udokozi wa vitu vya ndani na kuuza na kuleta wanawake huku akiwadanganya kuwa nyumba na usafiri wangu vyote ni vyake, ila kaamua kuniachia mdogo wake. Na sasa kuna msichana wake kanitumia meseji eti kwa nini nang'ang'ania nyumba na usafiri wa kaka badala ya kujitafutia maisha yangu mwenyewe! Thats is to say, hata wasichana wake wanaamini kuwa mimi ndo ninaishi kwa kaka! Wananisumbua, eti nawabana! - Sijui wana upeo mdogo kiasi gani!
Sasa mtu kama huyu hasaidiki, nitampeleka wapi? Nampiga chini leo leo. Namfukuzia mbali! Nimechoka!
Naomba ushauri!
HorsePower
Wewe umemdekeza huyo ndugu yako. Ungemtimua muda mrefu sahivi akili ingekuwa imemkaa sawa na si ajabu angekuwa na maendeleo.
halafu wewe nakutafuta sana.....upo?.....
jamani wewe ulipotelea wapi? Unanitafuta unilipe lile deni langu eeh? Lol.
maana naona tunapishana milango tu....lile ntakulipa wala usijali..lol...
vipi kama ingekuwa ni wewe ndiyo horsepower...ungemtiulia mbali huyo nduguyo sio?
haya, tuweke kambi hapa ili tusipishane. Lol.
Unajua edson, mara nyingine inabidi kufanya maamuzi magumu hasa kama unaona yataleta manufaa. Umeshaona watu ambao wametimuliwa kwao au kwa ndugu waliokuwa wanaishi nao? Wale watu hupata akili za maisha, anajua lazima ajibidiishe. Ningekuwa HP ningemtimua ila si kwa sababu simpendi, kwa kufanya hivyo ningempa opportunity ya yeye kuyajua maisha na kukabiliana nayo.
kuna post moj huko nimeelza kuwa mimi nilimtimua kaka yangu mtoto wa mama mkubwa.....ilikuwa kama hivi ilivyotokea kwa horse power....mimi nilimfukuza..huwezi amini husy jamaa aliondoa hata picha yangu ukutani na kuweka ya kwake...akawa anaaambia mademu zake kuwa hpo ni kwake....nilichukia sana niliprudi...nimekaa nae zaidi ya mara 5 kumuonya aache tabia hiyo lakini jamaa hasikii...kusimamia miradi hawezi kazi yake i kujitangaza kwa mabinti na kunywa pombe....uvumilivu ulipofika kikomo nilimtimua vibaya sana.....
Huyu ni kaka yangu kabisa, mama mmoja baba mmoja. Ana miaka 38 na kabla ya kuzaliwa mimi, walizaliwa kaka na dada zangu wengine 2, hivyo mimi ni mdogo wake wa 3, na hapo unaweza kujua tumepishana umri kiasi gani!
Haileweki. Alimaliza form akafeli. Wazazi walimlazimisha shule akakataa kata kata. Akawa anashinda anazurura na kufanya kazi za udalali huku akiishi kwa sisi wadogo zake. Alikuwa anakaa kwa kaka zangu mwanzo, akawa na tabia za ulevi wa kupindukia na kuiba vitu vidgo vidogo na kusumbua shemeji zake. Tumemkalisha vikao na kumuonya kashindwa kubadili tabia.
Kila mtu alimchoka tukaamua kumuacha na kuanza kuishi maisha kama chokoraa! Nilimuonea huruma, nikamchukua akae nyumbani kwangu. Nilijaribu kumfungulia miradi ikafa kwa maana ni muhongaji mzuri wa wanawake! Nilimpa hela aenda driving, na kupata leseni ili nifanyie mpango kazini kwangu akala hela zote na leseni hakupata. Niliamua kumtafutia leseni kwa juhudi zangu na kumpeleka akawe dereva kwenye kampuni moja kubwa ya kusafirisha mizigo, akaishia kutumia magari kubebea vimwana. Akafukuzwa kazi
Sasa kaanza tabia ya udokozi wa vitu vya ndani na kuuza na kuleta wanawake huku akiwadanganya kuwa nyumba na usafiri wangu vyote ni vyake, ila kaamua kuniachia mdogo wake. Na sasa kuna msichana wake kanitumia meseji eti kwa nini nang'ang'ania nyumba na usafiri wa kaka badala ya kujitafutia maisha yangu mwenyewe! Thats is to say, hata wasichana wake wanaamini kuwa mimi ndo ninaishi kwa kaka! Wananisumbua, eti nawabana! - Sijui wana upeo mdogo kiasi gani!
Sasa mtu kama huyu hasaidiki, nitampeleka wapi? Nampiga chini leo leo. Namfukuzia mbali! Nimechoka!
Naomba ushauri!
HorsePower
ukiona zigo umelibeba halibebeki unalitua. Acha jamii ikuone mbaya ila mungu anajua ulijitahidi vya kutosha.
Mambo yako vipi lakini?. (tushachangia topic inatosha). Lol.