Bring back our ajira

prucho

Member
Jul 22, 2016
39
94
Bring back our ajira.
Hatutaki mchezo na maslahi yetu binafc tumepoteza muda wa miaka kumi na nane mnatuhakikishia ajira zitatoka baada ya zoezi la uhakiki baadae mnaghairi.

Bring back our ajira we mwenyewe ndo ulitusainia vyeti vyetu vya art unavyovihita sanaa Leo mnatuona wa kazi gani? Kwann hujavikata kipindi kile unavisaini?

Bring back our ajira kwenye kampeni za kisiasa sisi mnaotuita Leo wasanii ndo tumewaweka madarakani na wengine kujitolea kufanya kampeni kwa Rais wetu wa wanyonge badala ya wa elimu,elimu,elimu alafu Leo unatugeuka?

Bring back our ajira hivi mnajua tungeazia certificate tungekuwa walimu wa primary tangu 2012 au tungechukua diploma tungeajiriwa toka 2015

Bring back our ajira unataka kutuaminisha hii nchi haipendi wasomi wa shahada,hii serikali haina haja nasisi?
Bring back our ajira hivi hamjui uchungu wa mwana, mnajua jamii inayotuzunguka inavyotucheka? Tunavyodharaurika hadi na walioishia form four wanatuona wajinga?

Bring back our ajira ,mnajua shida za upungufu wa walimu zilivyotapakaa Tanzania hizo data mnazitoa wapi? au mmeamua kumpelekea Rais wa wanyonge data hewa ?

Bring back our ajira sisi nao ni kama machinga, ni kama wale walionyanganywa ardhi yao Kule shinyanga,ni kama mama ntilie wanaonyasaswa kwa kodi bring back our ajira.
Nitoe wito kwa Rais wetu wa wanyonge aangalie kilio hiki tumesomea kufundisha walimu 30,000 tulioko huku tukiachwa hivi tukaanza kuandaa lesson plan kwenye vichwa vya watu hatutakuwa na asubuhi tena.

Bring back our, tumedhalilishwa tumeonenewa ,chama chetu cha mapinduzi hakiusiki katika hili Bali ni wateule wachache ambao hawajui ugumu wa kuoomba na kutafuta kura.

Bring back our ajira.
Na Mwl.Pasaka Rucho.
0756231744.
 
Bring back our ajira kwenye kampeni za kisiasa sisi mnaotuita Leo wasanii ndo tumewaweka madarakani na wengine kujitolea kufanya kampeni kwa Rais wetu wa wanyonge badala ya wa elimu,elimu,elimu alafu Leo unatugeuka?
kama hayo ndio maamuzi uliyofanya basi sawa, kwa hiyo ajira ukipewa pia utasahau muda wote uliokaa nyumbani na kuendelea kuwa mfuasi wa JPM?. kila la kheri kuweni wavumilivu labda serikali ya "wanyonge" ina plan B kuhusu walimu wa arts.
 
Kumbe chama chenu hakihusiki basi twendeni sawa

Mtoa mada acha kulia lia,walimu wa arts wako wengi na kinachofanyika ni reallocation ili kila shule ipate na sio walimu 70 shule moja yenye vidato vinne

Mkiajiriwa huko mtaenda kufanya nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom