Brigedia Jenerali Mbuge: Wazabuni wanakwamisha miradi ya SUMA JKT

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Jul 31, 2017
1,606
1,956
1.jpg

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) nchini Brigedia Jenerali Charles Mbuge amesema kuwa baadhi ya wazabuni wanaouza vifaa vya ujenzi wamekuwa wakiuza vifaa kwa bei ya juu na kuchelewesha vifaa hivyo pale vinapohitajika, jambo linalopelekea baadhi ya miradi inayotekelezwa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi hilo (SUMA JKT) kutokamilika kwa wakati.

Brigedia Jenerali Mbuge ameyasema hayo Februari 13, 2020 mjini Bariadi wakati akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya ujenzi inayotekelezwa na SUMA JKT mkoani Simiyu.

Ameongeza kuwa katika kukabiliana na changamoto hiyo, Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limejipanga kuanzisha maduka ya vifaa vya Ujenzi vitakavyouzwa kwa bei ya jumla ili kuwezesha upatikanaji wa vifaa kwa urahisi, haraka na kwa bei nafuu ikilinganishwa na wazabuni wengine.

“Tatizo moja ninaloliona kwenye utekelezaji wa miradi ni vifaa kuuzwa kwa bei ya juu sana na kucheleweshwa, tumeamua kuwa na maduka ya vifaa ya jumla; tutatoa maelekezo kwa wakuu wa kanda za ujenzi watatupatia mahitaji yao, ili kuwawezesha kufanya kazi kwa wakati kama tunavyokubaliana na washitiri wetu,” alisema Brigedia Jenerali Mbuge.
 
Kila kitu kitakuwa kinafanywa na idara za serikali/taasisi. Logic ya kutoa kazi kwa watu binafsi ni kuwawezesha na kutoa fursa na ajira kutoa mfuko wa huku hela na kuweka mfuko wa huku mzunguko utakuwa mdogo. Zaidi Taneps na kuweka being elekezi isiyovuka mipaka na kushirikisha wadau itasaidia.
 
Acheni sekta binafsi inufaike aisee. Kila kitu mnataka mfanye nyie tu. Mnaingiza hela huku mnatolea kule inaenda BOT, faida yote inarudi serikalini. Kila watu wafanye mambo majeshi yabobee kwenye masuala yahusihanayo na hayo. Wananchi wafanye biashara.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani hata sijui hawa watu wanawaza nini!! mnauwa uchumi wa nchi wanamaliza sector binafsi taratibu wakidhani wanaokoa pesa wakati ndio wanauwa kila kitu. Utajiri unaletwa na watu sio serikali.

Hii tabia ya kutumia Suma JKT ifike mwisho au wajisajili kama kampuni washindane na makampuni mengine kwa zabuni sio unapewa tender bila ushindani ni makosa. Mimi ni lofa sina interest wala sina hata duka lakini kwa mwendo huu tuanuwa kila zuri. pesa lazima iende kwenye mzunguko kampuni zitapata, watu watapata ajira, wauzaji watapata na wasambazaji watapata na katika chain hiyo wengi watakula wataenda kununua kwa wengine ndio maana ya uchumi. Kwa hali hii hatutafika mbali.
 
Mashirika mengi yanayojaribu kumiliki the all supply chain yenyewe huwa yanakosa ufanisi sijuI the case with SUMA JKT ila majeshi yetu siku hz yanawasomi wazuri hope hili walishalifanyia research.
 
Msiwasingizie wazabuni kuwa wanakwamisha miradi wakati nyie ndio hamuwalipi kwa wakati. Mnapoletewa mchanga, vifusi, matofali au vifaa vingine vya ujenzi hamlipi huku mkitaka mzabuni aendelee kuleta vifaa kwa gharama zake na hata mkija kulipa mnatoa fedha kidogokidogo!

Kitu hicho kimewafanya hata wakandarasi wa Kichina kuiga tabia hiyo mbaya ambayo inasababisha wazabuni wa Kitanzania wengi kufilisika kwani wanafanya kazi katika mazingira magumu sana
 
Msiwasingizie wazabuni kuwa wanakwamisha miradi wakati nyie ndio hamuwalipi kwa wakati. Mnapoletewa mchanga, vifusi, matofali au vifaa vingine vya ujenzi hamlipi huku mkitaka mzabuni aendelee kuleta vifaa kwa gharama zake na hata mkija kulipa mnatoa fedha kidogokidogo!

Kitu hicho kimewafanya hata wakandarasi wa Kichina kuiga tabia hiyo mbaya ambayo inasababisha wazabuni wa Kitanzania wengi kufilisika kwani wanafanya kazi katika mazingira magumu sana
Ujumbe umfikie Brigedia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao SUMA wao ndo wanachelewesha hela za hao wazabuni, kukwamnishana wanakuanzisha wenyewe

Sent using Jamii Forums mobile app
I hope na huko watakako kuwa wananunia votu kwa ajili ya madika yao ya jumla iwe vieandani aunpopote wtakuwa wakiwalipa kwa wakati vinginevyo ucheleweshaji utakuwa uko pale pale

Ukitaka kuletewa kwa wakati unatakiwa kulipa pia kwa wakati
Mfano mtu unatakiwa u supply chakula mashuleni unachukua mkopo benki ili uweze hiyp tenda riba kule inspabda serikali ulio supply hawalipi kwa wakati wanakwambia endelea tu kuleta haiwezekani
Biashara Ni ku supply kwa wakati na kulipwa kwa wakati vinginevyo hiyo sio biashara Ni biashara kichaa
 
Back
Top Bottom