Brent Renaud: Mwandishi wa Marekani auawa kwa kushambuliwa Ukraine

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,005
9,872
Mwandishi wa Habari wa Marekani anayefanya kazi nchini Ukraine ameuawa kwa kupigwa risasi katika mji wa Irpin, nje ya Kyiv, polisi wamesema.

Brent Renaud, mwenye umri wa miaka 50, alikuwa mwandishi wa habari na mtengenezaji wa filamu ambaye alikuwa akifanya kazi katika eneo hilo kwa muda sasa.

Mkuu wa Polisi wa Kyiv, Andriy Nebytov amesema kuwa alilengwa na wanajeshi wa Urusi. Waandishi wengine wawili walijeruhiwa na kupelekwa hospitali.

Ni kifo cha kwanza kuripotiwa cha mwandishi wa habari wa kigeni aliyeripoti vita nchini Ukraine.

Mmoja wa waandishi wa habari aliyejeruhiwa, Juan Arredondo, alimwambia mwandishi wa habari wa Italia kwamba alikuwa na Renaud wakati waliposhambuliwa.

"Tulikuwa kwenye moja ya madaraja huko Irpin, tukienda kupiga picha za wakimbizi waliokuwa wanaondoka, na tukaingia kwenye gari," alisema katika video iliyochapishwa kwenye Twitter.

"Kuna mtu alijitolea kutupeleka kwenye daraja lingine na tulivuka kituo cha ukaguzi, kabla ya kuanza kutufyatulia risasi. Kwa hivyo dereva akageuza, waliendelea kupiga risasi; Tulikuwa sisi wawili. Rafiki yangu Brent Renaud, akapigwa risasi ... nilishuhudia akipigwa risasi shingoni", alisema.

1647242952892.gif
 
Rais wa ukraine atafanya juu chini US na NATO washiriki hii vita ila hataki kukubali kaingizwa mkenge.

halafu hajui makubaliano yaliyowekwa 1990 kat bush n rais wa russia kipindi kile, kwa kifupi NATO kavunja mikataba mingi na kwa hili ni vita kbisa.

kwanza mrusi kalipua kambi iliyopo ukraine kilimita 25 kwenda poland yaan mpakani ili wasipokee silaha milio imefika mpaka poland

mziki wa mrussi hauko kwenye media operatio ilyoko kule c muda kitaelweka.

BBC, CNN ni waongo sana tizameni WION ya india mtajua ukweli au aljazeera angalau.
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Niliona habari ya mtengeneza movie aliyeenda ukraine mliweka hapa last week.
Yeye yupo hai bado?
 
Mwandishi wa Habari wa Marekani anayefanya kazi nchini Ukraine ameuawa kwa kupigwa risasi katika mji wa Irpin, nje ya Kyiv, polisi wamesema.

Brent Renaud, mwenye umri wa miaka 50, alikuwa mwandishi wa habari na mtengenezaji wa filamu ambaye alikuwa akifanya kazi katika eneo hilo kwa muda sasa.

Mkuu wa Polisi wa Kyiv, Andriy Nebytov amesema kuwa alilengwa na wanajeshi wa Urusi. Waandishi wengine wawili walijeruhiwa na kupelekwa hospitali.

Ni kifo cha kwanza kuripotiwa cha mwandishi wa habari wa kigeni aliyeripoti vita nchini Ukraine.

Mmoja wa waandishi wa habari aliyejeruhiwa, Juan Arredondo, alimwambia mwandishi wa habari wa Italia kwamba alikuwa na Renaud wakati waliposhambuliwa.

"Tulikuwa kwenye moja ya madaraja huko Irpin, tukienda kupiga picha za wakimbizi waliokuwa wanaondoka, na tukaingia kwenye gari," alisema katika video iliyochapishwa kwenye Twitter.

"Kuna mtu alijitolea kutupeleka kwenye daraja lingine na tulivuka kituo cha ukaguzi, kabla ya kuanza kutufyatulia risasi. Kwa hivyo dereva akageuza, waliendelea kupiga risasi; Tulikuwa sisi wawili. Rafiki yangu Brent Renaud, akapigwa risasi ... nilishuhudia akipigwa risasi shingoni", alisema.

View attachment 2149786
Jasusi kwa kivuli cha uandishi wa habari na film maker
 
jasus akashtukiwa kala bullets.mzee.wa 900 inapendeza alinusulika kula bullets.kazuga kwa warusi kuanzisha taasisi ya kuuza madawa wakamshtukia.
 
Rais wa ukraine atafanya juu chini US na NATO washiriki hii vita ila hataki kukubali kaingizwa mkenge.

halafu hajui makubaliano yaliyowekwa 1990 kat bush n rais wa russia kipindi kile, kwa kifupi NATO kavunja mikataba mingi na kwa hili ni vita kbisa.

kwanza mrusi kalipua kambi iliyopo ukraine kilimita 25 kwenda poland yaan mpakani ili wasipokee silaha milio imefika mpaka poland

mziki wa mrussi hauko kwenye media operatio ilyoko kule c muda kitaelweka.

BBC, CNN ni waongo sana tizameni WION ya india mtajua ukweli au aljazeera angalau.
Mwisho ungemaluzia urus kaomba msaada wa silaha na fedha kutoka china
 
Back
Top Bottom