BREAKING NEWZ: ALI KIBA kortini baada ya kusema uongo hadharani!

sundoka

JF-Expert Member
Oct 9, 2011
2,067
2,751
BREAKING NEWZ:

ALI KIBA kortini baada ya kusema uongo hadharani!

Mamlaka ya mapata tanzania PCCB imesema magari yote yanayoingizwa nchini yakalipie ushuru mara moja katika ofisi ya EWURA.
Akiongea afisini kwake, Mwendesha mashitaka mkuu wa serikali, amesema twiga huyo alikamatwa kwenye box kubwa tayari kusafishwa nje ya nchi kwa ndege maalum kwenda nchini kinyume na sheria ya mahusiano ya mwenye nyumba na wapangaji ya mwaka 1986. Aidha, aliwataka wananchi wa mkoa huo kuwa watulivu katika kipindi hiki uchunguzi unapoendelea. Katika mahojiano hayo, msemaji wa TFF alifafanua kuwa Sammata ameitoa kimasomaso Tamzania, na kuongeza kuwa, kupungua kwa maji katika bwawa la mtera kunaongeza uwezekano wa kamati maalumu ya bunge kufanya uchunguzi katika vitalu vya uwindaji kwenye pori hilo. Aliongeza kuwa, bandari ya Dar es Salaam kulindwa na jeshi la polisi.
Ikumbukwe kuwa, hapo awali, ndege hizo zilikuwa zikifanya safari mara tatu kwa wiki toka Tanzania kwenda Sudan. Alipohojiwa juu ya tatizo la maji kukatika mara kwa mara, msemaji wa bendi hiyo alisema wananchi wote wamezuiliwa kusafiri nje ya nchi kwa sababu za kiusalama na kuwa, tatizo hilo linashughulikiwa na msajili wa vizazi na vifo katika chuo kikuu Ardhi.

Wakati huo huo, mrakibu mkuu wa serikali amewaonya wakazi wa mkoa wa Kusini Pemaba kutokunywa maji mengi kwani huenda wakageuka wazungu. Zikiwa zimebaki siku tatu ili zoezi hilo likamilike, wananchi wameombwa kuwa watulivu ili kuongeza pato ghafi la taifa. Mkurugenzi wa wilaya ya Namtumbo alipotafutwa kwa njia ya simu ili alitolee ufafanuzi swala hilo hakuwa akipatikana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom