Taarifa zinazojiri hivi sasa ni kuwa ule mpambano wa Simba na Yanga leo upo hatarini kuakhirishwa baada ya kutokea utata kwenye tiketi za mchezo huo. Utata huo umesababishwa na viongozi wa Yanga kwa kuweka muhuri wenye aya za Quran na kupelekea wanaharakati na viongozi wa Kiislam kutaka ziondolewa mara moja kwani tiketi hizo hizo upande wa pili zinatangaza pombe.
Shirikisho la soka Tanzania ( TFF ) kwa kushirikiana na vilabu hivi viwili walikubaliana kila timu iweke alama katika tiketi ili kuepusha uwezakano wa kughushi tiketi. Simba wakaweka alama yao lakini viongozi wa Yanga wakaamua kuweka alama ya mojawapo ya sura ktk quran tukufu na kupelekea mtafaruku huo ulioanza jana.
Hadi wakati tukienda mitamboni nusu ya tiketi zilikuwa zimeshauzwa na waislam wametangaza leo kwenda kufanya fujo uwanja wa taifa kama tiketi hizo zitatumika.
Kwa upande wao Bakwata nao wametoa tamko kutaka mechi hiyo iakhirishwe na tiketi zingine zitengenezwe.
Akiongea na mwandishi wetu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Imani Madega amekiri kweli wameweka aya za quran tukufu kwenye tiketi lakini amedai wamefanya hivyo kwa nia njema kabisa kuwafanya wanaofoji tiketi waone vibaya kufoji mpaka quran tukufu.
Wakuu habari ndio hiyo! kandambili washalikoroga....
Shirikisho la soka Tanzania ( TFF ) kwa kushirikiana na vilabu hivi viwili walikubaliana kila timu iweke alama katika tiketi ili kuepusha uwezakano wa kughushi tiketi. Simba wakaweka alama yao lakini viongozi wa Yanga wakaamua kuweka alama ya mojawapo ya sura ktk quran tukufu na kupelekea mtafaruku huo ulioanza jana.
Hadi wakati tukienda mitamboni nusu ya tiketi zilikuwa zimeshauzwa na waislam wametangaza leo kwenda kufanya fujo uwanja wa taifa kama tiketi hizo zitatumika.
Kwa upande wao Bakwata nao wametoa tamko kutaka mechi hiyo iakhirishwe na tiketi zingine zitengenezwe.
Akiongea na mwandishi wetu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga Imani Madega amekiri kweli wameweka aya za quran tukufu kwenye tiketi lakini amedai wamefanya hivyo kwa nia njema kabisa kuwafanya wanaofoji tiketi waone vibaya kufoji mpaka quran tukufu.
Wakuu habari ndio hiyo! kandambili washalikoroga....