Haya yametokea pia duce,hapo wanafunzi wakiandamana kuelekea getini kuzuia magari yanayotoka mbagala-kawe na mwenge kushinikiza ombi lao!kama kawa
Haya yametokea pia duce,hapo wanafunzi wakiandamana kuelekea getini kuzuia magari yanayotoka mbagala-kawe na mwenge kushinikiza ombi lao!
duce yametoka asubuhi hii mpaka sasa bado watu wanaendelea na maandamano ila polis wamefika pale barabaran na mawashawasha!Ya duce ni lini yalitokea?
Hivi sasa mji wa Iringa unazizima
kwa maandamano ya wanachuo
kikuu kishiriki cha Mkwawa
kwenda kwa mkuu wa mkoa kisa
hawajaingiziwa fedha zao,HII NI
HAKI KWELI WAKATI MAMILIONI YA
KODI ZETU YANALIWA NA
WACHACHE SERIKALINI?
hii serikali ya ajabu sana huku UDOM inabidi hela tuingiziwe alhamisi ijayo tarehe3/5,lakini hadi leo kwa utaratibu wa siku hizi hadi tusaini fomu,na ipite hata wiki mbili baada ya kusaini,mpaka leo hakuna hata dalili za kusaini
Haya mambo yanasikitisha,kuna dr. moja wa mkwawa ni rafiki yangu, juzi aliniambia kuwa wanafunzi wa mkwawa wana hali mbaya ya kiuchumi kiasi kwamba wana shindia mapera. aliniambia kua alikutana na wanafunzi wake wakiwa chini ya mti wa mapera akawapongeza kwa utulivu na ku discus,wakamwambia "ticha yani hapa sio kwamba tuna discus ila hu mti wa mpera unatusaidia sana maana hatuna hata hela ya chakula muda wa week sasa hivyo tuna kula mapera kama lunch"huyo dr.aliniambia kuwa kwa hali hii lazima wanafunzi watagoma. Na kweli wamegoma. Ama kweli serikali sikivu.