Wikiliki
JF-Expert Member
- Dec 20, 2010
- 528
- 139
Ndugu wana jf nipo katika hospitali ya mkoa wa Arusha Mt. Meru ambapo wamelazwa majeruhi wa maandamano ya jana. Nimelazimika kufika hapa hospitali baada ya kusikia malalamiko mtaani kuwa majeruhi hao wananyanyaswa na hawapati huduma. Baada yakufika hapa nimejionea mwenyewe hali ni mbaya majeruhi wamejilalia bila huduma na ndugu zao wasema wanapodai huduma wanaambiwa kwa dharau ni nani aliwaambia waende kwenye maandamano. Kwa taarifa za hapa hospitali waliokufa ni watu watatu ila bado kuna majeruhi wenye hali mbaya sana.