break down

mandilo

Member
Sep 28, 2007
14
11
jamani ilikua siku ya jumamosi nikitokea kigamboni nakakatiza mitaa ya forodhani nikaona duka zuri la sylver nikaamua kupaki gari na kwenda kuangalia maana nilitaka kununua kitu,
nilipofika ndani ya duka kabla sijafanya chochote mwenye duka akaniambia dada kaondoe gari yako pale maana watu wa break down watakuja kuifungia gari yangu maana that was a wrong parking!!!! nikauliza mbona kibao hakuna?na mbona magari mengine mengi yamepaki?? hawakujibu...saa hiyohiyo nikageuka ili kurudi kwenye gari nikawakuta mijibaba mizima ikishuka kwa kasi ya ajabu kuja kilifunga gari yangu na nikasikia watu waliokua jirani na hapo wakiwaambia kua mnafunga la nini wakati mwenyewe yuko hapa na gari si bovu, mimi nakataka jiingie ndani ya gari ili nikitoe lakini kuna mbaba akanizuia ili wenzie wafunge gari yangu kwa kusimama kwenye mlango wa gari yangu na kuzizuia akijua fika mimi ni msichana na mdogo kwa umri na umbo na sina nguvu kama zake, nikiangalia kwa macho yangu wakilifunga gari yangu nikiwepo hapo hapo..... na mbaya zaidi eti walitaka niwepe elfu 40 au nikalipie elf 65 ofisini kwao!!!! wakamaliza wakaondoka nikabaki sina la kufanya nimeduwaa roho ikiniuma nikifikiria hiyo hela kwanza ntaitoa wapi asubui hile ....ikanibidi nipige simu na kuomba msaada wa pesa ili nikalipe elf 65 kwenye ofisi yao... yani walifunga gari yangu tuu mengine ya serikali na binafsi hawakuyagusa na kumbe nasikia walikua wananiona na walijua ni mwanamke nitawapa pesa.........mimi bora nitome elf 65 kuliko kuwapa wape mbwa hata shilingi mia yangu jamani changieni mliowai kukutana na zile kero za break down maana ...............
 
Pole sana mdada ,kwenye vifungu vya usalama barabarani ikiwa ni pamoja na parking layout wanaweza wakawa right.Usikimbilie kulipa hiyo hela kwanza.waambie wakuchoree map na kosa lako lipo wapi.U can sue them ,kwa sababu walitumia nguvu na ukatili.Ilishawahi kunitokea.
 
Ile video ya YouTube hata millardayo aliiweka kwenye page yake ambayo Mayor aliiongelea vipi sio kuwa ndio lilikuwa jibu LA kadhia hii? Kwakuwa unamiliki gari jaribu itafute YouTube au kwa millardayo uisikilize inaweza kuja kuwa msaada next time ukikamatwa maana mayor alisema Kuna ndani ya dk 60 hutakiwi kupigwa cheni. Ilisambaa sana kipindi Malima kakamatwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom