Bravo! A very good decision

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Varsity bans ethnic groups

By Pius Rugonzibwa
THE CITIZEN

The University of Dar es salaam (UDSM), recently marred by student riots over alleged administrative flaws, has banned all social and ethnic associations at the institution with immediate effect.

A memo issued to students through their organisation Daruso and signed by university dean of students Dr Martha Qorro said such associations were organs that weakened unity.

The dean cited ethnic conflicts in neighbouring countries saying such problems could not be allowed to grow among students of different ethnic backgrounds at institutions of higher learning.

There is need to encourage students to join associations that cut across the majority of students with more diverse interests rather than cling to district, regional or geographic associations.

Students at UDSM come from heterogeneous societies and any association falling short of this should not be encouraged, read part of the memo.

Tribal associations and ethnic identifications are very common especially during student government elections. The groupings are normally used as fora for by aspiring student leaders to woo voters from their own home areas.

However, has also not been uncommon to have student politics degenerate into chaos, especially when they are shaped along tribal lines.

Dr Qorro said the decision to ban tribal associations at UDSM was passed by the university council on March 13 this year, following concerns over growing disunity among students.

Students have welcomed the move, dismissing speculation that it had to do with last week's riots.

Daruso president Deo Daudi said students had initiated the move to de-register ethnic groupings.

Meanwhile, the student body's presidential elections were reportedly going on peacefully. A new student government is expected to be announced soon.
 
The University of Dar es salaam (UDSM), recently marred by student riots over alleged administrative flaws, has banned all social and ethnic associations at the institution with immediate effect.

What's wrong with the social associations? Having banned these, which type of associations are now permitted?

The administration should also seriously address what they seem to regard as mere allegations, that they do have flaws, or else the whole imbroglio will repeat itself notwithstanding the banning.
 
This is TOUGH!!!

To a certain extent, I agree with the move maana makundi makundi ya kikabila hasa kwa kizazi hiki sidhani kama yanahitajika, especialy kama yanatumiwa vibaya. Lakini, wakati mwingine yanafaa katika kuendeleza utamaduni, kama hiyo ndio nia yake. But where do we draw the line



____________________
 
What's wrong with the social associations? Having banned these, which type of associations are now permitted?

The administration should also seriously address what they seem to regard as mere allegations, that they do have flaws, or else the whole imbroglio will repeat itself notwithstanding the banning.

You don't know the problem of tribalism!?
Ask Wahutu and Watusi in Rwanda or Burundi.
 
You don't know the problem of tribalism!?
Ask Wahutu and Watusi in Rwanda or Burundi.

The University of Dar es salaam (UDSM), recently marred by student riots over alleged administrative flaws, has banned all social and ethnic associations at the institution with immediate effect.

Mkuu! Basi uwe unazisoma kabla ya kuzitundika! Wenyewe wamesema wanapiga marufuku 'social' NA 'ethnic' associations, vitu viwili tofauti. Mimi sikuulizia 'ethnic associations', nimeulizia 'social associations'. Sasa 'tribalism' kwenye social imeingia wapi? Ninavyoelewa mimi ethnicity ndiyo inayohusiana na tribalism wala sio social. Ingawa mimi ni Fundi Mchundo mwenye elimu duni lakini usidhani ni punguani!
 
Mkuu! Basi uwe unazisoma kabla ya kuzitundika! Wenyewe wamesema wanapiga marufuku 'social' NA 'ethnic' associations, vitu viwili tofauti. Mimi sikuulizia 'ethnic associations', nimeulizia 'social associations'. Sasa 'tribalism' kwenye social imeingia wapi? Ninavyoelewa mimi ethnicity ndiyo inayohusiana na tribalism wala sio social. Ingawa mimi ni Fundi Mchundo mwenye elimu duni lakini usidhani ni punguani!

Dr Qorro said the decision to ban tribal associations at UDSM was passed by the university council on March 13 this year, following concerns over growing disunity among students. Social Associations sometimes they don't have any different as compared to ethnic associations.

Mfano mmoja Chama cha Watoto wa vingunge, sisemi kwamba kulikuwa na chama kama hiki, lakini huko nyuma kulishakuwa na hill club ambapo baadhi ya wanafunzi walitengwa katika chama hicho kwa sababu tu hawakuwa na 'status' inayokubalika kuwa mwanachama wa hiyo Hill Club.

Vyuoni ni sehemu ambapo Watanzania toka kila kona ya nchi wanatakiwa wafahamiane zaidi na kujenga urafiki labda wa kudumu. Panapokuwa na jinsi yoyote ile inayosababisha kujenga uadui kwa sababu baadhi ya wanafunzi wanatengwa na wenzao kwa sababu moja au nyingine ikiwemo hiyo ya NA associations basi hizo NA associations zimepoteza mwelekeo na hazistahili kuruhusiwa kuendelea kuweko ndani ya vyuo vyetu.


You see now Mkuu!
 
Dr Qorro said the decision to ban tribal associations at UDSM was passed by the university council on March 13 this year, following concerns over growing disunity among students. Social Associations sometimes they don't have any different as compared to ethnic associations.

Mfano mmoja Chama cha Watoto wa vingunge, sisemi kwamba kulikuwa na chama kama hiki, lakini huko nyuma kulishakuwa na hill club ambapo baadhi ya wanafunzi walitengwa katika chama hicho kwa sababu tu hawakuwa na 'status' inayokubalika kuwa mwanachama wa hiyo Hill Club.

Vyuoni ni sehemu ambapo Watanzania toka kila kona ya nchi wanatakiwa wafahamiane zaidi na kujenga urafiki labda wa kudumu. Panapokuwa na jinsi yoyote ile inayosababisha kujenga uadui kwa sababu baadhi ya wanafunzi wanatengwa na wenzao kwa sababu moja au nyingine ikiwemo hiyo ya NA associations basi hizo NA associations zimepoteza mwelekeo na hazistahili kuruhusiwa kuendelea kuweko ndani ya vyuo vyetu.


You see now Mkuu!

Mkuu, haya ni maelezo ya ziada ambayo mimi nisingeyajua. Soma ulichobandika na utaona kuwa Qorro amezungumzia Social na Ethnic associations! Mimi nilijibu ulichobandika na si haya maelezo ya ziada ambayo hayakuwepo. Unapoteleza, Mkuu, uungwana ni kukiri na sio kutafuta visingizio! nakuwekea tena paragraph ya kwanza ya yale uliyoyabandika kujengea hoja yangu.

By Pius Rugonzibwa
THE CITIZEN

The University of Dar es salaam (UDSM), recently marred by student riots over alleged administrative flaws, has banned all social and ethnic associations at the institution with immediate effect.

A memo issued to students through their organisation Daruso and signed by university dean of students Dr Martha Qorro said such associations were organs that weakened unity.

Social associations zina wigo mkubwa kuliko hizo ethnic associations. Social associations zinaweza kuhusu upenzi wa burudani, mashairi, kusaidia wasiojiweza,mazingira na kadhalika. Msingi ni interest katika social issues. Ethnic associations mara zote ziko based kwenye ethnicity ambayo ni aidha ukabila, rangi au utaifa. hivi ni vitu viwili tofauti. hauwezi ku'ban' social associations kwa kusingizia kuwa zinaweza kuwa tribalised! Basi ban associations zote maana zote zina uwezekano wa kuwa tribalised! Association yeyote inaweza kutumiwa kwa maovu au mabaya.Jawabu si ku wholesale ban, bali ni kuvi'ban' vile tu vinavyoonekana vinamuelekeo mbaya!

Associations zote zina criteria ya nani wanataka awe mwanachama. Associations zote kwa misingi hiyo ni za kibaguzi (exclusive). hauwezi kudai association zote lazima ziwe wazi kwa wote maana ndiyo mwanzo wa kupoteza maana ya hao walioamua kujiunga kutokana na kukubaliana kimtazamo. Kama watoto wa vingunge wakianzisha association yao kuna tatizo gani? Badala ya watoto wa walala hoi ambao ni wengi kushindania kuingia humo ambako bila shaka masharti ya kila mmoja kuwa ni SUV hawatayaweza, kwa nini wasianzishe ya kwao ambayo itwaunganisha wale wote wanaopanda daladala! Shida iko wapi?
 
Na wasiishie kutoa notice tu, wafuatilie kuhakikisha kuwa vikundi hivyo vinatoweka kabisa
 
Thank you MN! Sidhani kama uongozi wa chuo umekurupuka tu na kufanya maamuzi hayo. Wameangalia trends mbali mbali hapo chuoni na pia kusikia toka kwa baadhi ya wanafunzi na kufikia uamuzi wa kuzipiga marufuku hivyo vikundi vya kikabila na visivyokuwa vya kikabila.
 
..ningependa kujua sababu zilizopelekea kuanzishwa kwa hivyo vyama vya KIKABILA. kuna uwezekano kabisa society at large imeshindwa kukidhi mahitaji na matarajio fulani kiasi kwamba wananchi wanakimbilia kwenye vyama vya kikabila.

..miaka ya zamani kulikuwa na vyama vya maendeleo vya kikabila. serikali ikavipiga vita kwamba havina msingi. lakini wananchi walipoona serikali imeshindwa ktk jukumu lake la kuchochea maendeleo vyama hivyo vikaibuka tena miaka ya 1990.

..vilevile huu uamuzi haujaingilia haki za msingi za kiraia za wanafunzi? je, kuna kipingele chochote cha sheria za UDSM ambacho kimekiukwa?

..pamoja na ukabila kuna fukuto lingine la UDINI. sasa sijui kama jumuiya za kidini nazo zitapigwa marufuku.

..kwa maoni yangu huu UMOJA wa WATANZANIA ni DIS-FUNCTIONAL. sababu hiyo ndiyo inayovipandisha chati vyama vya kikabila.

NB:

..labda serikali nayo iige mfano wa UDSM kwa kupiga marufuku mijumuiko ya kikabila/kiwilaya/kimikoa etc.

..shughuli kama fund-raising kwa ajili ya maendeleo ni za kikabila. viongozi wa serikali huhudhuria shughuli hizo na kuchangia.
 
Huto tuvyama katika ngazi ya University si muhimu sana kwa kuwa hata hao wahusika wenyewe sidhani kama wanaona manufaa zaidi ya mikakati ya kubebana katika chaguzi zao...Definately yaweza kuleta some feelings za tribalism...
 
Uamuzi huu wa kupiga marufuku vyama vya kikabila ni mzuri sana ingawa naona wamechelewa kuufanya. Miaka 10 iliyopita nilialikwa kama mgeni kwenye chama cha wajomba zangu wachaga watu wa Hai. Bibi mzaa baba anatokea Kimashuku, ndio ujomba nilio nao na wachaga. Sasa nilishangaa hoja walizokuwa wanajadili, mojawapo ilikuwa je watu wa Narumu nao wakubaliwe kwenye hicho chama au wasikubaliwe? Ukisikia hoja zilizokuwa zinatolewa za kuwakataa hao wenzao wa Narumu (ambako ni eneo hilohilo la Hai) utapata kichefuchefu! Baadae nilikuja kusikia vilitengenezwa vyama vya watu wa Masama, Siha, Machame, nk (kwa mazingira niliyoyaona mle ndani siku ile nilijua umoja ule ungekuwa shida tupu, maana hoja zilikuwa za kitenganishi na kibaguzi tu!) Na katika sherehe ya chama kingine cha kikabila cha pale mlimani (ilifanyika nje ya chuo), mmoja wa waalikwa ambaye alikuwa ofisa mwenye nafasi muhimu serikalini alipopewa nafasi ya kusalimia "wanandugu" au "homeboys" alitumia fursa hiyo kutaja idadi ya watu wa kabila hilo aliowapatia nafasi mbalimbali kupitia ofisi yake, na kuwachagiza wenzie kufuata mfano huo huku akisema "tupendane jamani!" Alitaja hata fursa nyingine zilizoko kwenye mamlaka yake na kuwataka watu wawahi kumuona naye atajitahidi kusaidia kama alivyosaidia wengine! Sasa hii ni nini kama si ukabila wa kutisha sana? Hongereni UDSM kwa uamuzi huu, lakini fuatilieni, kwani bado vinaweza hivi vyama vya kikabila kuendelea kufanya mambo yao clandestinely.
 
Kithuku,

..bila kuwahakikishia Watanzania kwa nadharia na vitendo kwamba watanufaika ndani ya "umoja" wa Tanzania nzima, basi hivi vyama vya kikabila vitaendelea kuchipuka.

..hivi vyama vilikuwepo, baadaye vikafifia, sasa vimeibuka tena kwa nguvu zote. pamoja na kuvipiga marufuku tunapaswa kwenda kujiuliza kwanini wananchi wanavikimbilia? what can we do to make tribal associatians irrelevant??
 
Kithuku,

..bila kuwahakikishia Watanzania kwa nadharia na vitendo kwamba watanufaika ndani ya "umoja" wa Tanzania nzima, basi hivi vyama vya kikabila vitaendelea kuchipuka.

..hivi vyama vilikuwepo, baadaye vikafifia, sasa vimeibuka tena kwa nguvu zote. pamoja na kuvipiga marufuku tunapaswa kwenda kujiuliza kwanini wananchi wanavikimbilia? what can we do to make tribal associatians irrelevant??

Hii ni kweli kabisa mkuu nakubaliana na wewe. Watu wanapoangalia matumaini yaliyopo kwenye umoja wa kitaifa na ule wa kikabila, wanaona ule wa kikabila ni nafuu zaidi na ni accessible zaidi. Lakini athari zake ni kubwa zaidi kuliko faida, ndio maana inabidi kuangalia kwa ukaribu. Hizi ni miongoni mwa aina za tafiti zenye maslahi ya taifa ambazo serikali ingefaa kuzigharamia maana zitaleta mapendekezo ya suluhisho muafaka zaidi kuliko tu kuishia kupiga marufuku. Pale Mlimani najua kuna Idara ya Sociology, na sina uhakika kama Anthropology ipo kama idara au kitengo ndani ya sociology, hii ni changamoto yao wanapaswa kuchukua wasaidie taifa hili.
 
haya ndio mambo ninayoyapinga

kuingilia watu na shughuli zao

kama hakuna mtu ambaye ameumia au kawa offended kwa nini watu wanakatazwa wasiwe na social groups? whats next watawakataza wasijiunge na social networking sites kama FACE BOOK kisha wataanza kuwaambia wasichangie mijadala JF ..kama wahaya au wachagga au wazaramo wameamua kuwa na vikundi vyao then whats wrong with that?


Hii nchi kila kukicha inageuka kuwa ORWELIAN state

whats next? waislam kuambiwa wasioe wake 4 na wakristo kuambiwa wakae kwenye mikeka kanisani

ukisikia nchi imekosa mwelekeo basi ndio hapa
 
Na katika sherehe ya chama kingine cha kikabila cha pale mlimani (ilifanyika nje ya chuo), mmoja wa waalikwa ambaye alikuwa ofisa mwenye nafasi muhimu serikalini alipopewa nafasi ya kusalimia "wanandugu" au "homeboys" alitumia fursa hiyo kutaja idadi ya watu wa kabila hilo aliowapatia nafasi mbalimbali kupitia ofisi yake, na kuwachagiza wenzie kufuata mfano huo huku akisema "tupendane jamani!" Alitaja hata fursa nyingine zilizoko kwenye mamlaka yake na kuwataka watu wawahi kumuona naye atajitahidi kusaidia kama alivyosaidia wengine!

Kwa hiyo wakuu mnataka kutuambia kwa kuvipiga marufuku tutaondokana na tatizo la ukabila? Mbona tunang'ang'ania kutibu symptoms na sio ugonjwa wenyewe? Na vyama vya wanawake? Vyama vya wenye ulemavu? navyo tutavipiga marufuku kwa sababu ni vya kibaguzi?
 
Nadhani serikali imechelewa ku-ban hivi vyama. Ukabila umezidi sana UDSM!
DARUSO imekuwa weak sana kutokana na utitiri wa vyama vya kikabila!
Mkuu Kitila Mkumbo, Kabwe Zitto
na waliowahi kusoma UDSM wanaelewa huu ugonjwa!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom