Boyfriend wangu ni mchafu sana

Magnumpi

Member
Oct 4, 2019
68
172
Najua mtanitukana na kunisema eti ni kazi ya mwanamke kumuweka mwanaume sawa lakini hapa nimenyanyua mikono, isiwe kesi bora tuachane tu.

Nimekua katika haya mahusiano mwezi wa 8 sasa, mwanzoni nilikua sijamuelewa sana huyu jamaa na tabia yake lakini yamenifika kooni.

I'm not the cleanest person lakini huyu mwanaume ni mchafu jaman. Akioga usiku kabla ya kulala asubuhi haogi.

Hata kama nikimsema yani analala na mwanamke usiku asubuhi anaenda kazini hivyo hivyo. Chumba chake ndo kichafu usiseme. Kuna wakati nilisafiri nikaenda mkoa mwingine kama mwezi hivi kurudi chumba hakitamaniki.

Nikaona isiwe shida nikamsafishia. Ikawa kila weekend nikienda nasafisha. Nilipata ugeni sikuweza kwenda kwake kwa takribani wiki mbili, Mungu wangu siku nilioenda ni kama pamepigwa bomu! Sahani aliolia chakula siku kama 3 zilizopita zipo humo, machupa ya maji, maganda ya ndizi.

Hapo kitandani ndo usiseme. Ana jiko na sebule lakini viombo vimejaa chumbani. Yani nikaona hii ni tabia yake.

I can't do this anymore. I'm like his house girl.hata mama hamlei mtoto wake hivi.Mwanaume haambiliki. Nikishauri ajitahidi usafi anasema nampanda kichwani( Male ego).

Sijaenda kwake wiki sasa I know nikienda huko huo uchafu ntakaokutana nao sina hamu.

He's a good guy lakini hii tabia yake imenishinda. Bora yaishe tu.

Kina dada mnaishije na hawa viumbe?. Huyu kanishinda
 
Kama kashindikana piga chini mama na umwambie kabisa sababu ni uchafu. Huyo ni mchafu tu toka kuzaliwa maana mwanaume smart ukiweka soksi kwenye kiti halafu girl wako akazitoa na kuziweka panapostahili kesho unatakiwa usirudie kuziweka tena hapo ila only mbumbumbu ndo atarudia.
 
Back
Top Bottom