Boxing.... Manny Pacquiao vs Juan Manuel Marquez live from USA.

mshikachuma

JF-Expert Member
Dec 2, 2010
2,853
626
Haya jamani kumekucha na mtanannge wa ngumi karibu utaanza.

Kwa wale wenye access ya super sport 2 kupitia ving'amuzi vya Dstv unaweza ukajionea mtanange huu wa kukata na
shoka kupitia chanel hiyo kati ya bingwa Manny Pacquiao na Juan Marquez(challenger) live from MGM Grand Garden
Arena-Las Vegas,United States.

Huu siyo mpambano wa kukosa kuangalia!....kwa wale wataalam wa michezo hii tunawaomba mtutupie utamu wa mabondia hawa wawili.
 
Naona ngumi za utangulizi ndiyo zinaanza hapa kabla ya main event.
Patrick hailand na Javia fartuna
 
Duuh naanza kusinzia! Maana nimeamka around saa tisa usiku kusubilia mpambano huu...walianza kuonyesha
histori ya maisha yao na walivyokua wanafanya mazoezi kwa kujiandaa na pambano hili
 
Kwenye hili pambano la kwanza la utangulizi nahisi Fortuna anashinda....huya jamaa anarusha makonde usipime
 
Fortuna ni black na Hyland ni mzungu....sasa ni round ya tano na mzungu keshaanza kuota manundu
 
Nimeamka saa 9 ila nadhan pambano lililoniamsha la huyu congressman pacquiao litakuwa saa 1...Anyway acha tuendelee kuwaangalia hawa 'ma underground'
 
Naona kibao kimegeuka...Fortuna anaanza kuchoka na anapata kichapo.
 
Nimeamka saa 9 ila nadhan pambano lililoniamsha la huyu congressman pacquiao litakuwa saa 1...Anyway acha tuendelee kuwaangalia hawa 'ma underground'
Weee acha tu...mie mwenyewe nimeamka saa tisa hiyohiyo na hapa nilipo naanza kusinzia
 
Namuona Mit Romney hapa live na yeye amekuja kushuhudia mpambano huu...ni yule mgombea urais aliyeshindwa
kwa Obama
 
Round ya 8 inaingia ya 9...bondia wangu Fortuna amechoka na ninahisi anapoteza pambano
 
Namuona Pacquiao ndani ya nyumba....round ya 12 sasa na ndiyo ya mwisho
 
Mpambano umeisha, na Fortuna katangazwa mshindi....pambano lingine la utangulizi linakuja.
 
Haya main event ndiyo hiyo inataka kuanza na sasa zinapigwa nyimbo za Taifa la Mexco na Philipini

Ila mtanisamehe sitaweza kulipoti live maana macho na akili yangu yote nayapeleka kwenye tv kushuhudia kila kitu.
 
50 Cent kapafom live....naona wanaume wa shoka sasa wanaingia teyari kwa kuuwana na kutoana madamu
 
Haya main event ndiyo hiyo inataka kuanza na sasa zinapigwa nyimbo za Taifa la Mexco na Philipini

Ila mtanisamehe sitaweza kulipoti live maana macho na akili yangu yote nayapeleka kwenye tv kushuhudia kila kitu.

Mkuu acha hizo uwe unaripoti hata baada ya kila round kwa mtindo wa summary.Wengine tuko mbali na runinga ila tunapenda kujua yanayojiri,umeweka thread sawa tuabarishe sasa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom