Boti ya kisasa (speed boat) inayofanya safari zake Mwanza-Bukoba imepunguza nauli kutoka 50,000 hadi 30,000

Nitasifu sana na kufurahi iwapo hiyo boat imeundwa na Songora Marine transport ya Mwanza.Mleta mada hebu nijuze mtengenezaji wa hiyo boat. Kama imeagizwa toka nje wooooi! nalaani.
Hiv ishu kama hizo huwa zinasimamia bei gani?
 
Sasa kama ni Masaa 4, Si wapige ruti mbili Go & Return kwa siku
Ni nzuri sema nafikiri watakuwa wanastudy route yao ili waone wanatekebisha/kuboresha wapi. Uzuri naona wako positive katika maoni ya wateja wao ...kwa kuanzia siyo mbaya hata kidogo
 
Changamoto iliyopo ni kwamba watu wanakuja muda umeisha hivyo wanaachwa, jamani hii boti wenyewe hawazidishi muda muda ukifika hata kama wana abiria mmoja wanaondoka.
 
Wadau hii boti bado ipo? Waliowahi kuitumia kwa siku za karibuni wanaionaje?
 
Changamoto iliyopo ni kwamba watu wanakuja muda umeisha hivyo wanaachwa, jamani hii boti wenyewe hawazidishi muda muda ukifika hata kama wana abiria mmoja wanaondoka.
Ndio vizuri. Lakini vipi utulivu wake, inaonekana ni ndogo imetulia kwenye maji au ndio mwendo wa kutapikiana hasa ukiwa na watoto.
 
Kampuni ya Earthwise Ferries (T) LTD ambayo imeleta boti ya kisasa MV Bluebird kwa ajili ya safari za Bukoba na Mwanza imepunguza nauli kutoka Tshs 50,000 hadi Tshs 30,000 kuanzia tarehe 11/01/2018.

Boti hiyo ambayo inatumia masaa manne kutoka mwanza kwenda Bukoba, na Bukoba kwenda mwanza, inauwezo wa kubeba watu 100.

Ratiba ya boti hiyo kwa wiki (11/01/2018 hadi 17/01/2018) hii ni;

  1. Itaondoka Mwanza kwenda Bukoba saa nne asubuhi (10:00AM) siku ya Alhamisi (11/01/2018), Jumamosi (13/01/2018), Jumatatu (15/01/2018) na Jumatano (17/01/2018)
  2. Itaondoka Bukoba kwenda mwanza saa saba mchana (13:00) siku ya Ijumaa (12/01/2018), Jumapili (14/01/2018), Jumanne ( 16/01/2018)
N.B
Kwa kifupi safari zao zinapishana kwamba akiingia leo Bukoba basi kesho yake anaenda Mwanza.

Kwa mawasiliano unaweza kufika katika ofisi zao zilizopo bandari ya Bukoba au bandari ya Mwanza kaskazini (Mwanza North Port) au mawasiliano +255 764 954 687 au +255 782 660 297

NAULI ni Tshs 30,000

Picha na video zipo hapo chini

Huko hakuna abiria, hawa ndugu zangu wamezoea kupanda malori ya ndizi ama ng'ombe katika safari zao ukizingatia hawaendagi kwao mpaka lifti za misiba.
 
Heko kwa wawekezaji Earthwise Ferries (T) Ltd. Ole wao wavuvi na wadau wengine wa hilo ziwa wasiojua maeneo inakopita.
 
Back
Top Bottom