Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
SWAHILI:
CORONAVIRUS: BoT YAONGEZA KIWANGO CHA MIAMALA YA KWENYE SIMU NA UNAFUU KWA HATI FUNGANI
Kamati ya Sera ya Fedha ya Bodi ya Benki Kuu ya Tanzania imepitisha hatua mbalimbali za kisera zinazolenga kukabiliana na athari za mlipuko wa #COVID19 katika Uchumi ili kudumisha uthabiti wa Sera ya fedha.
1. Kampuni zinazotoa huduma ya fedha kwa njia ya mtandao kuongeza kiwango cha miamala kwa siku kwa mteja kutoka Tsh. Milioni 3 hadi Tsh. Milioni 5 na kiwango cha akiba kwa siku cha mteja kutoka Tsh. Milioni 5 hadi Tsh. Milioni 10.
2. Kuongeza unafuu kwenye dhamana na hati fungani za Serikali zinanazotumika na benki kama dhamana wakati wa kukopa Benki Kuu. Kiwango cha dhamana kimepunguzwa kutoka 10% hadi 5% kwa dhamana za muda mfupi na pia kutoka 40% hadi 20% kwa hati fungani.
3. Benki Kuu itatoa unafuu kwa benki na taasisi za fedha zitakazotoa unafuu katika kurejeshwaji wa mikopo kwa namna zinavyoona inafaa na kujadiliana na Wakopaji kwa kuzingatia uwazi bila upendeleo.
4. Imeshusha kiwango cha chini cha kisheria cha sehemu ya amana kinachotakiwa kuwekwa Benki Kuu ya Tanzania, kutoka asilimia 7 hadi asilimia 6. Pia, imeshusha kiwango cha riba kinachotozwa kwa benki kukopa kutoka 7% hadi 5%.
Aidha, Benki Kuu inaufahamisha Umma kuwa nchi yetu ina akiba ya kutosha ya fedha za kigeni kuwezesha kuagiza bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi na Wananchi wanahimizwa kufanya miamala kwa kutumia Shilingi badala ya fedha za kigeni.
ENGLISH:
Tanzania central bank lowers reserve requirements due to coronavirus
NAIROBI, May 12 (Reuters) - Tanzania’s central bank lowered the statutory minimum reserves requirements for commercial banks to 6% from 7% and cut its discount rate for banks, to cushion the economy from the effects of the coronavirus crisis, it said on Tuesday.
The reduction of the reserves will come into effect on June 8 to provide additional liquidity to banks, governor Florens Luoga said in a statement.
The bank also cut its discount rate for lending to banks to 5% from 7% to “provide additional space for banks to borrow from the Bank of Tanzania at a lower cost, thus signalling lower lending rates by banks.”
The central bank will reduce haircuts on government securities to 5% from 10% for Treasury bills and to 20% from 40% for Treasury bonds to allow lenders to access funding from the central bank “with less collateral than before”, Luoga said.
Lenders will also be provided with “regulatory flexibility”, so they can change the terms of loans for borrowers who might fall into distress due to the crisis, the central bank said.
Tanzania has confirmed 509 cases of the coronavirus, with 21 deaths, according to the World Health Organization.
However, the government has been criticised for not providing regular updates on the spread of the outbreak, and the opposition has accused it of being secretive.
Tanzania launched an investigation after samples taken from a goat and a pawpaw tested positive for the new coronavirus, prompting President John Magufuli to question the efficacy of tests.
The WHO and the Africa Centres for Disease Control and Prevention disputed Magufuli’s assertion.
The International Monetary Fund expects Tanzania’s economic growth to slide to 2% this year, from 6.3% in 2019.