BoT yazuia matumizi ya pesa ya kidigitali - Crypto currency

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
BoT katika taarifa yake imeeleza kuwa inatambua juu ya uwepo wa watu wanaofanya malipo kwa kutumia sarafu hizo na yapo matukio ya uhamasishaji wa sarafu hizo

Wapo wanaodai kuwa wamewasiliana na Benki Kuu kuhusu uhalali wa matumizi ya sarafu kauli ambazo ni potofu

Taarifa ya BoT imewaonya wote kuwa biashara na uhamasishaji wa sarafu hizo ni kinyume na kanuni za udhibiti wa fedha za kigeni

====
TAARIFA KWA UMMAKUHUSU FEDHAZA KIMTANDAO

Benki Kuu ya Tanzania imeshuhudia kuwepo kwa wananchi wanaotumia fedha za kimtandao (cryptocurrencies) katika kufanya malipo hapa nchini. Aidha, Benki Kuu inatambua kwamba kuna matukio ya kuhamasisha biasharaya fedhahizi za kimtandao hapa nchini ili zionekane kamani fedha halali kwa ajili ya kufanya malipo. Vitendo hivyo ni pamoja na baadhi ya watu kudai kwamba wamewasiliana na Benki Kuu kuhusu matumizi ya fedha hizo za kimtandao.

Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuutahadharisha umma kwamba uuzaji, uhamasishaji wa biashara hiyo na matumizi ya fedha za kimtandao ni kinyume chakanuni za udhibiti wa fedha za kigeni.

Benki Kuuya Tanzania, kama taasisi pekee hapa nchini yenye mamlaka ya kuchapisha noti na kutengeneza sarafu na kuamua fedha halali kwa ajili ya matumizi hapa nchini,kama ilivyoainishwa kwenye Vifungu vya 26 na 27 vya Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006, inautarifu umma kwamba Shilingi ya Tanzania ndiyo fedha halali kwa ajili ya kufanya malipo hapa Tanzania. Fedha zingine za kigeni zinauzwa na taasisi zilizosajiliwa hapa nchini kwa mujibu wa taratibu zilizopo za kubadilisha fedha za kigeni. Fedha hizo zinazonunuliwa zinarudishwa kwenye nchi husika kwa mujibu taratibu zilizopo.

Hivyo, kwa taarifa hii, umma unatahadharishwa kutojihusisha na fedha za kimtandaona kwamba kufanya hivyo ni kinyume cha kanuni zilizopo za fedha za kigenina kunaweza kusababisha hasara kwa anayehusika.


1573549906021.png
 
Cryptocurrency hizo hazijaruhusuiwa kufanya transaction nchini si kwamba hawazitambui kwamba nchi nyingine zipo halali,ila hawaitambui so ni kwa wewe mwenye nazo utajua unazitumia vipi na zinakufaidisha vipi,

Watu wasio na elimu wasijechanganya crypto na forex trading, forex inaruhusiwa coz bank kuu inatambua fedha halali za nchi tofauti tofauti
 
Je kuna uwezekano watawala wakatrace account za cryptocurrency?
Kama upo watu wajiandae kulia.
 
Hawa BOT wasituzingue bwana, kwani crypto currency ni bidhaa kama zilivyo bidhaa nyingine tu
 
Huwezi kuzuia revolution of money hata iweje ! Kitu hicho kipo all over the world !
 
Cryptocurrency hizo hazijaruhusuiwa kufanya transaction nchini si kwamba hawazitambui kwamba nchi nyingine zipo halali,ila hawaitambui so ni kwa wewe mwenye nazo utajua unazitumia vipi na zinakufaidisha vipi,

Watu wasio na elimu wasijechanganya crypto na forex trading, forex inaruhusiwa coz bank kuu inatambua fedha halali za nchi tofauti tofauti
Fedha za kimtandao ni zipi? Ni kama kulpia bidhaa nje na PayPal?
 
Huwezi kuzuia revolution of money hata iweje ! Kitu hicho kipo all over the world !
Mkuu hizo Digital currency ni mjadala mkubwa hata kwenye nchi zilizo endelea, ngumu sana kudhiibiti matukio ya kufadhili uhalifu kama ughaidi au madawa ya kulevya au vita.

Serikali inaweza kukosa udhibiti wa mfumuko wa bei n.k.
Debate kubwa sana hiyo.
 
Habari wana jukwaa,

Kabla ya kuanza huu uzi napenda kunukuu maneno ya marehemu Ruge "Ogopa sana Mungu na technology".

Haya sasa naomba niulize je tunawezaje kusonga mbele pasipo technology? Na je teknolojia inazuilika? Zipi hasara za kuizuia au kuchelewa kuifahamu?

Binadamu amepitia zama nyingi sana kama zama za mawe, chuma n.k. Sasa lengo la zama au vipindi vyote hivyo ni kuweza kuyakabili mazingira na changamoto za kiuchumi, kiutamaduni n.k ndani yake.

Zama tulizonazo sasa ni zama za sayansi na teknolojia na hii ni katika nyanja za kiuchumi, kiutamaduni, na kijamii mambo mengi yanaenda na sayansi.

Ajabu ni kwamba BoT anashindwa kuendana nayo kwa sababu dhaifu. BoT kama chombo kikubwa cha usimamizi wa fedha imetangaza kutoitambua pesa ya kidigitali maarufu kama Cryptocurrency.

Na hii imekuja kutokana na Wimbi la watu wengi kuingia kuwekeza huko. Na maana yake hii biashara inaenda kufa Tanzania. Je hii ni sawa?

Na vipi kuhusu watu waliyowekeza mamilioni huko? Ila vipi fursa ya biashara hii kwa siku za usoni?

China ilikuwa miongoni mwa nchi zilizopiga marufuku biashara hii. Lakini sasa imeruhusu hii biashara na kusababisha kuongezeka thamani nafikiri kwa watu mnaofuatilia mmeliona hili, Marekani ni moja ya nchi ambayo mabilionea wake wamewekeza kwenye Cryptocurrency.

Na sasa ukienda nchi zilizoendelea kuna ATM za Cryptocurrency (Bitcoin), pia
Kuna makampuni yanayotoa mikopo kwa dhamana ya Bitcoin.

Je Tanzania kwa kupitia BoT hawaoni fursa ya nchi kubwa kuwekeza huko. Kama sijakosea hata Rais wa Kenya Mr. Kenyatta aliongelea positive hii biashara.

Tanzania tunakwama wapi? Kwa mtazamo wangu naenda kinyume na BoT kwa kutoa sababu dhaifu.

Screenshot_2019-11-12-17-07-32-1.jpeg
 
Habari wana jukwaa,
Kabla ya kuanza huu uzi napenda kunukuu maneno ya marehemu Ruge" Ogopa sana Mungu na technology" .
Haya sasa naomba niulize je tunawezaje kusonga mbele pasina technology?
Na je technologia inazuirika?
Zipi hasara za kuizuia au kuchelewa kuifahamu?
Binadamu amepitia zama nyingi sana kama zama za mawe, chuma n.k
Sasa lengo la zama au vipindi vyote hivyo ni kuweza kuyakabiri mazingira na changamoto za kiuchumi , kiutamaduni n.k ndani yake. Zama tulizonazo sasa ni zama za sayansi na technologia na hii ni katika nyanja za kiuchumi, kiutamaduni , na kijamii mambo mengi yanaenda na sayansi.
Ajabu ni kwamba Bot anashindwa kuendana nayo kwa sababu zaifu. Bot kama chombo kikubwa cha usimamizi wa fedha imetangaza kutoitambua pesa ya kidigitari maarufu kama Cryptocurrence.
nahii imekuja kutokana na Wimbi la watu wengi kuingia kuwekeza huko. Namaana yake hii biashara inaenda kufa Tz, Je hii ni sawa?
Na vp kuhusu watu waliyowekeza mamilioni huko?
Ila vipi fursa ya biashara hii kwa siku za usoni?
China ilikuwa miongoni mwa nchi zilizo piga marufuku biashara hii. Lakini sasa imeruhusu hii biashara na kusababisha kuongezeka thaman nafikiri kwa watu mnaofatilia mmeliona hili, Marekani ni moja ya nchi ambayo mabilionea wake wamewekeza kwenye Cryptocurrence.
Nasasa ukienda nchi zilizoendelea kuna ATM za Cryptocurrence (Bitcoin), pia
Kuna makampuni yanayotoa mikopo kwa dhamana ya Bitcoin.
Je Tz kwa kupitia BOT hawaoni fursa ya nchi kubwa kuwekeza huko. Kama sijakosea hata Rais wa Kenya Mr.kenyata aliongelea positive hii biashara . Tz tunakwama wapi?
Kwamtazamo wangu naenda kinyume na BOT kwa kutoa sababu dhaifu.
View attachment 1261444
Hawa wazee ni wapumbavu
 
Habari wana jukwaa,
Kabla ya kuanza huu uzi napenda kunukuu maneno ya marehemu Ruge" Ogopa sana Mungu na technology" .
Haya sasa naomba niulize je tunawezaje kusonga mbele pasina technology?
Na je technologia inazuirika?
Zipi hasara za kuizuia au kuchelewa kuifahamu?
Binadamu amepitia zama nyingi sana kama zama za mawe, chuma n.k
Sasa lengo la zama au vipindi vyote hivyo ni kuweza kuyakabiri mazingira na changamoto za kiuchumi , kiutamaduni n.k ndani yake. Zama tulizonazo sasa ni zama za sayansi na technologia na hii ni katika nyanja za kiuchumi, kiutamaduni , na kijamii mambo mengi yanaenda na sayansi.
Ajabu ni kwamba Bot anashindwa kuendana nayo kwa sababu zaifu. Bot kama chombo kikubwa cha usimamizi wa fedha imetangaza kutoitambua pesa ya kidigitari maarufu kama Cryptocurrence.
nahii imekuja kutokana na Wimbi la watu wengi kuingia kuwekeza huko. Namaana yake hii biashara inaenda kufa Tz, Je hii ni sawa?
Na vp kuhusu watu waliyowekeza mamilioni huko?
Ila vipi fursa ya biashara hii kwa siku za usoni?
China ilikuwa miongoni mwa nchi zilizo piga marufuku biashara hii. Lakini sasa imeruhusu hii biashara na kusababisha kuongezeka thaman nafikiri kwa watu mnaofatilia mmeliona hili, Marekani ni moja ya nchi ambayo mabilionea wake wamewekeza kwenye Cryptocurrence.
Nasasa ukienda nchi zilizoendelea kuna ATM za Cryptocurrence (Bitcoin), pia
Kuna makampuni yanayotoa mikopo kwa dhamana ya Bitcoin.
Je Tz kwa kupitia BOT hawaoni fursa ya nchi kubwa kuwekeza huko. Kama sijakosea hata Rais wa Kenya Mr.kenyata aliongelea positive hii biashara . Tz tunakwama wapi?
Kwamtazamo wangu naenda kinyume na BOT kwa kutoa sababu dhaifu.
View attachment 1261444
Nchi inajitenga.

Ina maana wameshindwa kufuata sheria za kimataifa kuhusu hizi transaction?
Pumbavu kabisa
 
Back
Top Bottom