BoT: Ukaguzi wakamilika

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Habari kutoka Mwananchi zinasema ukaguzi wa 'ufisadi' BoT umekamilika. Soma zaidi hapa chini:

Ukaguzi wa tuhuma za ufisadi BoT wakamilika


Na Ramadhan Semtawa

WAZIRI wa Fedha, Zakia Meghji amesema ukaguzi wa tuhuma za ufisadi wa mahesabu ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) uliofanywa na Kampuni ya Ernst &Young, umekamilika.


Meghji alisema jana kuwa ukaguzi huo uliokuwa unadafanywa na kampuni ya ukaguzi ya Ernst & Young kufuatia tuhuma za kuwepo ubadhilifu katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA)umekamilika na kwamba ripoti ya awali imepelekwa London, uingereza kwa ajili ya kuandaa ripoti kamili ambayo itakabidhiwa serikali.


Ukaguzi huo ulioanza Septemba 9 na ulipaswa kukamilika katika kipindi cha ndani ya siku 60 ambazo ziliisha jana.


Akizungumzia ukaguzi huo, Meghji alisema ripoti ya matokeo imekwenda kuandaliwa nchini Uingereza na kwamba itakabidhiwa serikalini ndani ya wiki tatu.


Meghji alisema serikali ilitoa siku 60 na kwamba baada ya kuuliza kampuni husika ilitoa maelezo kwamba kuchelewa kukabidhi ripoti kulitokana na ukaguzi ambao ulivuka hadi nje ya nchi.


Waziri Meghji alisema ukaguzi huo ambao ulisimamiwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), uliwezesha kampuni hiyo kwenda hadi nchini Afrika Kusini.


"Ukaguzi umekamilika kwa maana ya Field (vitendo), lakini ripoti bado haijawasilishwa serikalini, lakini kila kitu kwa maana ya Field tayari," alisema Meghji na kuongeza,


"Ripoti wamekwenda kuiandaa Uingereza, wameahidi kuikabidhi ndani ya kipindi cha wiki tatu baada ya kuifanyia kazi vema," alisisitiza waziri Meghji.


Alisema matokeo ya uchunguzi huo yatatangazwa hadharani baada ya ripoti yake kuwasilishwa kutoka kwa wakaguzi na kisha serikali kuipitia kwa kina.


Tuhuma katika EPA zinahusu pia sh10 bilioni ambazo zinadaiwa na wapinzani kuchotwa na kutumiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye kampani za Uchaguzi Mkuu wa wa mwaka 2005.


Kaimu Gavana wa BoT, Juma Reli aliliambia gazeti hili kwamba tuhuma hizo za kuchotwa sh 10 bilioni na CCM nazo zitafahamika baada ya uchunguzi huo.


Reli alisema hakuna kitakachofishwa na kwamba wakaguzi hao walifanya kazi zao kwa ufanisi kwa kuhoji na kupitia nyaraka mbalimbali za BoT.


Ernst &Young ilishinda zabuni hiyo baada ya kuyashinda makampuni saba, ambayo uchunguzi wake umekuwa ukiangaliwa kama kipimo kikuu cha serikali katika suala zima la kupambana na ufisadi nchini.


Uchunguzi huo unasaubiriwa kwa hamu kutokana na nchi 14 wafadhiri ambazo zilitoa msimamo wiki iliyopita kwamba matokeo ya uchunguzi huo utatoa mwelekeo wa uchangiaji wake wa fedha katika bajeti ya Tanzania kwa mwaka 2008/09.


Kampuni hiyo inapitia mahesabu katika kumbukumbu za malipo yaliyofanywa na benki hiyo katika kipindi cha mwaka 2005/6, kubaini kama kuna ukweli juu ya madai ya ubadhirifu wa fedha katika benki hiyo katika kipindi hicho.


Hata hivyo, serikali ilitoa tamko kwamba uchunguzi huo utakuwa huru na matokeo yake yatawekwa bayana na Rais Jakaya Kikwete, ameahidi kuwachukulia hatua wote watakaobainika kuhusika na ubadhirifu huo kama ripoti itakavyoonyesha.


Source link:mwananchi.co.tz

Swali: kwanini ipelekwe Uingereza kwanza?!

SteveD.
 
Asante SteveD.. ila hivi hata makaratasi ya kuandikia ripoti yako Uingereza. Mwanzo joho la Spika sasa hata typewriter?
 
lets wait and see,ila kwa kiburi cha mama meghji inaonesha ripoti it is on their favour ndio maana amekurupuka kabla ya ripoti kutoka kuonesha ushindi,utasikia ni uzembe tu ndio uliotokea,yako wapi yaliyotokea baada ya Bwana mchafu Hosea kutoa ripoti ya PCCB kuhusu sula la Richmonde,hata siku moja serikali ya sisiemu haiwezi kukiri kwamba wanakosea.
 
Asante SteveD.. ila hivi hata makaratasi ya kuandikia ripoti yako Uingereza. Mwanzo joho la Spika sasa hata typewriter?

...hebu fikiria tu, BAE systems kesi yao baada ya kuchunguzwa na kutoonekana na hatia (au migongano ya maslahi) baada ya Lord Chancellor wa huko Uingereza kusema hivyo ingepelekwa Uarabuni au Marekani kwanza?!

...tuombe ukweli ubakie tu ndani ya hizo report.

SteveD.
 
Asante SteveD.. ila hivi hata makaratasi ya kuandikia ripoti yako Uingereza. Mwanzo joho la Spika sasa hata typewriter?

hata dili la radar si lilianzia uingereza?
mkataba wa buzwagi scandal je?
huko ndiko mambo maovu ya Tanzania yanakoenda kupikwa.huu ni ulaghai wa hii kampuni ya watanania tu kwa serikali ili walipwe pesa nyingi.ningependa kujua na gharama walizolipwa hii kampuni ya Ernest and Young..
 
lets wait and see,ila kwa kiburi cha mama meghji inaonesha ripoti it is on their favour ndio maana amekurupuka kabla ya ripoti kutoka kuonesha ushindi,utasikia ni uzembe tu ndio uliotokea,yako wapi yaliyotokea baada ya Bwana mchafu Hosea kutoa ripoti ya PCCB kuhusu sula la Richmonde,hata siku moja serikali ya sisiemu haiwezi kukiri kwamba wanakosea.

Mkombozi, hizi hisia zako zinaweza kuwa na ukweli mwingi tu, isingekuwa on their favour wala usingesikia... labda ingeenda kutangazwa marekani hivyo kutokuwa na mvutano mwingi hapa nyumbani. Kwa kisingizio kuwa ilisha tolewa huko kwa wahisani wetu na wamekubaliana na yaliyomo, na masahihisho yanafanyika.

SteveD.
 
Ukishangaa ya Musa utayaona ya firauni......WTF is goin' on? kwani imeandikwa kwa penseli? i dont understand the TRIANGLE hapa, auditors are Americans,work in Tanzania kisha finishing UK. this is great tunaibiwa juu ya kuibiwa....kumbukeni OFISI YA MPIGA CHAPA MKUU WA SERIKALI, sijui inachapisha makorokocho gani? i hope it leaks coz i need to take a look at it know and not later(3wks)!Goddam it!!
 
Ngoja tusubiri na tuone wiki mbili/tatu siyo nyingi. nafikiri hakutakuwa na longolongo. Hila mbona walikuwa wameisha sema kuwa hakuna kitu hila ni political gain (Makamba et al 2007 and JK et al 2007)]

Kukipatikana tatizo watakana matamshi yao?
 
Mkombozi, hizi hisia zako zinaweza kuwa na ukweli mwingi tu, isingekuwa on their favour wala usingesikia... labda ingeenda kutangazwa marekani hivyo kutokuwa na mvutano mwingi hapa nyumbani. Kwa kisingizio kuwa ilisha tolewa huko kwa wahisani wetu na wamekubaliana na yaliyomo, na masahihisho yanafanyika.

SteveD.
wahisani ndio Mungu wao,kwa taarifa niliyonayo,Hazina hakuna pesa kabisa,huyu mama anajitahidi kuisafisha serikali ili pesa zije..hivi kwanini watu wasigome kulipa kodi mpaka hapo suala la BOT,Buzwagi litakapopatiwa ufumbuzi
 
wahisani ndio Mungu wao,kwa taarifa niliyonayo,Hazina hakuna pesa kabisa,huyu mama anajitahidi kuisafisha serikali ili pesa zije..hivi kwanini watu wasigome kulipa kodi mpaka hapo suala la BOT,Buzwagi litakapopatiwa ufumbuzi

Naweza kukubaliana nawe kabisa hapa. hasa hasa forex, kila chache zinazopatikana kutoka bandarini na kuuza kahawa kidogo zinamalizikia kwenye ziara za viongozi zisizoisha. Kila kidogo za madafu zinazopatikana, zinapelekwa kuwa posho za wabunge kizota. Kila chache zinazopatikana, zinatumika kununulia mashangingi ya 4.1 litres ili yatembee kwenye mitaa ya Dar na kukata mbuga za Tanzania.

Hilo la mgomo sijui... labda tuupigie debe mgomo wa wafanyakazi kwanza...

SteveD.
 
Hawa waingereza bado wanatutawala nini, isije ikawa ndio hivyo sisi hatujui, ya Mungu mengi!
 
Nafikiri huko ndio makao makuu ya Ernst and Young.

---sawa kama hilo ni jibu pekee la madukuduku yetu.

---May be we're just being sceptical, i don't know; but we know that " a wise man proportions his beliefs to the evidence".



SteveD.
 
...hawa watu siwaaimini kwa chochote,hapo tunapotezeana muda tuu huku billions zimeshaondoka na hazitarudi tena,inasikitisha sana kwa jengo kama lile la BOT to cost more than 200m $
 
Hivi nchi zilizo chini ya Commonwealth kiongozi wao mkuu ni nani?

Malkia. Hili lijumuiya linahitaji ukarabati wa sheria zake kwani wanaofaidika ni wachache na kwa ubaguzi sana. Utasikia wanasifia sana lakini ni pale tu wakubwa wanapofaidi.

Asante SteveD.. ila hivi hata makaratasi ya kuandikia ripoti yako Uingereza. Mwanzo joho la Spika sasa hata typewriter?

Haya watueleze walichokuwa wanapika kama kitaleta mabadiliko yoyote. Ukweli ni kwamba pesa imeliwa na wajanja, kwa sababu waliokula hiyo pesa wapo karibu na viongozi wakuu wa serikali hakuna kitakachotokea. TUNASUBIRI.
 
Swali ni kwamba nini kilikuwa kinachunguzwa. Mkaguzi wa mahesabu alitumwa na serikali iliyotuhumiwa, akasimamiwa na serikali iliyotuhumiwa na watuhumiwa wote bado ni mabosi, tutegemee riport gani??????????????????? tumeliwa tena sana. Ndio maana nchi nyingi zinaishia kupigana vita kwa sababu za upuuzi kama huu. Ngojeni msikie kwamba kulikuwa na makosa kidogo ya utendaji ila kila kitu sawa tu.
Swali ni kwamba Mkaguzi young anawajibika kwa nani.
Jina kamili la kampuni ya ukaguzi ni Masawe Ernst & Young
 
Swali ni kwamba nini kilikuwa kinachunguzwa. Mkaguzi wa mahesabu alitumwa na serikali iliyotuhumiwa, akasimamiwa na serikali iliyotuhumiwa na watuhumiwa wote bado ni mabosi, tutegemee riport gani??????????????????? tumeliwa tena sana. Ndio maana nchi nyingi zinaishia kupigana vita kwa sababu za upuuzi kama huu. Ngojeni msikie kwamba kulikuwa na makosa kidogo ya utendaji ila kila kitu sawa tu.
Swali ni kwamba Mkaguzi young anawajibika kwa nani.
Jina kamili la kampuni ya ukaguzi ni Masawe Ernst & Young

link hii itakusaidia kuwajua Ernst & Young Global zaidi na sio Masawe kama unavyotaka tuamini.
http://en.wikipedia.org/wiki/Ernst_&_Young#_note-0
Ernst & Young Global is based at London.
 
Ernst & Young Tanzania has six partners and a staff complement of 70 in our two offices in the country. As a member of Ernst & Young Global we offer a global reach while maintaining our national insight ,and in seeking solutions for clients we tap the power of both.

We are committed to providing innovative total solutions through our Client Service Teams and Industry Focus which are designed to meet your unique business needs.


Dar es Salaam

Contacts
Chairman : Ernest Massawe
Phone: +255 22 2666853 / 2667484/
26673683 / 2667227
Fax: +255 22 2666948
Email: info@ey.co.tz

Physical Address
Utalii House
36 Liabon Road
Oysterbay.

Postal Address
P.O. Box 2475
Dar es Salam
Tanzania



Arusha

Contacts
Resident Partner : Omari Mshana
Phone : +255 27 2503081/2 / 2502808
Fax : +255 27 2504402
Email: Ernst.young@habari.co.tz

Physical Address
AICC Building 5th Floor Ngorongoro Block
Boma Road
Arusha
Tanzania

Postal Address
P.O. Box 180
Arusha
Tanzania
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom