BoT Saga Unfolding: Basil Mramba ajiuzulu - Wito

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Niseme nini isipokuwa Bw. Basil Mramba akiwa Waziri wa Fedha aliruhusu Benki Kuu kulipa malipo ya ajabu kwenye makampuni zaidi ya 22 na hivyo kusababisha upotevu wa Shilingi bilioni 133 kama ilivyooneshwa katika ripoti ya Erns & Young.

Bw. Mramba na Mgonja ndio watu wengine wawili ambao Rais angetengua uteuzi wao mara moja. Badala ya wao kusubiri hadi Rais atengue uteuzi huo, kwanini wasiamue kujiuzulu mara moja na kuwajibika kwa vitendo vyao vilivyolinda na kuchochea ufisadi? Kwanini Bw. Mramba na Gray Mgonja hawakuanzisha uchunguzi wowote Benki Kuu licha ya tuhuma za matumizi mabaya kuzagaa kwenye taasisi hiyo kwa miaka nenda rudi?
 
Niseme nini isipokuwa Bw. Basil Mramba akiwa Waziri wa Fedha aliruhusu Benki Kuu kulipa malipo ya ajabu kwenye makampuni zaidi ya 22 na hivyo kusababisha upotevu wa Shilingi bilioni 133 kama ilivyooneshwa katika ripoti ya Erns & Young.

Bw. Mramba na Mgonja ndio watu wengine wawili ambao Rais angetengua uteuzi wao mara moja. Badala ya wao kusubiri hadi Rais atengue uteuzi huo, kwanini wasiamue kujiuzulu mara moja na kuwajibika kwa vitendo vyao vilivyolinda na kuchochea ufisadi? Kwanini Bw. Mramba na Gray Mgonja hawakuanzisha uchunguzi wowote Benki Kuu licha ya tuhuma za matumizi mabaya kuzagaa kwenye taasisi hiyo kwa miaka nenda rudi?

Mhh huyu Basiri Mramba inaonekana anaogopwa sana na Kikwete. Yaani JK ameshindwa hata kutaja jina lake kwenye show yake ya kufukuza kazi mtu aliyejiuzulu!

Mramba watanzania wanaendelea kula nyasi kama ulivyotaka! swali ni je, nyasi zikiisha watakula nini? ...... nyama za watu I think
 
Niseme nini isipokuwa Bw. Basil Mramba akiwa Waziri wa Fedha aliruhusu Benki Kuu kulipa malipo ya ajabu kwenye makampuni zaidi ya 22 na hivyo kusababisha upotevu wa Shilingi bilioni 133 kama ilivyooneshwa katika ripoti ya Erns & Young.

Bw. Mramba na Mgonja ndio watu wengine wawili ambao Rais angetengua uteuzi wao mara moja. Badala ya wao kusubiri hadi Rais atengue uteuzi huo, kwanini wasiamue kujiuzulu mara moja na kuwajibika kwa vitendo vyao vilivyolinda na kuchochea ufisadi? Kwanini Bw. Mramba na Gray Mgonja hawakuanzisha uchunguzi wowote Benki Kuu licha ya tuhuma za matumizi mabaya kuzagaa kwenye taasisi hiyo kwa miaka nenda rudi?

Ushindwe na ulegee kama umekula kungu.....
 
Mhh huyu Basiri Mramba inaonekana anaogopwa sana na Kikwete. Yaani JK ameshindwa hata kutaja jina lake kwenye show yake ya kufukuza kazi mtu aliyejiuzulu!

Mramba watanzania wanaendelea kula nyasi kama ulivyotaka! swali ni je, nyasi zikiisha watakula nini? ...... nyama za watu I think

Watakula mchanga...na udongo
 
I love your courage mdada wa Kiafrika .Hoji unayo haki .Mramba yule mtu sijui namna gani .
 
Posted Date::1/15/2008
Ufisadi BoT: Waziri wa Fedha hana mpango wa kujiuzulu
*Asema yeye ni msafi na si fisadi

Na Ramadhan Semtawa


PAMOJA na shinikizo la wapinzani kutaka ajiuzulu, Waziri wa Fedha Zakia Meghji, amesema hafikirii kuachia nafasi hiyo kutokana na tuhuma za ufisadi katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).


Badala yake, Meghji alifafanua kwamba hata Rais Jakaya Kikwete, akimwondoa katika nafasi hiyo bado rekodi yake wizarani hapo itakuwa ni ya mtu mwadilifu na si fisadi.


Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Meghji alisema haoni sababu ya kutakiwa kujiuzulu kwa ajili ya tuhuma hizo kwani ndiye aliyeshiriki kikamilifu kutaka ukaguzi wa kimataifa katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya BoT.


Meghji alifafanua kuwa shinikizo la kujiuzulu kwa kupewa taarifa potofu na Gavana aliyepita Daud Ballali kwa kuthibitisha malipo ya karibu sh 40 bilioni kwa Kampuni ya Kagoda Agriculture, halina msingi kwa kuwa alitengua barua yake ya awali siku nne baada ya kuthibitisha kulikuwa na uongo katika matumizi fedha hizo.


"Sioni sababu ya kujiuzulu na siwezi kujiuzulu, kama ni barua yangu ya kwanza kuthibitisha malipo kwa Kagoda niliitengua siku nne baada ya kubaini ni uongo. Ni sawa na Rais anamteua mtu halafu anatengua baada ya kubaini aliyemteua hafai," alisema Meghji na kuongeza:


"Lakini kama ningekuwa nimeidhinisha mimi malipo hayo ningejiuzulu, mimi niliombwa kuthibitisha malipo ambayo yalishafanyika, lakini nikabaini uongo nikatengua barua yangu," alisisitiza.


Waziri Meghji alifafanua kwamba, kutokana na mfumo wa utendaji kazi serikalini na nafasi aliyokuwanayo Ballali kama Mshauri Mkuu wa Mambo ya Uchumi wa nchi katika BoT na kazi ambayo fedha hizo imeombewa ambayo ni kwa ajili ya Usalama wa nchi, haikuwa rahisi kuweza kukataa lakini alipobaini kuwa ni uongo aitengua barua ya awali.


"Hapa naomba watu waelewe, sikuidhinisha malipo ya pesa hizo kwa Kagoda bali kuthibitisha malipo ambayo yalishalipwa mwaka 2005, Ballali kama Mshauri Mkuu wa Mambo ya Uchumi, alikuja akanitaka niandike barua kueleza kwamba fedha hizo zililipwa kwa ajili ya shughuli za usalama wa nchi," alisema.


Alisema malipo ya fedha hizo kwa Kagoda ambazo zililipwa mwaka huo 2005, utata wake ulibainika katika ukaguzi wa ya Kampuni ya Doloitte &Touche na kuongeza kwamba hakuwahi kusimamisha au kutengua zabuni ya kampuni hiyo ya ukaguzi ndani ya BoT.


"Sikuwahi kutengua au kusitisha mkataba wa BoT na Deloitte&Touche, hawa ndiyo wamegundua upotevu wa fedha hizi na wametusaidia, ndiyo maana pia serikali ikachukua taarifa ya kampuni hii na kuamua kufanya ukaguzi mzima katika EPA ambao ulifanywa na Ernst&Young," alisisitiza.


Alisema BoT ilikuwa na mkataba wake na Deloitte&Touche, hivyo haikuwa rahisi kwa yeye kuutengua na kuongeza kwamba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) chini ya sheria mpya ndiye mwenye mamlaka ya kuteua kampuni ya ukaguzi.


Waziri Meghji alipoulizwa vipi Kampuni ya Kilimo ya Kagoda inaweza kupewa fedha kwa madai ya shughuli za usalama wa nchi, alijibu: "Mambo ya usalama yanaweza kufanywa hata na kampuni au taasisi inayojifanya ina tafiti mambo ya elimu, usalama ni mambo mapana," alisema.


Katika hatua nyingine, serikali imesitisha malipo ya huduma za matibabu kwa Ballali kutokana na sasa kutokuwa Gavana.


Waziri Meghji alipoulizwa alijibu: "Nitalifuatilia kwa karibu kwa watu wa BoT wao wanaweza kuwa na taarifa zaidi."


Alipoulizwa tena, Ballali amelazwa katika hospitali gani na anaumwa nini, alisema ni vigumu kueleza kwa sasa.


Kauli hiyo ya Meghji ni sawa na ambayo ilitolewa wiki iliyopita Ikulu na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, ambaye naye alikataa kueleza maradhi ya Ballali na hospitali aliyolazwa.


Ukiacha Meghji na Luhanjo, ugonjwa wa Ballali na hospitali aliyolazwa umezidi kuwa siri kutokana na pia na Gavana mpya wa BoT Profesa Benno Ndulu, kukataa kueleza maradhi na hospitali.


Sakata la ufisadi katika BoT hasa wa zaidi ya sh 133 bilioni, umeibua mjadala mzito nchini kufuatia uamuzi wa Rais Jakaya Kiwete kumwachisha kazi Ballali, baadhi ya wanasiasa wa kambi ya upinzani wametaka hatua zaidi kwa wahusika wengine huku wakimtaja Meghji na Basil Mramba aliyekuwa Waziri wa Fedha wakati wa ufisadi huo, nao wajiuzulu.


Tuma maoni kwa Mhariri
 
Niseme nini isipokuwa Bw. Basil Mramba akiwa Waziri wa Fedha aliruhusu Benki Kuu kulipa malipo ya ajabu kwenye makampuni zaidi ya 22 na hivyo kusababisha upotevu wa Shilingi bilioni 133 kama ilivyooneshwa katika ripoti ya Erns & Young.

Bw. Mramba na Mgonja ndio watu wengine wawili ambao Rais angetengua uteuzi wao mara moja. Badala ya wao kusubiri hadi Rais atengue uteuzi huo, kwanini wasiamue kujiuzulu mara moja na kuwajibika kwa vitendo vyao vilivyolinda na kuchochea ufisadi? Kwanini Bw. Mramba na Gray Mgonja hawakuanzisha uchunguzi wowote Benki Kuu licha ya tuhuma za matumizi mabaya kuzagaa kwenye taasisi hiyo kwa miaka nenda rudi?
Ambalo haliniingii akilini ni:

Kwamba ni Mgonja aliye Mwambia Bi ZM kwamba hayo malipo ya Kagoda si kwa ajili ya usalama! Manake alijua ni ya nini... sasa baada ya hapo????

Yaani huyu Mgonja anapaswa awe Keko sasa hivi akitoa maelezo fasaha! Pleaaaaaaase Jk do the needful
 
Rwabugiri, hilo ndilo tatizo.. watu wa kuwabana ni kina Mgonja, kwanini baada ya kutoka Wizara ya Fedha akapelekwa Hazina?

Hadi hivi sasa kazi imeshaanza. Jumamozi Mkurugenzi wa BoT katika mkoa mmoja wa Kanda ya Magharibi alikuwa anashikiliwa na Polisi... Ndani ya hiyo ripoti kuna majina ya watu karibu 40 ambao wanahusika na upotevu huo wa fedha..

Ili wajue sisi tukiipata hiyo ripoti tutaiweka hadharani, ni jukumu lao kuilinda!
 
RAIA MWEMA

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Basil Mramba, akiwa Waziri wa Fedha mwaka 2005 alisamehe kodi ya mafuta kwa makampuni ya madini kwa muda wote, uamuzi ambao ulibarikiwa mwaka huu na Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, alipoidhinisha mkataba wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi, Raia Mwema limethibitisha.

Msamaha huo wa kodi umetolewa kwa makampuni yanayochimba madini ya dhahabu pekee na unalenga kuzuia utekelezaji wa Sheria ya Ushuru wa Barabara na Mafuta ya mwaka 1985 (The Road and Fuel Tolls Act, 1985) inayohusu utozwaji wa ushuru kwa magari na mafuta yote yanayotumika nchini.

Habari zinaeleza ya kuwa Mramba alifanya uamuzi huo Aprili 2005, kipindi ambacho viongozi wa serikali walikuwa ‘likizo’ wakiwa katika harakati za uchaguzi ikiwa ni siku chache kabla ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kufanya mkutano wake mkuu uliomteua Jakaya Kikwete kuwa mgombea wake wa urais.

Kwa mujibu wa tangazo la serikali (GN) namba 99, lililochapishwa katika gazeti rasmi la serikali la Aprili 15, 2005, Mramba alitoa nafuu hiyo ya kodi, “kwa kipindi chote cha Mkataba wa Uendelezaji Madini (MDA) ama uhai wa mgodi husika au chochote kitakachotangulia kati ya mambo hayo mawili.”

Ofisa mmoja mwandamizi wa serikali aliliambia Raia Mwema kwamba, msamaha huo ni matokeo ya udhaifu wa sheria hiyo inayompa mamlaka Waziri wa Fedha kutoa msamaha “anapojisikia kufanya hivyo” hali ambayo inaweza kutumika vibaya na kiongozi dhaifu.

Wakati kifungu cha 7 (2) kinaeleza wazi kwamba ushuru huo unapaswa kulipwa na mtu yeyote anayenunua mafuta, sehemu ya 8 inampa mamlaka makubwa Waziri wa Fedha kuweza kutoa msamaha wa kodi kwa jinsi atakavyoona inafaa.

“Waziri anaweza, kwa kutangaza katika gazeti la serikali (Government Gazette) kutoa msamaha kwa mtu ama chombo chochote (taasisi ama kampuni) ama gari lolote kuguswa na kifungu cha sheria ya ushuru wa barabara na mafuta, msamaha ambao unaweza kuwa wa jumla jumla ama unaweza kupangiwa kipindi maalumu kulingana na waziri atakavyoona inafaa,” inaeleza sehemu ya 8 ya sheria hiyo.

Anayetajwa kuanza kutumia mamlaka hayo kutoa msamaha kwa makampuni ya uchimbaji dhahabu alikuwa Daniel Yona, akiwa Waziri wa Fedha, siku ya kuadhimisha miaka 22 ya kuzaliwa kwa CCM, Februari 5, 1999, lakini yeye alitoa msamaha huo kwa mwaka mmoja wa kwanza tu baada ya kuanza rasmi kwa uzalishaji wa dhahabu.

Habari zinasema kwamba Mramba ‘alimzidi kete’ Yona, kwa yeye kuamua kutoa msamaha huo kwa kipindi chote cha uhai wa migodi ya dhahabu, jambo ambalo limeanza kugusa hisia za watendaji serikalini wakiwamo wajumbe wa kamati iliyoundwa awali kwa maelekezo ya Rais Kikwete kupitia upya mikataba ya madini.

Kamati hiyo iliyoongozwa na aliyekuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Laurence Masha, ilionyesha wazi kutoridhika na kipengele hicho na kupendekeza mabadiliko makubwa katika kutolewa kwa misamaha hiyo.

Wajumbe wengine wa kamati hiyo walitoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Wizara ya Mipango na Uchumi na Uwezeshaji, Wizara ya Fedha, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Sheria na Katiba, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Idara ya Jiolojia, Benki Kuu na STAMICO.

Kamati hiyo ilielezea jinsi ambavyo makampuni mengi ya madini yanatumia mafuta mengi kutokana na kutotumia umeme wa gridi na badala yake wanatumia jenereta za dizeli wakati wote na kushauri kuwapo kwa marekebisho katika misamaha ya kodi kwa makampuni ya madini.

Mtaalamu mmoja wa uchumi alilieleza Raia Mwema kwamba kwa siku makampuni ya mafuta hutumia zaidi ya lita 300,000 za mafuta kwa uzalishaji, kiwango ambacho husamehewa kiwango kikubwa cha fedha kwa kila lita kinachokadiriwa kuwa takriban Sh bilioni 46 kwa mwaka.

Hata hivyo, Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, hakuzingatia kabisa ushauri huo wa kamati alipokwenda kusaini mkataba wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi kati ya serikali na kampuni ya Pangea Minerals Limited, kampuni tanzu ya Barrick. Katika mkataba wa Buzwagi kifungu cha 4.4.3 kimeweka wazi kwamba Pangea hawatawajibika kulipa ushuru wa mafuta kwa kuzingatia marekebisho yaliyofanywa na Waziri Mramba.

Karamagi aliliambia Bunge mjini Dodoma kwamba mkataba wa Buzwagi umezingatia mapendekezo ya kamati ya madini iliyoundwa kwa maelekezo ya Rais.

Kwa mujibu wa kumbukumbu rasmi za Bunge (hansard) akijibu bungeni hoja ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, aliyetaka kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuhusu kusainiwa kwa mkataba wa Buzwagi, Waziri Karamagi alisema mapendekezo ya kamati ya Rais yametekelezwa katika kusaini mkataba wa Buzwagi.

“Mheshimiwa Kabwe Zitto, anasisitiza kuwa zoezi la kudurusu mikataba bado linaendelea. Mtoa hoja labda anachanganya tena zoezi la kudurusu mikataba na zoezi linaloendelea na kudurusu Sheria ya Madini ya Mwaka 1998 na Sheria zinahusu mfumo wa kodi katika sekta ya madini; kitu ambacho ni kipana zaidi na kinawahusu wadau wote yaani, wawekezaji wakubwa, wawekezaji wadogo na wote wanaojihusisha na utafiti katika sekta ya madini. Akielewa hili mtoa hoja atabaini kuwa maagizo ya (kamati ya) Rais yalitekelezwa kikamilifu na matokeo yake yameshaanza kujitokeza,” alisema Karamagi.

Mbali na msamaha katika ushuru wa mafuta, Mkataba wa Buzwagi pia umepingana na ushauri wa Kamati ya Masha iliyoundwa kwa maelekezo ya Rais kuhusu ulazima wa makampuni ya madini kuishirikisha Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika ufunguaji wa akaunti katika offshore banks za nje. Mbali ya kuonyesha wasiwasi wake kuhusu makampuni mengi ya madini kutozingatia kipengele hicho, Kamati ya Masha ilipendekeza kufanyika kwa uchunguzi wa kina chini ya usimamizi wa pamoja wa Wizara ya Nishati na Madini na BoT.

Mkataba wa Buzwagi uliosainiwa na Karamagi nchini Uingereza, unazingatia kuwapo kwa kibali cha BoT katika kipengele cha 5.1 lakini katika kipengele cha 5.2 mkataba huo unaweka wazi kwamba BoT itakaposhindwa ama kukataa kutoa ruhusa hiyo katika kipindi cha siku 30, kampuni husika itaendelea na mpango wake wa kufungua akaunti bila kuhitaji ruhusa hiyo. Sakata la Buzwagi liliibuka bungeni baada ya Zitto kuhoji, pamoja na mambo mengine, usiri wa mkataba huo ambao ulisainiwa nchini Uingereza, lakini Karamagi alitetea kwa nguvu zote akidai kwamba hakukua na ukiukwaji wowote wa sheria na taratibu na ulizingatia maslahi ya taifa.

Katika kuhoji kwake, Zitto alitoa maelezo akitaka kuundwa kwa kamati teule ya Bunge kuchunguza suala hilo, lakini hoja yake ilishindwa kwa kura na wabunge wa CCM japo sasa wengi wanaona walifanya makosa kuzuia hoja hiyo.

Hoja hiyo pia ilimponza Zitto kwani Mbunge wa Mchinga kupitia CCM, Mudhihir Mohamed Mudhihir, aliwasilisha hoja akidai kwamba Zitto alisema uongo wakati akimtuhumu Karamagi, na kupendekeza afungiwe.

Bunge kwa kura nyingi za wabunge wa CCM walipitisha uamuzi wa kumfungia Zitto, kifungo kilichomalizika katikati ya Novemba, baada ya kuigharimu CCM kwa kiasi kikubwa kutokana na wananchi wengi kuonekana kumuunga mkono Zitto na hata kuwazomea viongozi wa serikali na wale wa CCM.

Kabla hata ya Zitto kumaliza ‘kifungo’, Rais Kikwete aliunda kamati ya kupitia mikataba na sheria za madini, huku mbunge huyo kijana akiwa mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo na kuzua maswali mengi kuhusu msimamo wa Rais kuhusu suala hilo.
 
Vyombo vya habari vimebaini kuwa Mkurugenzi wa kampuni inayohakiki makampuni yanayochimba dhahabu Alex Stewarts Assayers ni mtoto wa Mhe. Basil Pesambili Mramba aliyekuwa Waziri wa Fedha wakati kampuni hiyo ilpopata mkataba huo Juni 2003. Katika miaka miwili ya mkataba huo, kampuni hii imekuwa inalipwa dola 751,267 sawa na sh. 939 millioni kila mwezi. Kwa muda wa miaka miwili imejikusanyia dola milioni 18 sawa na sh. 22.5 bilioni. Kampuni hii pia ilisamehewa kodi kwa notisi za serikali za Novemba 25 2005 iliyotiwa saini na aliyekuwa Waziri wa Fedha. Ni wazi kuna mgongano wa manufaa (conflict of interest) ya Waziri wa fedha kuipa mkataba kampuni ambayo mtoto wake ni mkurugenzi na pia kuisamehe kodi. Mpaka hivi sasa serikali haijatoa maelezo ya kina kufafanua utata huu ambao unaashiria matumizi mabaya ya madaraka kunufaisha familia yako ambayo ni rushwa. Rais anawajibika kulichunguza suala hili kwa kina na ikiwa taarifa ambazo zimeandikwa katika vyombo vya habari na vielelezo vyake zina chembe ya ukweli, basi waziri awajibishwe kwa kufukuzwa kazi na Tume ya Kuzuia Rushwa ichukue hatua za kisheria kuwafikisha wahusika mahakamani.

Kutoka: http://cuf-tz.com/666.html
 
Mike Williams | Published 09/9/2005 | Habari za Kitaifa |

Mramba asema Serikali haijafilisika
Waziri Fedha, Bw. Basil Mramba amesema ucheleweshwaji wa mishahara ya wafanyakazi wa serikali kwa kipindi cha Agosti mwaka huu, siyo kielelezo cha kuhalalisha madai kuwa imefilisika.

Bw. Mramba aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu kuchelewa kulipwa kwa wafanyakazi hao.

Badala yake, Bw. Mramba alisema, ucheleweshwaji huo ulisababishwa na hitilafu katika chombo kinachojulikana kama Server kilichopo kwenye mitambo ya kompyuta zinazotumika kuhifadhi kumbukumbu na mifumo ya ulipaji wa mishahara hiyo.

’Serikali haijafilisika, ninapenda wafanyakazi wa serikali na Watanzania wajue hivyo, ucheleweshwaji wa mishahara uliotokea ulisababishwa na hitilafu kwenye mfumo wa kompyuta za hazina zinazotumika kwa kazi hiyo,’ alisema.

Kwenye mkutano huo, Bw. Mramba alifuatana na Mkuu wa Kitengo cha Kompyuta (Hazina), Bi. Bernadeta Kamazima na Mhasibu Mkuu wa Serikali, Bi. Blandina Nyoni.

Alisema, madai kuwa uchelewashaji wa kulipa mishahara hiyo ulisababishwa na mambo ya kampeni za Uchaguzi Mkuu na Benki Kuu kuzuia malipo yake (serikali), hazina msingi wala ukweli wowote. Hata hivyo, Bw. Mramba alisema uharibifu huo umetokea kwa mara ya tatu sasa, ingawa kwa kipindi kilichopita hakuna hitilafu yoyote iliyotokea.

Alisema, kuharibika huko kulitokea wakati ambapo Wizara ilikuwa imeagiza vifaa vipya vya kisasa vya kompyuta ambavyo vinakidhi mabadiliko yanayotokea katika mfumo wa kompyuta.

Naye Bi. Kamazima alisema, uharibifu wa kifaa hicho kinachotumika kwenye kompyuta aina ya Compaq HP, ulisababisha usumbufu kwa serikali kutafuta mahali pa kukipata katika nchi mbalimbali duniani bila mafanikio, hadi kilipopatikana na hatimaye kununuliwa nchini Afrika Kusini.

Ingawa hakutaja gharama za ununuzi wa kifaa hicho, Bi. Kamazima alisema ununuzi huo ulifanywa na kampuni ya Cats iliyoingia mkataba na wizara hiyo katika kuzikarabati kompyuta zake.

Hata hivyo, Bw. Mramba alisema hivi sasa hali imerejea kuwa ya kawaida ambapo Hazina imeshawasilisha mishahara hiyo kwenye wizara na katika halmashauri kwa ajili ya malipo.

’Kama kuna wafanyakazi hawajalipwa, nadhani ni kwa sababu ya taratibu za kibenki kutoka wizarani ama katika halmashauri husika,’ alisema.

Wakati huo huo, Bw. Mramba alisema Wizara hiyo itaanza kuwalipa wafanyakazi wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuanzia Septemba 19, mwaka huu.

Alisema, utaratibu na mfumo wa malipo hayo utatangazwa baadaye na Katibu Mkuu wa wizara hiyo.

Alisema, wizara hiyo itatumia kiasi cha Sh bilioni 50 kuwalipa wafanyakazi hao kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2005/2006.

’Kama tukimaliza kuwalipa na kuona kuwa bado kuna malipo ya ziada yanayohitajika, tutaendelea na zoezi hilo,’ alisema.

Aidha, Bw. Mramba alisema malipo yatakayotolewa yatawahusu wafanyakazi waliohakikiwa na kwamba zoezi la kuwahakiki wafanyakazi wengine (hakutaja idadi yao) bado linaendelea.

Gazeti-Nipashe

ISSN 0856-5414

Tarehe: Ijumaa Septemba 9,2005

My take:

Angalieni hizi tarehe vizuri sana na linganisheni na lini pesa zilichotwa benki kuu..
 
Vyombo vya habari vimebaini kuwa Mkurugenzi wa kampuni inayohakiki makampuni yanayochimba dhahabu Alex Stewarts Assayers ni mtoto wa Mhe. Basil Pesambili Mramba aliyekuwa Waziri wa Fedha wakati kampuni hiyo ilpopata mkataba huo Juni 2003. Katika miaka miwili ya mkataba huo, kampuni hii imekuwa inalipwa dola 751,267 sawa na sh. 939 millioni kila mwezi. Kwa muda wa miaka miwili imejikusanyia dola milioni 18 sawa na sh. 22.5 bilioni. Kampuni hii pia ilisamehewa kodi kwa notisi za serikali za Novemba 25 2005 iliyotiwa saini na aliyekuwa Waziri wa Fedha. Ni wazi kuna mgongano wa manufaa (conflict of interest) ya Waziri wa fedha kuipa mkataba kampuni ambayo mtoto wake ni mkurugenzi na pia kuisamehe kodi. Mpaka hivi sasa serikali haijatoa maelezo ya kina kufafanua utata huu ambao unaashiria matumizi mabaya ya madaraka kunufaisha familia yako ambayo ni rushwa. Rais anawajibika kulichunguza suala hili kwa kina na ikiwa taarifa ambazo zimeandikwa katika vyombo vya habari na vielelezo vyake zina chembe ya ukweli, basi waziri awajibishwe kwa kufukuzwa kazi na Tume ya Kuzuia Rushwa ichukue hatua za kisheria kuwafikisha wahusika mahakamani.

Kutoka: http://cuf-tz.com/666.html

1. BASIL P. MRAMBA

Mheshimiwa Basil Mramba ni Mbunge wa muda mrefu wa Jimbo la Rombo na Waziri wa Viwanda na Biashara na kwa miaka kumi ya utawala wa Rais Mkapa alikuwa ndiye Waziri wa Fedha. Katika kipindi hicho cha miaka kumi, Mheshimiwa Mramba amehujumu taifa la Tanzania kama ifuatavyo:

(i) Kwa kutumia wadhifa wake kama Waziri wa Fedha, alishinikiza kampuni ya Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation ya Washington DC, Marekani kupewa kazi ya kukagua mahesabu ya makampuni ya uchimbaji dhahabu. Chini ya mkataba wake na Serikali ya Tanzania, Kampuni hiyo inalipwa asilimia 1.9 katika ya asilimia 3 za mrahaba inaolipwa Serikali ya Tanzania na makampuni ya madini ya dhahabu. Kufuatana na barua ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu, katika mwaka wa fedha 2005/06, Alex Stewart (Assayers) walilipwa shilingi 14,175,753,189.46 kama malipo ya ukaguzi wa mahesabu ya makampuni ya dhahabu, ijapokuwa “hakuna ripoti za ukaguzi zilizowasilishwa na wakaguzi hawa kuhusu ukaguzi uliofanywa katika mwaka 2005/06”! Vile vile Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu alisema katika barua yake kwamba “hakuna ushahidi wowote wa kuthibitisha kwamba wakaguzi hawa wa dhahabu walipatikana kwa kufuata utaratibu wa zabuni ya ushindani.”

(ii) Vile vile kuna taarifa za kuwepo kwa rushwa na/au ufisadi mkubwa kuhusiana na mkataba kati ya Serikali na Alex Stewart Assayers. Barua pepe iliyoandikwa na Erwin Flores ambaye ni Makamu wa Rais Mtendaji wa kampuni hiyo ya Novemba 14, 2006 inamtaja mtu mmoja mwenye jina la Bwana Basil ambaye ana wadhifa wa Waziri katika serikali ya Jamhuri ya Muungano na kuwa yeye pamoja na wenzake ambao hawakutajwa wana asilimia 12.5 za hisa kwenye kampuni hiyo na kuwa analipwa na kampuni hiyo. Kwa mujibu wa Flores, hakuwezi kukawa na ushahidi wowote kuthibitisha kwamba ‘Bwana Basil’ anapokea malipo kutoka kwa Alex Stewart kwa vile malipo yote kwake yamekuwa yakifanyika nje ya nchi. Kwa kadri tunavyofahamu, mtu pekee aliyekuwa waziri katika serikali ya Awamu ya Tatu na ambaye pia ni waziri katika Serikali ya Awamu ya Nne na ambaye ana jina la ‘Basil’ ni Mheshimiwa Basil Pesambili Mramba. Tumemtaka Waziri wa Fedha kutupatia nakala ya Mkataba kati ya Benki Kuu na Alex Stewart, na kuwataka Mheshimiwa Basil Mramba na Erwin Flores walete maelezo yao kwetu kwa mujibu wa Sheria ya Mamlaka, Haki na Kinga za Bunge ya mwaka 1988 kwa barua yetu ya tarehe 18 Julai 2007 ili waweze kujibu tuhuma hizi. Bado tunasubiri majibu hayo

Chanzo: "Orodha ya Mafisadi"- Dr Slaa, Tundu Lissu et al
 
Hivi ngoja niulize: inakuwakuwaje kikundi kidogo cha watu ukilinganisha na raia wote kwa ujumla kinakuwa na madaraka na uwezo wa kufanya chochote kipendacho halafu sisi tulio wengi tunakaa na kulia lia tu bila kufanya kweli? Hii inawezekanaje?
 
Rwabugiri, hilo ndilo tatizo.. watu wa kuwabana ni kina Mgonja, kwanini baada ya kutoka Wizara ya Fedha akapelekwa Hazina?
Hadi hivi sasa kazi imeshaanza. Jumamozi Mkurugenzi wa BoT katika mkoa mmoja wa Kanda ya Magharibi alikuwa anashikiliwa na Polisi... Ndani ya hiyo ripoti kuna majina ya watu karibu 40 ambao wanahusika na upotevu huo wa fedha..

Ili wajue sisi tukiipata hiyo ripoti tutaiweka hadharani, ni jukumu lao kuilinda!

Mkuu hapo umenichanganya, kwani kuna tofauti ya Wizara ya Fedha na Hazina? Maana najua Mgonja alikuwa katibu mkuu Hazina mda mrefu akishirikiana na Penieli Lymo aliyepelekwa Kilimo na sasa wizara inabaki na PS mmoja ambaye ni Mgonja. Ikumbukwe pia kwamba bodi ya wakurugenzi wa BOT ndio imepewa mamlaka ya kushughulikia hili sakata wakti huo huo Mgonja kutokana na cheo chake ni Bod member wa BoT sasa kuna uwazi hapo kweli?
 
Mkuu hapo umenichanganya, kwani kuna tofauti ya Wizara ya Fedha na Hazina? Maana najua Mgonja alikuwa katibu mkuu Hazina mda mrefu akishirikiana na Penieli Lymo aliyepelekwa Kilimo na sasa wizara inabaki na PS mmoja ambaye ni Mgonja. Ikumbukwe pia kwamba bodi ya wakurugenzi wa BOT ndio imepewa mamlaka ya kushughulikia hili sakata wakti huo huo Mgonja kutokana na cheo chake ni Bod member wa BoT sasa kuna uwazi hapo kweli?

Quote:
Rwabugiri, hilo ndilo tatizo.. watu wa kuwabana ni kina Mgonja, kwanini baada ya kutoka Wizara ya Fedha akapelekwa Hazina?
Hadi hivi sasa kazi imeshaanza. Jumamozi Mkurugenzi wa BoT katika mkoa mmoja wa Kanda ya Magharibi alikuwa anashikiliwa na Polisi... Ndani ya hiyo ripoti kuna majina ya watu karibu 40 ambao wanahusika na upotevu huo wa fedha..

Ili wajue sisi tukiipata hiyo ripoti tutaiweka hadharani, ni jukumu lao kuilinda!


Nadhani Mjj alikuwa anamaanisha kutoka BoT kwenda Hazina
 
Hivi ngoja niulize: inakuwakuwaje kikundi kidogo cha watu ukilinganisha na raia wote kwa ujumla kinakuwa na madaraka na uwezo wa kufanya chochote kipendacho halafu sisi tulio wengi tunakaa na kulia lia tu bila kufanya kweli? Hii inawezekanaje?


Inawezekana! angalia makelele humu tunayopiga. Nyani wee Giladi Yee-Huko masikioni wanaona hizi zilipendwa(contemporary)!

My view...Hii ni njaa yetu iliopata kiinua mgongo(Ufisadi/Mafisadi)-mda mrefu tulitaka Kujikomboa au Kujichotea kiuchumi- balaa lake ndilo hilo watu wachache kwa kutumia tactics za umafia kuteka shehena kubwa ya Uchumi wa Mtanzania.
 
Basil has to go too!!

Yes SYLLOGIST...it is a family (MAFIA) business....don't interrupt!!
 
Hivi ngoja niulize: inakuwakuwaje kikundi kidogo cha watu ukilinganisha na raia wote kwa ujumla kinakuwa na madaraka na uwezo wa kufanya chochote kipendacho halafu sisi tulio wengi tunakaa na kulia lia tu bila kufanya kweli? Hii inawezekanaje?

Nyani,

Nitumie msg uulize maswali yako yote ya namna hiyo kwenye PM nitakujibu.

Kwa ufupi watu wamejipanga na kupangika, in the near future uongozi na hatma ya nchi hii kiuchumi na utawala utakuwa unaamuliwa na baadhi ya watu.

Kinachonishangaza hawa jamaa zetu wajiitao "usalama wa Taifa", hivi hawaoni chochote? Uzalendo kweli umewaishia ndugu zangu? au nyie ni wamarekani? Shauri zenu watoto wenu watakapokuwa House boys na hose girls za hao mnaowalinda!

Fisadi Daima
 
Quote:
Rwabugiri, hilo ndilo tatizo.. watu wa kuwabana ni kina Mgonja, kwanini baada ya kutoka Wizara ya Fedha akapelekwa Hazina?
Hadi hivi sasa kazi imeshaanza. Jumamozi Mkurugenzi wa BoT katika mkoa mmoja wa Kanda ya Magharibi alikuwa anashikiliwa na Polisi... Ndani ya hiyo ripoti kuna majina ya watu karibu 40 ambao wanahusika na upotevu huo wa fedha..

Ili wajue sisi tukiipata hiyo ripoti tutaiweka hadharani, ni jukumu lao kuilinda!


Nadhani Mjj alikuwa anamaanisha kutoka BoT kwenda Hazina

Okay Mfuatiliaji hapo nimekupata kaka.

Sasa hii issue iko hivi, Mgonja alikuwa BOT alipo kuja mkapa akampeleka Hazina kwa secondment (kwa kuazimwa) na mktataba wake nasikia ulishaisha ilikuwa arudi BOT kwa sababu yeye sio mtu wa payrol ya hazina bali ya BOT. Jamaa kwa kuwa ni mchezaji kiungo wa (Midfilder) wa Ufisadi ilibidi wamuongezee mda wa kuwa PS hazina. Watu wengi walitegemea Kija ambaye ni naibu PS ndie angechukua hiyo nafasi lakini mambo hayakuwa vile. So Mgoja ni mtu muhimu sana kwa timu nzima ya mafisadi. Huyu jamaa ni member bodi wa BOT kwa hiyo anajua kila kitu, huyu jamaa nadhani ni mwenyekiti wa bodi ya NSSF sijui nako huko ni mambo gani yanaendelea. Anamengi huyu na ndio maana alitishia kwenda Mahakamani lakini akaishia getini.

Mramba na Mgonjwa go! go! go! na washitakiwe kwani hawa si ni wezi kama wanao robe mabenki?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom