BoT na CMSA wautahadharisha umma kuhusu Taasisi ya Upatu ya D9 Club

Nmefurahi sana maana nlidhan mmetusahau watanzania maana weng wanaibiwa kuna dada kashatoa million 4.kambiwa kila week ataingiziwa laki 4 lakin zitakatwa riba ila mpaka sasa hakaingiziwa hata sh. 500 ya silver hii ni hatari.....

Pia BOT muwe mnawah kutoa taarifa coz D9 ipo muda kdg toka ianze kutangazwa so n vyema mnapoona mambo haya haraka sana mnataarifu wananchi maana weng wanataamaaa na pesa za haraka haraka na hawajui hzo pesa znazalishwa vp had mtu akupe ww milllion 16 kwa kuwa umetoa million 4??? Okay jamn sambazan hiyo barua nanyi tuwaokoe ndugu zetu wanaoliwa
Inaonekana unaumia sana watu wanapopiga hela.....
 
Hii kitu ina miaka na miaka na sijawahi kusikia kwamba mtu analalamika ameibiwa. Kwa hyo ni vema wange eleza ni watu gani waliowekeza huko walio lalamika kuibiwa . vinginevyo ni chuki tu za kutaka wachache ndio watajirike and the rest wabaki . Uzuri wake hii kitu inachezwa mtandaoni sijui kama wataweza. Miezi mitatu ela yako imerudi sasa hapo mtu anatapeliwaje. Mfano mm mwenyewe huu mwezi wa sita , nimerudisha ela yangu miezi mitatu ya mwanzo na sasa nimeshakula faida ya 2m miezi miwili na bado saba. Hapo wakisitisha huduma zao utasrmaje nimeibiwa
Muda Umefikia sasa wa kusikia walioibiwa kwa vile new members wanaenda kutoweka, malipo yalikua yanatoka kwa Wateja wapya ndo maana watu wanahangaika kushawishi wenzao, subiri wote wapate taarifa baada ya wiki tatu utawasiki walio tapeliwa mbaya zaidi kwa wale new members Sababu watakua hawawezi kurudisha pesa yao
 
Kuna bit coin pia mkuu....hebu nayo imulikwe
Bit coin ni mfumo wa malipo wa kielectronic ambao mtu anaweza kutumia kuafanya malipo, huwa ni vigumu kutrace malipo na pia hakuna sheria Kama za mabenki hiyo biashara haramu kwenye mitandao zimekua zikiupenda zaidi, hata kile kirusi cha juzikati (ransomware) kilihitaji malipo yafanyike Katika mfumo wa bitcoin, mfumo wenyewe hauna shida watumiaji kama d9 ndo wanashida Kama vile bastola inaweza kutumiwa kiusalama na kwa uhalifu inategemea na mtumiaji
 
Ukiona vitu kama hivi vinashamiri ujue hali ya uchumi ni mbaya .Watu hawana cha kufanya au namna ya kujiingizia kipato sasa wanatafuta hela za chapchap.
 
Mamlaka imetoa tahadhari kwa umma kwamba, taasisi ijulikanayo kama D9 Club inayotangaza au kushawishi, pamoja na mambo mengine ununuzi wa hisa, inafanya hivyo bila vibali vya mamlaka husika. Kumekuwepo na Michango tofauti kupitia JamiiForums kuhusiana na Taasisi=>D9 Club, upatu unaosambaa kwa kasi Tanzania kama moto wa kifuu. Tuwe makini.
View attachment 523909

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) zinapenda kuutahadharisha umma kwamba, taasisi ijulikanayo kama D9 Club inayotangaza au kushawishi, pamoja na mambo mengine ununuzi wa hisa, inafanya hivyo bila vibali vya mamlaka husika.

Ni imani ya BoT na CMSA kuwa ushawishi unaofanywa na D9 Club kwa umma kushiriki katika mpango wao utasababisha watu kupoteza fedha zao, na pia ni kinyume na Sheria ya Makosa ya Jinai Sura ya 16 ya Sheria za Tanzania ambayo katika Fungu la 171A,171B na 171C, ni kosa la jinai kuendesha, kushawishi watu kushiriki, na kushiriki au kuchangia fedha katika upatu.

Ifahamike kwamba upatu haramu hubuniwa kwa namna ambayo fedha za kila mshiriki mpya hutumika kumlipa mshiriki aliyetangulia, na hakuna maelezo ya namna yoyote ya kuwekeza au kuzalisha fedha hizo.

Kwa taarifa hii, umma unasisitizwa kutoshawishika kwa namna yoyote ile kushiriki katika upatu uliobuniwa na D9 Club na mipango mingine ya aina hiyo. Aidha, wananchi watoe taarifa kwa vyombo vinavyohusika, ikiwemo Benki Kuu ya Tanzania, Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana na vyombo vya usalama (Polisi) kuhusiana na mikutano au mafunzo yanayoendeshwa na D9 Club na mipango mingine haramu kama inayofanana na huo.

Imetolewa na:

BENKI KUU YA TANZANIA & MAMLAKA YA MASOKO YA

MITAJI NA DHAMANA

14 Juni 2017

Kwa maelezo zaidi wasiliana na: kanyoni@bot.go.tz & info@cmsa.go.tz

Kwa kagame marufuku
 
Mimi huwa sifanyi biashara za Mitandaoni! kwa sababu mara nyingi ni vigumu kufahamu mumiliki halali ni nani, anapatikana wapi na pia kuna kiwango kidogo cha usalama!
Mmiliki halali anaitwa Danilo Santana na tarehe 7 July anaingia Dar. atakuwa pale Mlimani City na atapewa escort ya king'ora kutoka serikalini. Akishaondoka ndo mtajadili juu ya utapeli. Uganda kuna registered office ambayo ina operate kwa ajili ya Tanzania, Kenya na Uganda. ofisi nyingine iko Nigeria. Usipofanya wewe haizuii wengine kufanya. Hata hapa Dar ipo ofisi ndogo inayosimamiwa na ofisi ya Uganda na ndio inayoandaa mapokezi ya CEO wa D9. Wala hajifichi na biashara sio upatu. Ukiingia leo unapewa contract ya mwaka mmoja kwa hela yako. Kuingiza watu ni kutaka kuongeza kipato tu ila kama una shughuli zako nyingine unaendelea tu.
 
Muda Umefikia sasa wa kusikia walioibiwa kwa vile new members wanaenda kutoweka, malipo yalikua yanatoka kwa Wateja wapya ndo maana watu wanahangaika kushawishi wenzao, subiri wote wapate taarifa baada ya wiki tatu utawasiki walio tapeliwa mbaya zaidi kwa wale new members Sababu watakua hawawezi kurudisha pesa yao
Malipo yapo kama kawaida mkuu. Ni biashara ya mtandaoni na inatoka kimtandao. Kwa wenzetu nje unatoa bank through bitcoins ila huku kwa vile tumezoea ujamaa na kujitegemea huku migodi ikiuzwa ndo mnalishwa umbea eti ni upatu. Hii ni biashara. Kama hujui ni bora ukajifunza kulikokusema watu wanaibiwa wakati watu tunakula hela kihalali.
Haya mabenki yanayojifanya kumjali mwananchi mbona tukienda akuomba mikopo hata ya 5m wanazingua eti mp uwe na dhamana. Leo ndo wamekuwa watetezi wa wananchi? Wana hofu maana wenye akili wanatoa fixed zao ambapo unapata faida ndogo.
 
Wapendwa wanaJF,

leo nimekutana na vijana fulani wako very aggressive kuna njia mpya {networking ....] unawekeza kati ya US dola 50 - 20,000 na unapata daily return ya 1% - 1.9% kila siku. details www.amazontraders.co.uk.

Hawajamaa hawana ofisi yeyote nchini wala east africa, kwa kandaa hii ipo Africa Kusini tu. Swali kwa wajuzi je hii sio ponzi game?

mfano ukiwekeza USD 50 kwa siku unapewa 1% sawa na cent 50 kwa siku 360 unapata USD 180.

swali hiyo fedha inatoka wapi? kwenye kabrash lao wanasema amazon wanajihusisha na ununuaji na uuzaji wa hati fungani na HISA kwenye masoko mbali mbali, lakini je masoko hayo yangekuwa na faida kubwa si kina mengi, MO na wangine wangeachana na viwanda na kuwekeza kwenye masoko hayo?

Lakini assume kama ni kweli hiyo biashara inalipa na ni halali, je incase of bankruptcy/kufilisika waliowekeza wanapataje fedha zao walizowekeza?

kwa wale wenye uelewa zaidi waje tueleweshane hapa.

hakuna kutoleani bunduki au povu hapa tujulishane maana vinginevyo taifa litaangamia kwa jinsi nilivyoona trend.
 
watanzania ni watu rahisi sana kuibiwa

1. Kuna wanaobet wakitarajia miujiza ya kupata hela ya mkupuo...........WAPO

2. kuna wanaoiba hela za matumizi ya familia na kupeleleka kwenya upatu uitwao " mchezo" @ vikoba......WAPO

3. kuna wanaojiunga na mitandao mbalimbali ya pyramidy schemes wakidanganywa kupata fedha za mkupuo......WAPO

4. Kuna wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji matapeli kupeleka fedha zao eti zifanyiwe manuva ziwe nyingi ......WAPO

5.Kuna wanaopeleka kiasi kikubwa cha fedha kwenye makanisa ya kisasa yaitwayo 'UPAKO' wanadanganywa eti wanapanda mbegu na watanunua magari wakati fedha hizo wachungaji wao wanatanua nazo mpaka kununua ndege....WAPO

6.kuna wagojwa wanaibiwa na matapeli wapya waitwao "SANITARIUM CLINIC" kwa kushikishwa kikompyuta cha kibashite eti kinaangalia magojwa mwili mzima na kutoa sumu mwilini.......WAPO
 
Wadau tuambieni mmefikia wapi na upatu wa hawa jamaa bado mnavuta madolari?
 
Wasiliana nami via watsup 0676790927 (Edgar)
Facebook username: Edgar Mfala
Kama utataka kufahamu zaidi kuhusu D9 hiki nikitu cha kweli

Natamani waandishi was habari was Tanzania waende kuona kesho kitachotokea huko Uganda,maana ni sherehe kubwa za D9 zinafanyika hapoo na watu wataondoka na magari nna zawadi kemkem

Hizo picha ni maandalizi tuu.
Endelea kuzubaaa ukisema ni deci

Kuna advocate alikua akielezea kuhusu D9 on NTV ngoja niwarushie video,mwenye macho aambiwi Tazama
 

Attachments

  • IMG-20170708-WA0017.jpg
    IMG-20170708-WA0017.jpg
    45.8 KB · Views: 70
  • IMG-20170708-WA0016.jpg
    IMG-20170708-WA0016.jpg
    81.4 KB · Views: 80
  • IMG-20170708-WA0015.jpg
    IMG-20170708-WA0015.jpg
    96 KB · Views: 70
  • IMG-20170708-WA0014.jpg
    IMG-20170708-WA0014.jpg
    102.2 KB · Views: 68
  • IMG-20170708-WA0013.jpg
    IMG-20170708-WA0013.jpg
    72.2 KB · Views: 57
  • IMG-20170707-WA0075.jpg
    IMG-20170707-WA0075.jpg
    59.4 KB · Views: 58
  • IMG-20170707-WA0076.jpg
    IMG-20170707-WA0076.jpg
    48.4 KB · Views: 65
  • IMG-20170707-WA0074.jpg
    IMG-20170707-WA0074.jpg
    29.4 KB · Views: 71
  • IMG-20170707-WA0073.jpg
    IMG-20170707-WA0073.jpg
    44.2 KB · Views: 59
  • VID_20170708_201113.mp4
    9.4 MB · Views: 36
Back
Top Bottom