BOT inafanya MNADA mida hiii!!

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,985
20,263
Kama siamini ninachokiona kwa macho yangu dk hii,yani kuna mnada kama ile ya majembe aksheni mati inayofanyikaga maeneo ya stende au sehemu za wazi, laki leo huu unafanyika ndani ya bot kwenye maegesho ya magari juu ya gorofa ya nne!

Kinacho nadiwa hapa kuanzia magari mpaka kijiko cha chai!
Najaribu kufuatilia uhusiano wa BOT na bidhaa hizi!

UPDATES:

Nichogundua kuna dizaini mpya ya ufisadi unaofanyika ktk wizara zetu! Hawa wanaoendesha mnada wameniambia kuwa wao wamekodi ukumbi lakini wamegoma kujitaja kuwa ni kampuni gani ya udalali na nani amewapangisha!
Nimejaribu kuwasiliana na mmoja wa maafisa anaehusika na uratibu wa maegesho hayo anasema yeye hupo likizo na hajui nini kinaendelea na hawana utaratibu wa kukodisha kwa shughuli yoyote ile!

Updates:
Nilichobaini baada ya mchakato wa masaa mawili wa kujua uhusiano wa mali zinazo nadiwa na bot nimegundua kuwa ni mali za serikali nyingi zimeandikwa namba za vitengo vya wizara!
Nimebahatika kuongea na watu wawili ambao ni wafanyakazi wa bot na wizara ya fedha wamenithibitishia kuwa ni mali za wizara zilizotumika, nikawauliza kuwa je huo ndio utaratibu wa wizara kuuzia kwenye kwenye paking wakasema wao si wasemaji ila wapo kwa uangalizi tu!

Chaajabu baadhi ya namba za kwenye bidhaa hizo zimefutwa na magari yana no za kiraia!
Hata aina ya uuzaji ni kama kugawana maana watu si wengi na wanatoa taarifa za uongo ukijaribu kuzungumza nao!
 
mnada wanafanyikia kwenye BOT?............................................................KWANINI?
 
mnada wanafanyikia kwenye BOT?............................................................KWANINI?
Hii ndo tz kila kitu kinawezeka ndugu!
Usihangae siku unaambiwa ikulu yetu ya dar ni kijiwe cha wezi duniani
 
kwa hali ya sasa-hilo ni jambo la kawaida,kama ikulu kunafanyika biashara,sembuse bot?
ikiwezekana wapige manada na hayo majengo kabsa.....
 
Sio vya bot ila jamaa wanafanya kazi ya kukodisha zile paking siku za weekend

JB Umekosea, hukufanya uchunguzi wako vizuri. Ungenunua hata kijiko uone risiti unayopewa ni ya kampuni gani. Nasikitika kukwambia kuwa, umepotosha JAMVI. Zile parking haziwezi kamwe kukodishwa kwa ajilli ya shughuli kama hizo.
 
Jason Bourne again..em fatilia vizuri mzee wa za jikoni isije ikawa na uhusiano na BoT..sasa hii ni balaa
 
JB Umekosea, hukufanya uchunguzi wako vizuri. Ungenunua hata kijiko uone risiti unayopewa ni ya kampuni gani. Nasikitika kukwambia kuwa, umepotosha JAMVI. Zile parking haziwezi kamwe kukodishwa kwa ajilli ya shughuli kama hizo.
Hata mimi nilistuka hivyohivyo baada ya kusikia matangazo kupitia spika kubwa ndani ya paking hizo ndipo nika amua kuingia tena unaingilia huku geti la bot kabisa!

Hakuna risiti inayotolewa ya maana ila imeaandi Cash Sale kisha jina la aliyenunua yani ni ya kihuni tu!
Ukitaka kuthibitisha nenda pale bot waone walinzi au sogea kwenye ofisi ya John Tendwa panawalinzi waulize hao ndio walionisaidia mpaka nikafika sehemu ya mnada huo! Mara ya kwanza nilidhani kuna shere ya kipaima mara nikasikia 2000!,3000,5000,
 
Updates:
Nilichobaini baada ya mchakato wa masaa mawili wa kujua uhusiano wa mali zinazo nadiwa na bot nimegundua kuwa ni mali za serikali nyingi zimeandikwa namba za vitengo vya wizara!
Nimebahatika kuongea na watu wawili ambao ni wafanyakazi wa bot na wizara ya fedha wamenithibitishia kuwa ni mali za wizara zilizotumika, nikawauliza kuwa je huo ndio utaratibu wa wizara kuuzia kwenye kwenye paking wakasema wao si wasemaji ila wapo kwa uangalizi tu!

Chaajabu baadhi ya namba za kwenye bidhaa hizo zimefutwa na magari yana no za kiraia!
Hata aina ya uuzaji ni kama kugawana maana watu si wengi na wanatoa taarifa za uongo ukijaribu kuzungumza nao!
 
Updates:
Nilichobaini baada ya mchakato wa masaa mawili wa kujua uhusiano wa mali zinazo nadiwa na bot nimegundua kuwa ni mali za serikali nyingi zimeandikwa namba za vitengo vya wizara!
Nimebahatika kuongea na watu wawili ambao ni wafanyakazi wa bot na wizara ya fedha wamenithibitishia kuwa ni mali za wizara zilizotumika, nikawauliza kuwa je huo ndio utaratibu wa wizara kuuzia kwenye kwenye paking wakasema wao si wasemaji ila wapo kwa uangalizi tu!

Chaajabu baadhi ya namba za kwenye bidhaa hizo zimefutwa na magari yana no za kiraia!
Hata aina ya uuzaji ni kama kugawana maana watu si wengi na wanatoa taarifa za uongo ukijaribu kuzungumza nao!

Huo mnada wa zana za serikali ulitangazwa wapi?
 
Back
Top Bottom