The Monk
Platinum Member
- Oct 12, 2012
- 19,254
- 42,873
Ukiusoma huo mwongozo vizuri,unawapa mabenki uhuru wa kuamua kufuata hayo masharti au lah-we have a very long way to go.Njia thabiti ni mabenki yenyewe kulazimishwa na hali ya soko kushusha riba.Kiuhalisia riba za Tanzania ni kubwa mno mno.
Mkuu hali ya soko itasukuma mabenki kushusha riba. Watu siku hizi hawaangalii jina la benki unakoweka pesa zako, wanachofuata ni huduma wanayotaka kama inapatikana.
Leo hii benki yeyote ikishusha riba, watu wataambizana tu kwamba kuna benki wana riba ndogo za mikopo, watu watakimbilia huko, hiyo italazimisha benki zingine zishushe kunusuru kukimbiwa na wateja.
Ikiwa mtu hana ulazima wa kukopa sasa hivi bora akasubiria kidogo hadi mwakani hizi sheria na taratibu zikianza kutumika, unaweza kukopa sasa hivi ukapigwa riba ya sasa baadae wakija kubadili unaendelea kulipa mkopo kwa ile ile riba ya zamani.
Ilinikuta hii nilikua nalipa 22.5% wakati benki walishusha hadi 16%. Na walikua wananibembeleza nichukue tena nikawaambia nikitaka ntaenda tena. Kwa hii habari, tutaonana mwakani tena ikishakua 10%.