Bosi wa meli iliyoua aibuliwa: AYOUB Hashim Jaku, mbunge wa Bunge la Muungano (CCM) anatajwa

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
picture-11.jpg

Na Jabir Idrissa - Imechapwa 14 September 2011

Ndani ya Jamii
jaku.jpg



AYOUB Hashim Jaku, mbunge wa Bunge la Muungano (CCM), ni mmoja wa wanaotajwa kumiliki meli ya mv Spice Islander 1 iliyozama na kuangamiza maisha ya watu zaidi ya 250 visiwani Zanzibar.

Jaku ameingia bungeni kupitia nafasi tano za wabunge wanaotokana na baraza la wawakilishi Zanzibar. Ni mwakilishi wa jimbo la Muyuni, mkoa wa Kusini Unguja.
Taarifa kutoka ndani ya serikali ya Muungano, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) na Chama Cha Mapinduzi (CCM), zinasema Jaku anamiliki meli hiyo, pamoja na wafanyabiashara wengine wanne.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, wamiliki wengine wa meli hiyo, ni familia ya mfanyabiashara maarufu visiwani, Salum Battash, pamoja na mfanyabiashara mwingine aliyefahamika kwa jina moja la Thinei anayeishi Dubai.


Meli ya mv Spice Islander 1 ilizama usiku wa manane Ijumaa iliyopita, katika mkondo mkuu wa Nungwi, kaskazini mwa kisiwa cha Unguja.


Katika ajali hiyo mbaya ya kwanza kutokea katika historia ya Zanzibar, watu 610 wameripotiwa kuokolewa wakiwa hai.


Hata hivyo, takwimu hizo bado zina utata kutokana na watu mbalimbali kuripoti kutowaona ndugu zao.


MwanaHALISILI lilipowasiliana na Jaku kutaka kufahamu umiliki wake katika meli hiyo, alikana kuhusika na lolote katika meli hiyo.


Alisema, "Mimi sihusiki katika hao wanaotajwa kumiliki meli hii. Sina hisa na wala siwafahamu wamiliki wake."


Alipoambiwa gazeti hili limeelezwa kuwa jina lake linatajwa ndani ya viongozi wa serikali na jeshi la polisi kuwa mmoja wa wamiliki wa meli ya mv Spice Islander 1, Jaku alisema, "Hao wananitaja tu. Mimi simo."


Hata hivyo, MwanaHALISI limedokezwa na vyanzo vyake vya ndani kwamba Jaku ni mmoja wa wamiliki wa meli hiyo; mara kadhaa amekuwa akionekana bandarini kufuatilia kazi za meli yake.


"Sikiliza kijana, hii meli ni Jaku na wenzake. Sisi ndani ya serikali tunafahamu hivyo; nyaraka tulizonazo zinaonyesha hivyo pia," ameeleza kiongozi mmoja mwandamizi ndani ya serikali ya Zanzibar.


Habari zinasema jina la Jaku na Battash limetajwa hata ndani ya kikao cha viongozi wakuu wa visiwani kilichoshirikisha Kamati ya Kudumu ya Bunge, ulinzi na usalama kilichofanyika Zanzibar, juzi Jumatatu.


Meli hiyo iliyotengenezwa nchini Ugiriki mwaka 1967 (miaka 44 iliyopita) na kupewa jina la Mariana ilibeba zaidi ya abiria 1000.


Mwaka 1988 mmiliki wa meli hiyo aliuza na kupewa jina la Apostolos na mwaka 2007 iliuzwa tena kwa kampuni ya Honduras, ya nchini Marekani Kusini, na kupewa jina la sasa la mv Spice Islander.


Hadi sasa, hakuna taarifa yoyote kutoka serikalini inayoeleza sababu ya kuzama kwa meli hiyo.


Hata hivyo, duru huru za kiuchungizi zinasema meli ya mv Spice Islander 1 imezama kutokana na kuzidiwa na uzito wa mizigo na abiria.


Serikali ya Zanzibar imesita kutaja mmiliki wa meli hiyo, jambo ambalo linatiliwa shaka na baadhi ya wachambuzi kwamba linalenga kuendeleza utamaduni wa kulindana.


"Ndugu yangu, hapa Zanzibar hakuna asiyefahamu kuwa Jaku ndiye mmiliki wa meli hii. Lakini inaoenekana wakubwa wanataka kuficha ukweli. Sisi tunajua kwamba, kila meli ikitia nanga Zanzibar, Jaku anafuatilia utendaji wake," anaeleza Farahani Saidi, mmoja wa wabeba mizigo bandarini Unguja


 
Wow... Siku hizi Wabunge wetu woote ni Wafanya Biashara, hawajali Uhai wa Wananchi... MORE POWER TO AZIMIO LA ZANZIBAR!!!
 
Si ndio hawa walisema SUMATRA wafungashe?
Sasa kinaeleweka, tunapata magulio ya wafanya biashara badala ya wawakilishi wawanchi.
 
Kwa wale wanaotaka kuona picha za meli hii ni hizi hapa. Utashangaa kuona ni jinsi gani meli hii iliweza kurusuhusiwa kusajiriwa kubeba abiria nchini, kwa jinsi inavyotisha kwa kuoza hata kwa kuonekana!
 

Attachments

  • Spice Island.pdf
    358.9 KB · Views: 159
Huu ni mwanzo mzuri na nina matumaini kwamba sheria itaendelea kuwa msumeno bila kujali nafasi ya mtu katika jamii.
 
Wow... Siku hizi Wabunge wetu woote ni Wafanya Biashara, hawajali Uhai wa Wananchi... MORE POWER TO AZIMIO LA ZANZIBAR!!!

Hakuna dhambi kwa mtu kuwa mbunge na mfanyabiashara, kama anazingatia maadili ya kazi na biashara zake, pamoja na kuzingatia sheria za nchi.
 
Spice Islander I: Wikipedia: Built in 1967 as Marianna for an unknown owner, she was later sold to Theologos P. Naftiliaki, Piraeus, Greece. In 1988, Marianna was sold to Apostolos Shipping and renamed Apostolos P. She was later sold to Saronikos Ferries and placed in service on the Piraeus - Aegina - Angistri route.

In 2005, Apostolos P was registered to Hellenic Seaways. In 2007, she was sold to Makame Hasnuu, Zanzibar, Tanzania and renamed Spice Islander I.

On 25 September 2007, Spice Islander I was off the coast of Somalia when she experienced engine problems due to contaminated fuel. After the alarm had been raised via Kenya, USS Stout from Combined Task Force 150 was sent to her aid.

The ship was on a voyage from Oman to Tanzania and was not carrying any passengers. USS James E. Williams also responded. Stout provided the ship with 7,800 US gallons (30,000 l; 6,500 imp gal) of fuel and supplied the ten crew with food and water. After her engines were restarted, she resumed her voyage to Tanzania.
 
Hakuna dhambi kwa mtu kuwa mbunge na mfanyabiashara, kama anazingatia maadili ya kazi na biashara zake, pamoja na kuzingatia sheria za nchi.

Hapa kwetu bado hatuna Wafanyabiashara ambao wameingia kwenye SIASA kusaidia wananchi; Angalia wote wana Maslahi yao Ndani ya Nchi Hii

Nipe Mfano wa Mfanyabiashara ambaye sio Maluki ndani ya Bunge
 
Hapo kuanzia waziri wa uchukuzi mpaka meneja wa banbari wanatakiwa waachie ngazi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hakuna dhambi kwa mtu kuwa mbunge na mfanyabiashara, kama anazingatia maadili ya kazi na biashara zake, pamoja na kuzingatia sheria za nchi.

mshika mawili....kama unataka kufanya biashara fanya biashara kama unataka kutumikia wananchi kama Baba wa taifa Nyerere tumikia wananchi, sio kushika kote....shida ipo kwani ikija ishu ya kutoa tenda lazima atapendele kampuni yake hata kama haina vigezo....
 
Hapo kuanzia waziri wa uchukuzi mpaka meneja wa banbari wanatakiwa waachie ngazi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kwa wale wanaotaka kuona picha za meli hii ni hizi hapa. Utashangaa kuona ni jinsi gani meli hii iliweza kurusuhusiwa kusajiriwa kubeba abiria nchini, kwa jinsi inavyotisha kwa kuoza hata kwa kuonekana!

Dah! Kama meli yenyewe ndio ilikuwa hivi ilikuwa hamna haja ya kusajiliwa.............Poor Tanzania.
 
Back
Top Bottom