kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,839
- 17,437
Boris Johnson ajiunga na Biden, watwanga usingizi katikati ya mkutano wa tabianchi, Glasgow
Nov 03, 2021 10:48 UTC
Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amejiunga na Rais wa Marekani Joe Biden na kutwanga usingizi mfupi wakati wa vikao vya Mkutano wa Hali ya Hewa unaofanyika Glasgow huko Scotland.
Picha ilizosambaa mitandaoni ya mojawapo ya vikao vya jana, Jumanne huko Grasgow, inamuonyesha Johnson akiwa amezama kwenye uingizi bila ya kuwa na barakoa akiwa karibu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na mwanaharakati wa hali ya hewa wa Uingereza Sir David Attenborough, ambaye ana umri wa miaka 95.
Katika kikao cha Jumatatu iliyopita Rais Joe Biden wa Marekani pia alionekana kwenye picha za video na kamera zilizonasa matukio ya shughuli za vikao vya mkutano huo, akiwa amechapa usingizi, jambo ambalo limemfanya adhihakiwe katika mitandao na vyombo vya habari kote duniani.
[https://media]Joe Biden katika mkutano wa Glasgow
Nchini Uingereza waandishi wa habari na wanasiasa wamemkosoa Boris Johnson kutokana na jinsi anavyoonekana akiwa amelala kwenye kikao hicho wakisema kuwa picha hiyo haiendani na tukio la hali ya hewa duniani.
Mbunge David Lammy wa Uingereza ameandika katika mtandao wa Twitter kwamba: "Ni wakati wa Boris Johnson kuamka, dunia inaungua. Sir David Attenborough anazingatia mgogoro wa hali ya hewa, hivyo ni wakati wa serikali yako pia kufanya hivyo."
Viongozi kutoka nchi zaidi ya 100 duniani wanahudhuria mkutano huo wa 26 wa kujadili mabadiliko ya tabianchi, ulioanza tarehe 31 Oktoba na kuendelea hadi tarehe 12 ya mwezi huu wa Novemba mjini Glasgow, Uskochi.
Nov 03, 2021 10:48 UTC
Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amejiunga na Rais wa Marekani Joe Biden na kutwanga usingizi mfupi wakati wa vikao vya Mkutano wa Hali ya Hewa unaofanyika Glasgow huko Scotland.
Picha ilizosambaa mitandaoni ya mojawapo ya vikao vya jana, Jumanne huko Grasgow, inamuonyesha Johnson akiwa amezama kwenye uingizi bila ya kuwa na barakoa akiwa karibu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na mwanaharakati wa hali ya hewa wa Uingereza Sir David Attenborough, ambaye ana umri wa miaka 95.
Katika kikao cha Jumatatu iliyopita Rais Joe Biden wa Marekani pia alionekana kwenye picha za video na kamera zilizonasa matukio ya shughuli za vikao vya mkutano huo, akiwa amechapa usingizi, jambo ambalo limemfanya adhihakiwe katika mitandao na vyombo vya habari kote duniani.
[https://media]Joe Biden katika mkutano wa Glasgow
Nchini Uingereza waandishi wa habari na wanasiasa wamemkosoa Boris Johnson kutokana na jinsi anavyoonekana akiwa amelala kwenye kikao hicho wakisema kuwa picha hiyo haiendani na tukio la hali ya hewa duniani.
Mbunge David Lammy wa Uingereza ameandika katika mtandao wa Twitter kwamba: "Ni wakati wa Boris Johnson kuamka, dunia inaungua. Sir David Attenborough anazingatia mgogoro wa hali ya hewa, hivyo ni wakati wa serikali yako pia kufanya hivyo."
Viongozi kutoka nchi zaidi ya 100 duniani wanahudhuria mkutano huo wa 26 wa kujadili mabadiliko ya tabianchi, ulioanza tarehe 31 Oktoba na kuendelea hadi tarehe 12 ya mwezi huu wa Novemba mjini Glasgow, Uskochi.