Kuuliwa kunatokana na kihere here chako kwa mambo yasiokuhusu! Majanga haya yanawapata wote ambao wana shida ya kuwa viherehere kama mbelgiji wenu wa M4C


Sawa endeleeni kuua.

Niliwahi andika kuwa kabla Lisu hajalamba mchanga na kuingia katika Lango la kuzimu atashuhudia Wale wote waliomshambulia wakiingia kuzimu wao na familia zao

Endelea kutazama hii Filamu.

Alafu utajua Mshindi atakuwa Nani Duniani na kaburini.
 
Robert kama Robert ,achana na hao oooh sijui mama hivi sijui mama vile hivi wangepewa mama zao nchi in a week tu wangeweza kweli
Mpeni mama yangu nchi muone kama kuna ujinga utaendelea! Labda mumuee kama mlivyomfanya mzee kipara
 
Kwani Zakaria alikuwa assasinated pia mkuu, hebu tuache utani kwanza did they kill this man? If yes imeniumiza sana yani dah😟


Nafikiri huelewi thamani ya Roho ndio maana unaona mtu auawe tuu kiholela.

Muombe Mungu msamaha vinginevyo katika maisha yako utakuja kuonyeshwa thamani ya Roho ya mtu uelewe Kwa njia ngumu
 
Nafikiri huelewi thamani ya Roho ndio maana unaona mtu auawe tuu kiholela.

Muombe Mungu msamaha vinginevyo katika maisha yako utakuja kuonyeshwa thamani ya Roho ya mtu uelewe Kwa njia ngumu
Roho ni kitu priceless ila pia waliodhuriwa wengi walikuwa na shida wachache ndio walionewa hao waliotaka kuporwa fedha kupitia kufanywa mateka!
 
Roho ni kitu priceless ila pia waliodhuriwa wengi walikuwa na shida wachache ndio walionewa hao waliotaka kuporwa fedha kupitia kufanywa mateka!


Upo utaratibu wa kimahakama mtu akikosea.

Sio Kwa upumbavu wako kisa unakacheo gani serikalini unateka watu utakavyo kana kwamba wewe ni MUNGU.
Hiyo hufanyika Kwa watu wasiostarabika, wahuni, waovu na hakika watajibiwa vivyo hivyo.

Kila mtu mi wathamani hapa duniani, taratibu zifuatwe.

Kumuua au kumdhuru mtu kisa unachokiita kiherehere hicho hicho ndio kitaiingiza laana kwenye kizazi chako.

Kama unaona Roho ni Priceless nafikiri sina cha kujadili na wewe katika hilo
 
Wakuu Kwema!!!

Tutozane.
Tukamuane,
Tuzinguane,
Tuchapane,
Tuchanane,
Lakini tusiuane.

Kwa kweli Mimi Taikon naona ni mara elfu Tozo kuliko Kutekana, kuuana, kupotezana Kwa kisingizio cha Uzalendo, sijui maendeleo, sijui vitu gani.

Nchi sasa inaenda Sawa Sawa, mambo yamenyooka.
Mapungufu kidogo hayakosekani lakini sio Yale ya kutisha, kutishana na kumalizana..

Hakika ni Bora tuwe kwenye nchi Masikini isiyomwaga Damu za watu wake kuliko kuwa na Nchi yenye maendeleo isiyojali maisha ya watu.

Sisi wote ni ndugu ndani ya taifa hili. Hata Kama upo utofauti wa kichama, Kidini, kikabila n.k lakini tunaunganishwa na udongo WA taifa letu.

Kuchikizana kupo, kukwazana kupo, kutofautiana kupo, hayo yote isiwe sehemu ya kumalizana kupotezana.

Kwa kweli, kamwe siwezi jivunia nchi inayoshindwa kuthamini maisha ya watu wake, na hapa namaanisha Uhai.

Niliwahi sema, fanya ufanyalo usiinajisi nchi Kwa kumwaga damu za watu wako mwenyewe Kwa kisingizio chochote kile. Ni laana, na Kama Mungu aishivyo itakutafuna.

Ni Bora Tozo,
Ni Bora umasikini,
Ni Bora malumbano ya hoja yenye lengo la kujenga,
Kuliko chuki zinazopelekea watu kuuana.

Ndugu Watanzania, nasisitiza, usiinajisi Nchi Kwa kumwaga damu isiyo na hatia.

Taikon Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
We jamaa umeniwahi ku upload huu uzi. Ingekua kule story of changes ningekupa kura yangu.
Kusema ukweli maisha ya kutekana tekana sio kabisa..
 
Wakuu Kwema!!!

Tutozane.
Tukamuane,
Tuzinguane,
Tuchapane,
Tuchanane,
Lakini tusiuane.

Kwa kweli Mimi Taikon naona ni mara elfu Tozo kuliko Kutekana, kuuana, kupotezana Kwa kisingizio cha Uzalendo, sijui maendeleo, sijui vitu gani.

Nchi sasa inaenda Sawa Sawa, mambo yamenyooka.
Mapungufu kidogo hayakosekani lakini sio Yale ya kutisha, kutishana na kumalizana..

Hakika ni Bora tuwe kwenye nchi Masikini isiyomwaga Damu za watu wake kuliko kuwa na Nchi yenye maendeleo isiyojali maisha ya watu.

Sisi wote ni ndugu ndani ya taifa hili. Hata Kama upo utofauti wa kichama, Kidini, kikabila n.k lakini tunaunganishwa na udongo WA taifa letu.

Kuchikizana kupo, kukwazana kupo, kutofautiana kupo, hayo yote isiwe sehemu ya kumalizana kupotezana.

Kwa kweli, kamwe siwezi jivunia nchi inayoshindwa kuthamini maisha ya watu wake, na hapa namaanisha Uhai.

Niliwahi sema, fanya ufanyalo usiinajisi nchi Kwa kumwaga damu za watu wako mwenyewe Kwa kisingizio chochote kile. Ni laana, na Kama Mungu aishivyo itakutafuna.

Ni Bora Tozo,
Ni Bora umasikini,
Ni Bora malumbano ya hoja yenye lengo la kujenga,
Kuliko chuki zinazopelekea watu kuuana.

Ndugu Watanzania, nasisitiza, usiinajisi Nchi Kwa kumwaga damu isiyo na hatia.

Taikon Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Iliwachukua mwaka mmoja na miezi sita kuanza kuteka watu na kupoteza.

Hawa wanamiezi sita tu tayari tumeshaanza kufunguliana makesi ya ugaidi tuupe nafasi muda utujulishe yajayo.
 
Iliwachukua mwaka mmoja na miezi sita kuanza kuteka watu na kupoteza.

Hawa wanamiezi sita tu tayari tumeshaanza kufunguliana makesi ya ugaidi tuupe nafasi muda utujulishe yajayo.

Ndio maana nikasema ni Bora Tozo kuliko Kutekana
 
Wasiojulikana wao watapukutika kwa karma uzuri ilianza na boss wao ndizi imeiva tokea nchani.
 
Back
Top Bottom