MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,011
- 16,748
Kama Mwamamichezo Halisi ( japo sijifichi ni mwana Simba SC ) nianze kwa Kuwapongeza Kaizer Chiefs FC kwa Ushindi wa Goli Nne na niwape pia Pole Simba SC kwa Kufungwa Mchezo huu wa Kwanza leo.
Zifuatazo ni sababu zangu Binafsi za Kiuchambuzi Mimi Krav Maga kwanini Simba SC tumefungwa na Kaizer Chiefs FC ambazo hata hivyo sikulazimishi uziamini japo unatakiwa uziheshimu kama ambavyo nami naheshimu ( nitaheshimu ) zako.
1. KUBWETEKA KWA WACHEZAJI
Huitaji Akili Kubwa ama kuona au kugundua kuwa Mafanikio ya hivi karibuni ya Simba SC yamewapa Kiburi cha Kipuuzi Wachezaji wa Simba SC kiasi cha kuanza Kubweteka wakijiona ni akina FC Barcelona.
2. MIPIRA YA KROSI NI TATIZO SUGU KWA MABEKI WA SIMBA SC
Nilidhani baada ya mwaka Juzi Kufungwa Goli Tano Tano na AS Vita na Al Ahly kwa Mipira ya Krosi Simba SC ingejifunza na Kulifanyia Kazi Ila leo Makosa haya haya ya Kutokujua Kukaba Krosi yamesababisha Beki Shomari Kapombe asababishe Kufungwa Goli 3 huku Beki Mohammed Hussein Zimbwe nae akisababisha Goli 1 ( tena la Nne ) kwa Kumzawadia Pasi ya Upendo Adui na akafumua bonge la Shuti ( Muwa )
3. UZEE KWA MABEKI WA KATI WA SIMBA SC NA KUCHOKA KWAO UPESI
Ifike mahala sasa Simba SC ijifunze ama kutokupenda Kusajili au Kung'ang'ania Wachezaji Wakongwe ( Wazee ) huku wale Vijana na wenye Uwezo kama Beki Kijana ninayemkubali sana Ame Ibrahim na David Kameta Duchu tukiacha Kuwatumia. Leo akina Wawa na Onyango wamefanya Makosa makubwa mno na laiti yangetumiwa vyema na Washambuliaji wa Kaizer Chiefs FC huenda leo tungefungwa hata Magoli 7 au 8 pale Bondeni kwa Madiba.
4. KOCHA WA SIMBA SC KUKARIRI KIKOSI NA KUKOSA PLAN B YA HARAKA
Nikiri tu kuwa Kocha Mkuu wa Simba SC Didier Gomez kweli ni Tactician ila nae sasa ajifunze Kucheza Mechi zake Kimkakati na Kimazingira zaidi kuliko Kujiamini sana na kuingia Kichwa Kichwa tu.
5. VYOMBO VYA HABARI KUPENDA KUIPA SIFA SIMBA SC ZISIZOSTAHILI
Nilitegemea kuona Vyombo vingi vya Habari nchini Tanzania ( hasa vya Michezo ) vingekuwa vinaiambia Ukweli Simba SC kuhusu Klabu ya Kaizer Chiefs Matokeo yake Kutwa tu Magazeti na Watangazaji wa Vipindi vya Michezo Kazi yao ni Kuisifia tu Kinafiki Simba SC kwa kutokujua kuwa Wanawaharibu Wachezaji kupelekea kutokuwa na Ufanisi.
6. UBOVU WA LIGI YA TANZANIA. KUDEKEZWA SANA NA TFF HUKU MWILI KUTOKUWA TAYARI KIMCHEZO
Binafsi niliwashangaa mno Wapenzi na Mashabiki wa Simba SC walipokuwa wakiibeza Klabu ya Kaizer Chiefs kwakuwa iko nafasi ya Kenda ( Tisa ) katika Ligi Kuu yao.
Watu wa Simba SC walisahau kuwa Kaizer Chiefs FC wapo katika Moja ya Ligi Kuu bora barani Afrika ambayo ni Professional League wakati yetu hapa ya VPL ni Semi - Amateur kwa sasa.
Pia sasa imefika wakati TFF kuambiwa ukweli juu ya kupenda Kuidekeza Simba SC na Kuisikiliza kwa kila walitakalo wakati kumbe hapo wanakuwa hawaijengi Klabu bali wanazidi tu Kuibomoa.
Sikuona sababu ya Simba SC kukaa karibia Siku 9 au 11 kutokucheza Mechi yoyote ile ya Kimashindano ( hasa Ligi Kuu ) kwa Kisingizio kuwa wana Mechi za Champions League na hawataki Wachezaji wao ( wetu ) Kuumizwa.
Cha Kushangaza Kaizer Chiefs FC ndani ya Siku hizo hizo ambazo Simba SC ilidekezwa na TFF kwa Kusikilizwa na kutokucheza Mechi yoyote ile ya Ligi Kuu ya VPL wao Kaizer Chiefs wameweza Kucheza Mechi zao Mbili za Ligi Kuu yao Kubwa ya PSL.
Kwangu Mimi Krav Maga naamini mojawapo ya sababu Kubwa ya Simba SC yangu kupokea Kipigo Kitakatifu ni Wachezaji kutokuwa na Match Fitness tofauti na Wenzao ( Kaizer Chiefs FC ) ambao kuendelea Kwao kucheza Mechi zao za Ligi Kuu zimewasaidia Kuwaimarisha Kimwili, Kiufundi na Kimchezo.
Simba SC wangeacha Kudekadeka na TFF nayo kukubali Kuidekeza ingecheza Michezo yake Miwili ya Ligi Kuu VPL dhidi ya Watani zao Yanga SC na Coastal Union FC ingekuwa Faida Kwao ya kukijua Kikosi na kukifanyia marekebisho ili isifungwe Kifedheha na Kaizer Chiefs FC kama ilivyotokea leo ( jana ) pale Soccer City ( FNB Stadium )
7. SIMBA SC HAINA KIKOSI CHA MICHUANO YA NUSU FAINALI YA CL BALI INA CHA KUCHEZA VPL, ASFC NA CHA KUISHIA TU ROBO FAINALI YA CL
Ili ujue ( mjue ) kuwa Simba SC ina Wachezaji tu wa Kuifikisha hapo Robo Fainali CL na siyo Nusu Fainali CL angalieni jinsi Wachezaji mahiri wa Simba SC ambao Kutwa huwa tunawaimba walivyokuwa outshined kwa kila Kitu na Wachezaji wa Kaizer Chiefs FC ambao wanaonyesha kuwa wameandaliwa vyema na katika Misingi hasa ya Soka.
Sasa ni wakati wa Simba SC kupitia Mwekezaji wake Mo Dewji kufikiria Kusajili Wachezaji wa Viwango vikubwa vya Kucheza hatua ya Nusu Fainali ya CL na siyo hawa tulionao ambao uwezo wao ni wa kutufikisha tu kila mara katika hatua za Robo Fainali CL.
Kuna Wachezaji wa Kigeni mahiri mno Walisajiliwa kwa Mbwembwe zote na Simba SC kuja Kuongeza Nguvu kama akina Junior Lukosa na Peter Maduhwa ila sijajua wamepotelea wapi, wameitia Hasara Kiasi gani Simba SC yetu na kwanini Kutoweka Kwao wana Simba SC hatukuambiwa pia.
Hata hivyo nihitimishe tu kwa kusema kuwa japokuwa Simba SC leo ( jana ) imefungwa Goli Nne kwa Bila ila ikijipanga vyema na kuwa na Mikakati ya Ushindi ya ndani na nje ya Uwanja Krav Maga nina uhakika Jumamosi ijayo Kaizer Chiefs FC anafungwa hata Goli Sita kwa Sifuri Uwanja wa Machinjio wa Benjamin Mkapa Temeke Mkoani Dar es Salaam.
Kutokana na Hali ya Hewa ya Baridi Kali la Afrika Kusini nawashauri Simba SC hii Mechi yao ya marudiano ichezwe Saa 9 Alasiri ili iwe Changamoto Kwao Kimchezo na Faida Kwetu.
Kikubwa tu tuvumilieni Kuchekwa na Watani zetu wakubwa Yanga SC kwani ndiyo mpira na Utani huo ila nasi sasa tujitahidi kuyafanyia Kazi mapungufu yetu yote ya Kimchezo kusudi Mchezo wa marejeano Simba SC tupindue Matokeo kwa Ushindi kisha nasi tuendelee Kuwaacha Kimafanikio huku wakiendelea tu kupoteza Alama ( points ) kama kwa Namungo FC leo ( jana ) na watukabidhi mapema Ubingwa wetu wa Nne mfululizo wa VPL.
Tumefungwa, lakini tusikate tamaa pia.
Zifuatazo ni sababu zangu Binafsi za Kiuchambuzi Mimi Krav Maga kwanini Simba SC tumefungwa na Kaizer Chiefs FC ambazo hata hivyo sikulazimishi uziamini japo unatakiwa uziheshimu kama ambavyo nami naheshimu ( nitaheshimu ) zako.
1. KUBWETEKA KWA WACHEZAJI
Huitaji Akili Kubwa ama kuona au kugundua kuwa Mafanikio ya hivi karibuni ya Simba SC yamewapa Kiburi cha Kipuuzi Wachezaji wa Simba SC kiasi cha kuanza Kubweteka wakijiona ni akina FC Barcelona.
2. MIPIRA YA KROSI NI TATIZO SUGU KWA MABEKI WA SIMBA SC
Nilidhani baada ya mwaka Juzi Kufungwa Goli Tano Tano na AS Vita na Al Ahly kwa Mipira ya Krosi Simba SC ingejifunza na Kulifanyia Kazi Ila leo Makosa haya haya ya Kutokujua Kukaba Krosi yamesababisha Beki Shomari Kapombe asababishe Kufungwa Goli 3 huku Beki Mohammed Hussein Zimbwe nae akisababisha Goli 1 ( tena la Nne ) kwa Kumzawadia Pasi ya Upendo Adui na akafumua bonge la Shuti ( Muwa )
3. UZEE KWA MABEKI WA KATI WA SIMBA SC NA KUCHOKA KWAO UPESI
Ifike mahala sasa Simba SC ijifunze ama kutokupenda Kusajili au Kung'ang'ania Wachezaji Wakongwe ( Wazee ) huku wale Vijana na wenye Uwezo kama Beki Kijana ninayemkubali sana Ame Ibrahim na David Kameta Duchu tukiacha Kuwatumia. Leo akina Wawa na Onyango wamefanya Makosa makubwa mno na laiti yangetumiwa vyema na Washambuliaji wa Kaizer Chiefs FC huenda leo tungefungwa hata Magoli 7 au 8 pale Bondeni kwa Madiba.
4. KOCHA WA SIMBA SC KUKARIRI KIKOSI NA KUKOSA PLAN B YA HARAKA
Nikiri tu kuwa Kocha Mkuu wa Simba SC Didier Gomez kweli ni Tactician ila nae sasa ajifunze Kucheza Mechi zake Kimkakati na Kimazingira zaidi kuliko Kujiamini sana na kuingia Kichwa Kichwa tu.
5. VYOMBO VYA HABARI KUPENDA KUIPA SIFA SIMBA SC ZISIZOSTAHILI
Nilitegemea kuona Vyombo vingi vya Habari nchini Tanzania ( hasa vya Michezo ) vingekuwa vinaiambia Ukweli Simba SC kuhusu Klabu ya Kaizer Chiefs Matokeo yake Kutwa tu Magazeti na Watangazaji wa Vipindi vya Michezo Kazi yao ni Kuisifia tu Kinafiki Simba SC kwa kutokujua kuwa Wanawaharibu Wachezaji kupelekea kutokuwa na Ufanisi.
6. UBOVU WA LIGI YA TANZANIA. KUDEKEZWA SANA NA TFF HUKU MWILI KUTOKUWA TAYARI KIMCHEZO
Binafsi niliwashangaa mno Wapenzi na Mashabiki wa Simba SC walipokuwa wakiibeza Klabu ya Kaizer Chiefs kwakuwa iko nafasi ya Kenda ( Tisa ) katika Ligi Kuu yao.
Watu wa Simba SC walisahau kuwa Kaizer Chiefs FC wapo katika Moja ya Ligi Kuu bora barani Afrika ambayo ni Professional League wakati yetu hapa ya VPL ni Semi - Amateur kwa sasa.
Pia sasa imefika wakati TFF kuambiwa ukweli juu ya kupenda Kuidekeza Simba SC na Kuisikiliza kwa kila walitakalo wakati kumbe hapo wanakuwa hawaijengi Klabu bali wanazidi tu Kuibomoa.
Sikuona sababu ya Simba SC kukaa karibia Siku 9 au 11 kutokucheza Mechi yoyote ile ya Kimashindano ( hasa Ligi Kuu ) kwa Kisingizio kuwa wana Mechi za Champions League na hawataki Wachezaji wao ( wetu ) Kuumizwa.
Cha Kushangaza Kaizer Chiefs FC ndani ya Siku hizo hizo ambazo Simba SC ilidekezwa na TFF kwa Kusikilizwa na kutokucheza Mechi yoyote ile ya Ligi Kuu ya VPL wao Kaizer Chiefs wameweza Kucheza Mechi zao Mbili za Ligi Kuu yao Kubwa ya PSL.
Kwangu Mimi Krav Maga naamini mojawapo ya sababu Kubwa ya Simba SC yangu kupokea Kipigo Kitakatifu ni Wachezaji kutokuwa na Match Fitness tofauti na Wenzao ( Kaizer Chiefs FC ) ambao kuendelea Kwao kucheza Mechi zao za Ligi Kuu zimewasaidia Kuwaimarisha Kimwili, Kiufundi na Kimchezo.
Simba SC wangeacha Kudekadeka na TFF nayo kukubali Kuidekeza ingecheza Michezo yake Miwili ya Ligi Kuu VPL dhidi ya Watani zao Yanga SC na Coastal Union FC ingekuwa Faida Kwao ya kukijua Kikosi na kukifanyia marekebisho ili isifungwe Kifedheha na Kaizer Chiefs FC kama ilivyotokea leo ( jana ) pale Soccer City ( FNB Stadium )
7. SIMBA SC HAINA KIKOSI CHA MICHUANO YA NUSU FAINALI YA CL BALI INA CHA KUCHEZA VPL, ASFC NA CHA KUISHIA TU ROBO FAINALI YA CL
Ili ujue ( mjue ) kuwa Simba SC ina Wachezaji tu wa Kuifikisha hapo Robo Fainali CL na siyo Nusu Fainali CL angalieni jinsi Wachezaji mahiri wa Simba SC ambao Kutwa huwa tunawaimba walivyokuwa outshined kwa kila Kitu na Wachezaji wa Kaizer Chiefs FC ambao wanaonyesha kuwa wameandaliwa vyema na katika Misingi hasa ya Soka.
Sasa ni wakati wa Simba SC kupitia Mwekezaji wake Mo Dewji kufikiria Kusajili Wachezaji wa Viwango vikubwa vya Kucheza hatua ya Nusu Fainali ya CL na siyo hawa tulionao ambao uwezo wao ni wa kutufikisha tu kila mara katika hatua za Robo Fainali CL.
Kuna Wachezaji wa Kigeni mahiri mno Walisajiliwa kwa Mbwembwe zote na Simba SC kuja Kuongeza Nguvu kama akina Junior Lukosa na Peter Maduhwa ila sijajua wamepotelea wapi, wameitia Hasara Kiasi gani Simba SC yetu na kwanini Kutoweka Kwao wana Simba SC hatukuambiwa pia.
Hata hivyo nihitimishe tu kwa kusema kuwa japokuwa Simba SC leo ( jana ) imefungwa Goli Nne kwa Bila ila ikijipanga vyema na kuwa na Mikakati ya Ushindi ya ndani na nje ya Uwanja Krav Maga nina uhakika Jumamosi ijayo Kaizer Chiefs FC anafungwa hata Goli Sita kwa Sifuri Uwanja wa Machinjio wa Benjamin Mkapa Temeke Mkoani Dar es Salaam.
Kutokana na Hali ya Hewa ya Baridi Kali la Afrika Kusini nawashauri Simba SC hii Mechi yao ya marudiano ichezwe Saa 9 Alasiri ili iwe Changamoto Kwao Kimchezo na Faida Kwetu.
Kikubwa tu tuvumilieni Kuchekwa na Watani zetu wakubwa Yanga SC kwani ndiyo mpira na Utani huo ila nasi sasa tujitahidi kuyafanyia Kazi mapungufu yetu yote ya Kimchezo kusudi Mchezo wa marejeano Simba SC tupindue Matokeo kwa Ushindi kisha nasi tuendelee Kuwaacha Kimafanikio huku wakiendelea tu kupoteza Alama ( points ) kama kwa Namungo FC leo ( jana ) na watukabidhi mapema Ubingwa wetu wa Nne mfululizo wa VPL.
Tumefungwa, lakini tusikate tamaa pia.