Stream line
JF-Expert Member
- Apr 22, 2015
- 393
- 239
Usiku wa kuamkia tarehe 19.5.2015 tumeshuhudia/kusikia mabomu yakirushwa katikati ya makazi ya wanetu wasomi wa UDSM. Sababu kuu ni kuwa watoto wetu hawa wamefikia hatua ya mwisho ya uvumilivu wa kuishi kwa mikate - chai, kwani muda wao wa kupokea 'Boom' umepitiliza kwa siku 21.
Swali ni 1. je, ni sawa kwa watoto hawa kupelekewa mbwa na kupigwa mabomu ya machozi au ni kupewa kile ambacho wameaminishwa kuwa watapewa na ktk mda muafaka ili kuwawezesha kuendelea na masomo yao?
2. Kwa nini aliyewapa ratiba ya boom asitoe maelezo mbele yao siku nyingi kabla ya wao kutopata boom kwa mda uliokubalika?
3. Kwa nini wahusika wasiwajibishwe? Bali watoto hawa ndo wanapelekwa polisi kwa kosa la kudai pesa ya chakula?
Nina mengi ya kusema, mfano: sasa watoto wetu wa kike wamegeuzwa asusa na wenye tamaa mbaya. Wakiacha wake zao na kushambulia watoto hao. Hilo wazazi wenzangu mlitambue.
MAONI YANGU: Kama zamani watoto walisoma bila mikopo, hata sasa pesa hiyo inayowatesa yaweza pelekwa vyuoni kama ilivyokuwa zamani na ikawa mwisho wa kutupigia/kutufukuzia shule wanetu ambao tumewatumikia toka wachanga hadi ktk hatua ya mwisho wanapofukuzwa shule kwa kuwa wanalilia chakula.
Mbaya zaidi ni vitisho walivyowekewa, kuwa hawana haki ya kudai boom na kwa kufanya hivyo wanajifukuza shule. Sheria hiyo itazamwe upya. Pia tujifunze yaliyotokea Hong Kong. Kwa mda mrefu vijana waligoma lakini hatukuona mabomu.
Swali ni 1. je, ni sawa kwa watoto hawa kupelekewa mbwa na kupigwa mabomu ya machozi au ni kupewa kile ambacho wameaminishwa kuwa watapewa na ktk mda muafaka ili kuwawezesha kuendelea na masomo yao?
2. Kwa nini aliyewapa ratiba ya boom asitoe maelezo mbele yao siku nyingi kabla ya wao kutopata boom kwa mda uliokubalika?
3. Kwa nini wahusika wasiwajibishwe? Bali watoto hawa ndo wanapelekwa polisi kwa kosa la kudai pesa ya chakula?
Nina mengi ya kusema, mfano: sasa watoto wetu wa kike wamegeuzwa asusa na wenye tamaa mbaya. Wakiacha wake zao na kushambulia watoto hao. Hilo wazazi wenzangu mlitambue.
MAONI YANGU: Kama zamani watoto walisoma bila mikopo, hata sasa pesa hiyo inayowatesa yaweza pelekwa vyuoni kama ilivyokuwa zamani na ikawa mwisho wa kutupigia/kutufukuzia shule wanetu ambao tumewatumikia toka wachanga hadi ktk hatua ya mwisho wanapofukuzwa shule kwa kuwa wanalilia chakula.
Mbaya zaidi ni vitisho walivyowekewa, kuwa hawana haki ya kudai boom na kwa kufanya hivyo wanajifukuza shule. Sheria hiyo itazamwe upya. Pia tujifunze yaliyotokea Hong Kong. Kwa mda mrefu vijana waligoma lakini hatukuona mabomu.