Book reading: Unasoma au Umesoma kitabu gani ungependa wengine wakisome?

wiki hii nimesoma kitabu maarufu sana kwa sasa, kiitwacho NDOA YANGU, NINGEJUA. Nimekipenda sana kwa sababu kinaeleza kwa kinagaubaga kwa nini ndoa nyingi hazina amani. Kwa kweli kimenigusa kwa sababu kuna sehemu mtunzi ameeleza historia ya ndoa yangu utadhani ananijua, na hasa zaidi maswali aliyouliza: 1. KAMA UNGEJUA MKEO AMA MUMEO ATAKUWA NA TABIA ALIYO NAYO SASA, JE UNGEKUBALI KUOANA? swali hili ni zuri kwa sababu kwangu mimi nisingekubali, na hata mke wangu alipojibu swali hili, nae akasema asingekubali. Ukweli kitabu hiki ni kiboko, na ingawa nimekiazima, kwa kweli sitamrudishia mwenyewe, nataka nikisome zaidi na zaidi nitambue makosa yangu na huenda kikanisaidia pia katika kuwashauri wenzangu.
Kitabu cha pili nilichosoma kinaitwa MY DEAR BOTTLE, ukianza kukisoma andaa mbavu zako, maana kinaonyesha jinsi ambavyo pombe kumfanya mtu akapoteza utu wake na thamani kwa wengine

Watu kama nyie ndo mliotufundisha uchoyo wa vitabu. Unakuta mtu anapitia wakati mgumu au anahangaika na jambo fulani na unaona una kitabu unachofikiri kitamsaidia unaamua kumpa asome kisha akurudishie. Ukija kuhesabu vitabu ulivyorushwa na thamani yake unakoma kiherehere. Siku hizi simpi mtu kitabu hata nisukumwe vipi moyoni. Namwelekeza jinsi ya kukipata au namnunulia chake kama zawadi ili kupunguzia moyo takataka.

Kama wewe kimekusaidia na unatamani kukisoma tena na tena ili uweze kuwashauri na wengine kwa nini upange kutokukirudisha badala ya kupanga kukirudisha na kununua cha kwako? Huoni kama ni dhuluma na kukosa shukrani? Aliyekupa unadhani hataki kukisoma tena na tena kama wewe au unadhani hana ndugu na marafiki anaotamani wapone kama wewe? Tunapowaazima vitabu si kwamba tunakuwa hatuvihitaji tena ila tunakuwa tumeamua kutanguliza mahitaji yenu mbele na kuweka ya kwetu nyuma. Samahani bwana. Ni kwamba comment yako imeamsha kumbukumbu ya vitabu vyangu nilivyodhulumiwa. Mrudishie mhusika kitabu chake na umuombe radhi kwa kukichelewesha. Vinginevyo unamkatisha tamaa asiweze kuhudumia wengine kama alivyokuhudumia wewe. Dhuluma ni dhuluma hata kama si fedha.
 
Kwa mwaka huu nimesoma:
1. Battlefield of the mind: Winning the battle in your mind by Joyce Meyer. Hiki ni cha mrengo wa kikristo
2. Eat that frog by Brian Tracy
3. Raising worldlywise but innocent kids by David Wyrtzen
4. Nimerudia The big picture cha Ben Carson
5. It worked for me in life and leadership - biography ya Colin Powel. Sijakimaliza.

Pia ni mpenzi wa jarida (magazine) la Parents: caring for you and your family la Kenya la kila mwezi.
 
Screenshot_20170709-151409.png
M
how the west was lost-dambisa moyo
 
Habari zenu wadau napenda kuitambulisha kwenu Klabu ya Whatsapp kwa ajili ya
Usomaji wa vitabu mbalimbali na kwa pamoja
kupeana mbinu mbalimbali za usomaji wa vitabu
kubadilishana uzoefu wa usomaji
Kubadilishana mawazo kuhusu vitabu vizuri

Kama unapenda kujiunga na Klabu yetu wasiliana na Admins wa Group kwa Whatsapp
0625809610 au
0692487394
 
Hiki cha Maisha na Mafanikio sio cha Munga. Collections ya kazi za Munga zimetengenezewa kitabu kinaitwa ''Jitambue''. Nilkinunuaga Kariakoo kwenye meza ya wauza vitabu. Ntakuangalizia kama kuna Contacts mle then ntakutumia kiongozi. Ntaku-pm my number kwa mawasilaino zaidi.
Pius Hugo high I high high in jug lithium hui Hui this buoy you buy hui took out I guilty KTU Hugh thug high I hit hut juju I by youth you I it I of Kikuyu you Yuki yoko yuyyiohhjjjvz
Hiki cha Maisha na Mafanikio sio cha Munga. Collections ya kazi za Munga zimetengenezewa kitabu kinaitwa ''Jitambue''. Nilkinunuaga Kariakoo kwenye meza ya wauza vitabu. Ntakuangalizia kama kuna Contacts mle then ntakutumia kiongozi. Ntaku-pm my number kwa mawasilaino zaidi.

Kwa muda nimekuwa natamani kuwa na club kwa ajili ya watu kupata nafasi kusoma vitabu mbali mbali na taarifa mbal mbali ili kupanua uwezo na uelewa wa mambo mbali mbali katika maisha yetu. Club hii ningependa tuwekee zaid vitabu vya soft copy ili kufanya watu wengi waweze kupata nafasi ya kusoma vitabu hivyo ,pia tutatumia club hii kuweza kupeana ushauri na mbinu nzuri za usomaji wa vitabu , kuandika vitabu na pia kuuliza na kuelekezwa majina mbali mbali ya vitabu na hata wapi vinauzwa au kupatikana ( soft copy na hardcopy)

Malengo ya club hii hapa jf
1. Kupeana hamasa na kujenga/kuboresha tabia ya watu kupenda kusoma vitabu na taarifa mbali mbali
2.kuweza kupata nafasi ya vitabu mbali mbali , majina ya vitabu hivyo , na majarida mbali mbali
3. Kujenga na kupanua wigo kwa watu wengi kuweza kujifunza mambo mengi ili kupeana ujuzi kupitia vitabu
4.kupeana changamoto za kutafuta msomaji mzuri wa vitabu ( hapa vigezo vitajadiliwa na wa club ili kupata msomaji mzuri)
5. Kutakuwa na zawadi kwa msomaji mzuri wa vitabu(pia vigezo na zawadi vitajadiliwa na wana club)

Karibuni sana kwenye ulimwengu mpya wa kusoma vitabu kutokea hapa hapa JF


Binafsi ntaleta vitabu soft copy chache hapa na wengine wataendelea kuongeza vingine


Sent from my HUAWEI LUA-U22 using JamiiForums mobile app
 
Hiki cha Maisha na Mafanikio sio cha Munga. Collections ya kazi za Munga zimetengenezewa kitabu kinaitwa ''Jitambue''. Nilkinunuaga Kariakoo kwenye meza ya wauza vitabu. Ntakuangalizia kama kuna Contacts mle then ntakutumia kiongozi. Ntaku-pm my number kwa mawasilaino zaidi.
Pius Hugo high I high high in jug lithium hui Hui this buoy you buy hui took out I guilty KTU Hugh thug high I hit hut juju I by youth you I it I of Kikuyu you Yuki yoko yuyyiohhjjjvz
Hiki cha Maisha na Mafanikio sio cha Munga. Collections ya kazi za Munga zimetengenezewa kitabu kinaitwa ''Jitambue''. Nilkinunuaga Kariakoo kwenye meza ya wauza vitabu. Ntakuangalizia kama kuna Contacts mle then ntakutumia kiongozi. Ntaku-pm my number kwa mawasilaino zaidi.

Kwa muda nimekuwa natamani kuwa na club kwa ajili ya watu kupata nafasi kusoma vitabu mbali mbali na taarifa mbal mbali ili kupanua uwezo na uelewa wa mambo mbali mbali katika maisha yetu. Club hii ningependa tuwekee zaid vitabu vya soft copy ili kufanya watu wengi waweze kupata nafasi ya kusoma vitabu hivyo ,pia tutatumia club hii kuweza kupeana ushauri na mbinu nzuri za usomaji wa vitabu , kuandika vitabu na pia kuuliza na kuelekezwa majina mbali mbali ya vitabu na hata wapi vinauzwa au kupatikana ( soft copy na hardcopy)

Malengo ya club hii hapa jf
1. Kupeana hamasa na kujenga/kuboresha tabia ya watu kupenda kusoma vitabu na taarifa mbali mbali
2.kuweza kupata nafasi ya vitabu mbali mbali , majina ya vitabu hivyo , na majarida mbali mbali
3. Kujenga na kupanua wigo kwa watu wengi kuweza kujifunza mambo mengi ili kupeana ujuzi kupitia vitabu
4.kupeana changamoto za kutafuta msomaji mzuri wa vitabu ( hapa vigezo vitajadiliwa na wa club ili kupata msomaji mzuri)
5. Kutakuwa na zawadi kwa msomaji mzuri wa vitabu(pia vigezo na zawadi vitajadiliwa na wana club)

Karibuni sana kwenye ulimwengu mpya wa kusoma vitabu kutokea hapa hapa JF


Binafsi ntaleta vitabu soft copy chache hapa na wengine wataendelea kuongeza vingine


Sent from my HUAWEI LUA-U22 using JamiiForums mobile app
 
Wale wenzangu na mie tunaokaa na kazi siku nenda siku rudi haiishi, tunaosubiri kazi zipungue ndo tufanye vitu fulani, tunaotaka Mungu aongeze siku iwe na saa 33 - wale wa ".... nitafanya kesho, nitafanya baadae, hii ngumu sana nitafanya nikimaliza hiki au kile, hii inachusha labda nibadilishe mazingira ndo nifanye, hii natupilia mbali kama ni kazi na nifukuzwe...." tusome "Eat That frog: 21 Great ways to stop procrastinating and get more done in less time" by Brian Tracy.


Thanks Nandera, huyu ni mimi typical!
Ntakitafuta hiki.. sounds interesting.
 
Thanks Nandera, huyu ni mimi typical!
Ntakitafuta hiki.. sounds interesting.

Hahahaaa..... unajikuta hujui uanzeje, uanze na nini uishie na nini mwisho unazira unaamua kujishindia JF. Kitafute mpendwa; hakika hutakuwa yule wa mwanzo.
 
Hahahaaa..... unajikuta hujui uanzeje, uanze na nini uishie na nini mwisho unazira unaamua kujishindia JF. Kitafute mpendwa; hakika hutakuwa yule wa mwanzo.

Acha tu, ukiona list niliyo nayo sasa?
Mpaka wakati mwingine natamani kuchukua vacation kwa ajili ya kusoma tu ili nimalizane na malengo ya mwaka.
Thanks dear nitakitafuta.
 
"Men are from mars women are from venus" by John Gray. hiki kitabu kinahusu mambo ya mahusiano kinakupa guidance za kuielewa jinsia ya pili uwapo kwenye mahusiano, ni kizuri sana
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom