Bongoland II Itaonyeshwa Minneapolis

PastorPetro

Senior Member
Feb 25, 2008
189
35
ghhhhhh.jpg


Naona huyo jamaa Kibira yuko tayari kumwaga filamu nyingine:Nimepata hii kwenye barua pepe.

Moja kwa moja kutoka mjini Dar-Es-Salaam, tunafurahi kutangaza siku ya uzinduzi maalumu wa sinema ya Bongoland II. Tarehe ya uzinduzi ni mwezi April 5, 2008 hapa mjini Minnepolis, Minnesota katika ukumbi wa sinema wa Oakstreet Cinema.

Sinema hii ilitengenezwa mwaka jana July pale mjini Dar. Vitongoji maarufu vya mji huo kama Manzese na Magomeni vilitumika katika utengenezaji wa sinema hii. Kusema kweli, hii itakuwa ni hadhi kubwa ya wasanii wa ki-Tanzania maana sinema hii itaonyeshwa katika tamasha mbali mbali za sinema za kimataifa.

Sinema hii ni inamhusu Juma Pondamali ambaye baada ya maisha na malengo yake kutofanikiwa nchini Marekani, aliamua kurudi nyumbani. Lakini visakato alivyovikuta nyumbani vilimshangaza sana na hakuna kitu chochote hapa ulimwenguni ambacho kingemtayarisha kupambana na visakato hivyo. TRELA MPYA
Jitayarishe kuwaona wacheza sinema wakongwe wa Tanzania kama Mzee Kipara, Bi Chuma Selemani Mzee na Bi Thecla Mjatta. Vile vile pia kuwaona wachezaji chipukizi kutoka mjini Dar-es-salaam.

Msanii mhusika mkuu ni Peter Omari ambaye anacheza kama Juma. Peter, ambaye kwa sasa anishi Mwanza, aliwahi kucheza katika sinema yetu iliyopita iliyoitwa TUSAMEHE.
 
Duh We Umetokea Wapi?lete Habari Za Mafisadi Wanaohujumu Uchumi Ili Tuangushe Vibuyu,we Unaleta Habari Za Bongoland 2,ebu Cheki Hiyo Trela Inavyoonesha Uchafu Wa Huko Manzese,sasa Si Aibu Hiyo Kama Itaoneshwa Mpaka Nchi Za Nje.kuna Watu Wanakula Pesa Zetu Ambazo Zingetumika Ktk Kuondoa Huo Uchafu Unaonekana Katika Hiyo Trela,usilete Issue Kama Hizi Hapa Jf.au Mnasemaje Wana Jf?
 
Kaboka, hiyo sinema ya Bongoland II inaonyesha Manzese sawa. Watu si wanakaa huko kwa nini isionyeshwe?

Kuhusu ufisadi unataka niongeze nini? Kuna mafisadi wa kutoka enzi za Mwalimu lakini hawaguswi. Nyang'anyi na Pontoon yake unakumbuka.
 
enhe mambo si hayo ebu weka full picha kuhusu huyu fisadi wa kale,yaan nyan'ganyi maana mie nilikuwa sina hizo habari
 
Kiboka vipi mkuu?

Unaogopa kwenu mkuu?Mbona comment yako imenichanganya sana..yaani eti manzese kuna uchafu..hapo ni wapi tanzania au somalia?Si kwenu jamani please give me a break mkuu yaaani umenipotezea network kabisa....

Nafikiri umepata point yangu..manzese ndio tanzania na ni kwetu mie na wewe na most of Jambo forum member.

Siku njema
Buswelu
 
Kwenye website yao inasema kuwa imepigwa Manzese, Magomeni, na Oyster Bay.
 
Back
Top Bottom