Yo Yo
JF-Expert Member
- May 31, 2008
- 11,217
- 1,702
Khaa!! soma mwenyewe from Chemi Che-Mponda's blog
Jumamosi ya juma lililopita tarehe 22 majira ya jioni,
Nilipata nafasi ya kutembelea duka la nguo lijilikanalo Mr.Price hapo mlimani city,
Katika kujichagulia nikapenda na top moja nyeupe,mi nikaenda kuijaribisha ile top,pamoja na nguo zingine nilizozipenda,wakati naangia na ile nguo,yule dada amabye yuko mlangoni kwenye chumba cha kubadilisha akaniambia angalia nguo yangu nyeupe usije ukaichafua
Ah mi nikamwambia kwa mfano ikitokea ikachafuka itakuwaje akasema ah aha mi nakuambia tu,basi mie nikajaribu kwa umakini sana tena sana lakini haikunitosha so ikawa sio chaguo langu tena,ile nguo ilivyotoka nje baada ya dakika 10 wakati najaribu nguo nyingine na kunitosha ndo nikawa naelekea kaunta kulipa zile zilizonitosha
yule dada akaniitia walinzi wao kuwa nimechafua shati lao jeupe kwa wanja(make up ya machoni),na sheria yao ni kwamba mtu akichafua nguo lazima alipe.basi wakaning'an'gania nilipe ile top ya thamani ya Tsh22,000/=
Kwa kweli nilighadhilika na kuwaambia kuwa mimi sitaweza kulipa maana sikuona kuwa nimechafua na kama nimeichafua ni bahati mbaya na wala hamkuniambia kuwa kuna malipo iwapo mteja akitokea kudamage nguo,basi nikawaambia hapa kwenye kapu nina nguo ya thamani ya 150,000 na hii top moja mnayotaka kuninunulisha ni 22,000 tu sasa nilipie hizi zilizonisha nah ii niache au niziache hizi za laki na nusu,wakasema utajua mwenyewe,na hapo uku mie mteja napewa lugha za kashfa na dharau mtindo mmoja kutoka kwa hawa wafanyakazi wa humo MR PRICE.
Basi mie nikaawaambia mie narejesha hizi za laki na nusu na kulipia moja ya 22,000/= wakasema kwa jeuri sawa.sasa sijui hapa nani kaumia ni mimi ambaye iyo Top nilimpa mdogo wangu hapo hapo maana ilikuwa inamtosha au wao kuleta sifa mbaya na kutokuwa na customer care na kupoteza laki na nusu na kuku bali 22,000 pia kupoteza wateja?
Maana sikatai kuwa kuna watu wananunua hadi laki5 but mteja ni mteja tu hata kama akiwa mweusi mwenzio na wewe uko unafanya kazi kwenye duka la mzungu sasa unajiona na wewe mzungu,na kudharau wabongo wenzio.
Hii ni tahadhari kwa WaTanzania wenzangu watembeleapo maduka ya MR Price pale mlimani city dar es salaam,unaweza ukapata kiherehere cha kujaribu nguo labda kwa lengo la kuja kuifata kesho then ukawa hauna pesa,utajikuta umegadishwa kwa muda mrefu na kupoteza muda wako kwa wabaguzi na wasiojua biashara ya nguo kama hawa.
Ni hayo tuu.
MDAU