Bomu linalomwandama Magufuli

si ndio watoto wa dadaake sijui hebu wekeni fresh nauyo kebbys ndo nani yupo wapi?
Kebby's ni hotel ipo Mwenge karibu na kituo cha Bamaga, ni hotel ya hawala yake Magufuli anayeitwa Kabula dada (Kb) au Kebby. Inasemekana ni nguvu za mzee.
 
Huyu Magufuli sina hakika kama atafikisha kura milioni tatu
Kama mke wake tu hamkubari na ninahisi mke wa makufuri lazima kura atampa lowassa na ukienda huko kwao ndio hawamuelewi kabisa je hizo kura milion 3 atazipata wapi?
 
Ingekuwa vizuri habari hii ikachipishwa front page kuwakumbusha watanzania maana walishasahau. Kama iliandikwa na Salva Rweyemamu mwandishi wa habari wa rais kwa sasa, basi ni credible. Ichapishwe tena. Nawasilisha

Naunga mkonyo hoja. Kura zikitosha ichapishwe haraka sn ili watz wasiendelee kupotoshwa
 
Ndio maana magufuli hana confidence kabisa kwa sababu ya matatizo makuu manne
1. Mke wake kumsusa
2. Ufisadi aliofanya kwenye uuzaji wa nyumba
,3. Kushindwa kesi ya Samaki wa magufuli na kuliingizia taifa hasara kubwa
4. Kumpa kimada wake nyumba ya serikali
 
Kwani Sundi yupo wapi?Kabula nae ni nani?

Sundi ndiye yule kimada aliyezaa naye mtoto Jerry ambaye alimuhonga nyumba ya Serikali enzi hizo za kuuza nyumba za Serikali....

Kabula wa Keby's ni kimada wake wa sasa aliyemjengea Keby's hotel pale maeneo ya Mwenge.

Kwa hali hiyo kweli wife haimuumi!?

Jangwani yenyewe alisahau kumtambulisha mkewe halali Janeth, mpaka dakika za mwisho alipokumbushwa na JK.
Kwa udhalilishwaji huo , huyo mama ajipumzikie tu.
 
Sundi ndiye yule kimada aliyezaa naye mtoto Jerry ambaye alimuhonga nyumba ya Serikali enzi hizo za kuuza nyumba za Serikali....

Kabula wa Keby's ni kimada wake wa sasa aliyemjengea Keby's hotel pale maeneo ya Mwenge.

Kwa hali hiyo kweli wife haimuumi!?

Jangwani yenyewe alisahau kumtambulisha mkewe halali Janeth, mpaka dakika za mwisho alipokumbushwa na JK.
Kwa udhalilishwaji huo , huyo mama ajipumzikie tu.
Ivi yule bwana mkubwa kama amepita mote humo atakuwa amekosa kakichwani kweli na inaoneka yule mzee anapenda sana chini hadi hadi anahonga nyumba serikali.
 
Ivi yule bwana mkubwa kama amepita mote humo atakuwa amekosa kakichwani kweli na inaoneka yule mzee anapenda sana chini hadi hadi anahonga nyumba serikali.

Kweli ccm ni ileile na wanaccm ni walewale. mkapa alimhonga mramba wizara ya fedha. Mwenzake kikwete alikuwa anahonga wilaya na mikoa sasa km akiwa waziri alikuwa anahonga nyumba za serikali je akiwa rais atahonga nn?
Tafakari chukua hatua weka ccm mbalo na watz.
 
Kweli ccm ni ileile na wanaccm ni walewale. Mwenzake kikwete alikuwa anahonga wilaya na mikoa sasa km akiwa waziri alikuwa anahonga nyumba za serikali je akiwa rais atahonga nn?
Tafakari chukua hatua weka ccm mbalo na watz.
Ataanza kuhonga nyumba za ikulu ndogo za wilaya.
 
Habari hii ilichapishwa kwenye gazeti la RAI miaka michache iliyopita ikisomeka...

Huyu Ndiye Pombe Magufuli:

- Wasema nyumba 8,000 kauza kwa mkono wake mwenyewe
- Apuuza maonyo ya wataalamu- Mafaili ya Sundi na Musa aliyabeba kwapani

ALIYEKUWA Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, katika Serikali ya awamu ya tatu, aliteka madaraka na kuwa mwenyekiti wa zoezi la kuuza nyumba za serikali ambazo hadi sasa, zimeshauzwa 8,288 imefahamika.

Habari zilizopatikana ndani ya wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), zimethibitishia Rai wiki hii kwamba Magufuli alihakikisha anashiriki kama Mwenyekiti katika zoezi zima la kuuza nyumba, ambalo kimsingi lilistahili kusimamiwa na Mtendaji Mkuu wa TBA.

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya ‘fujo’ katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.

Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.

Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.

“Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi,” vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.

Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.

“Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili,” chanzo hicho cha habari kinaeleza.

Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.

Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.

Chini ya sheria hiyo, Waziri anaruhusiwa kuteua wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.

Hadi Machi mwaka huu, wajumbe hao walikuwa ni J. Kijazi, E. Lipambila, E. Lugwisha, Msangi, E. Mwakalinga, D. Kisasi, P. Ncheye, F. Werema na A. Bukuku.

Hata hivyo, sheria haitoi nafasi yoyote kwa Waziri kusimamia shughuli za uuzwaji au upangaji wa nyumba za serikali.

Mtendaji Mkuu wa TBA Togolayi Makumba Kimweri, alipoulizwa kupitia kwa Katibu Muhtasi wake, alimwambia mwandishi wa Rai aandike maswali kisha asubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya ofisi.

Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa muda wa saa moja, mwandishi alipokwenda kuuliza akaambiwa kwamba Kimweri tayari alikwishaondoka ofisini kupitia mlango wa nyuma na asingeweza kurudi ofisini.

Lakini baadhi ya wafanyakazi wa TBA wameiambia Rai kwamba kinachoandikwa kwenye magazeti kuhusu ushiriki wa Magufuli kuuza nyumba za Serikali ni kidogo mno kuliko hali halisi.

Kama ilivyokuwa kwa mdogo wake Musa, waziri Magufuli alishinikiza mtoto wa dada yake anayeitwa James Doto Mgosha auziwe nyumba za serikali kwa kumtengenezea ajira ya muda mfupi katika TANROADS.

Tofauti na Musa, Doto ameuziwa nyumba hiyo kwa jina la mtu mwingine lakini anaishi katika nyumba hiyo, namba 64 iliyopo Kinondoni Flats.

Habari kutoka TBA zinaonyesha jina la mtu mwingine (tunalihifadhi) kuwa ndiye aliyeuziwa nyumba hiyo mtu huyo alipata kupitia utaratibu wa Magufuli kupeleka jina lake kwenye wakala wa majengo na kulazimisha apewe nyumba.

Alipoulizwa kwa njia ya simu, Doto alisema suala la ajira na nyumba waulizwe waliomwajiri na kumpa nyumba. Akakata simu.

Mfanyakazi mwingine alieleza Rai kwamba msichana mwingine (jina tunalihifadhi) akiwa na miezi minne tu kazini alipelekwa na Magufuli katika Wakala wa Majengo akilazimisha auziwe nyumba hata kabla ya kuthibitishwa kazini. Nyumba hiyo iko Block A, Ocean Road.

Hata hivyo, habari hizo zinaeleza kwamba msichana huyo ambaye hadi sasa anaishi na wazazi wake, ameipangisha nyumba hiyo kwa mfanyakazi mmoja wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na analipwa kwa dola za kimarekani.

“Kuuza nyumba za serikali sawa, lakini kweli katika mtindo huu? Sisi tunaoshiriki kuzikagua na kuziratibu tukiomba hatupati, lakini wengine wanaingia serikalini miezi miwili wanapata nyumba. Na wengine hata si wafanyakazi, wanapata, hii si sahihi, alilalamika mfanyakazi mmoja aliyeandikia Rai kwa njia ya barua pepe.

Hadi Machi mwaka huu Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) walishauza nyumba 8,288 ambazo hata hivyo zilitakiwa kuuzwa kwa watumishi wa serikali.

Katika mauzo hayo, Serikali ilitarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00. Hata hivyo hadi sasa Serikali imepata shilingi 22,684,108,115.08.

Kwa sasa, Serikali imebakiwa na nyumba 1,098 zinazosimamiwa na TBA. Kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa Serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.

SALVA RWEYEMAMU
RAI

Nani kaandika, mbona jina ni la Boss wa Kurugenzi kuu ya Habari State house au jina limefanana!?
 
Ndio maana magufuli hana confidence kabisa kwa sababu ya matatizo makuu manne
1. Mke wake kumsusa
2. Ufisadi aliofanya kwenye uuzaji wa nyumba
,3. Kushindwa kesi ya Samaki wa magufuli na kuliingizia taifa hasara kubwa
4. Kumpa kimada wake nyumba ya serikali

Hiyo ya nne umma haua uthibitisho ila hizo tatu za kwanza zinajulikana na Watanzania walio wengi!
 
Nani kaandika, mbona jina ni la Boss wa Kurugenzi kuu ya Habari State house au jina limefanana!?
Aliandika enzi hizo kabla ya kulambishwa asali ya ukurugenzi nafikiri leo akiiona makala hii anaweza kuikana.
 
Uzi upo tangu jana lakini wale jamaa zetu wa it wanachungulua tu wasepa hakuna anaye tetea mhhh imewakuna njooni kina
jinga lao
moto chin
liz
ritz
vip mpo kwenye sabato au leo kanisani tutawasubiri kesho
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom