Bomba la mafuta lasababisha maafa Nigeria

under_age

JF-Expert Member
Apr 17, 2007
317
115
Ripoti kutoka Nigeria zinaarifu kuwa watu ishirini na wanane wamefariki baada ya bomba la mafuta kulipuka katika mji mkuu wa kibiashara wa Lagos.

Mlipuko huo ulitokea wakati watu wakichota mafuta baada ya bomba hilo kupasuka.

Vipande vya miili ya binadamu vilitapakaa kote kote baada ya mlipuko huo kutokea na waokoaji wamefika kusaidia waathiriwa na kuzima moto.

Mlipuko kama huo ulitokea mjini Lagos wakati kama huu mwaka jana na kuua zaidi ya watu mia mbili.
source:BBC
http://www.bbc.co.uk/swahili/news/story/2004/06/000000_leoafrica.shtml
 
Inasikitisha!

Mbona huwa matukio haya sasa yamekuwa ya kila siku?
ni kweli mzalendo, hususan katika maeneo yetu ya afrika. nadhani ni ile tabia yetu ya kutokujali na kutokujirekebisha kutokana na makosa yaliotokea.inasikitisha sana ila labda tutafika. matukio kama haya yakitokea bara ulaya yanapata uchunguzi na utafiti wa hali ya juu na kama kuna anaehusika basi huwa anawajibishwa lakini afrika bado tunahitaji muda kufika huko.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom