Barca
JF-Expert Member
- May 3, 2013
- 1,404
- 1,548
Habari ya muda hii. Bomba la gesi limepasuka maeneo ya somanga taharuki imetanda maeneo haya. Vyombo vya ulinzi na usalama kama kawaida hawatoi elimu kwa wananchi wapo tu wamezagaa hovyo. Tanzania hatujifunzi kabisa kuepuka majanga. Magari yote yanayotoka Dar es Salaam na kwenda Dar es Salaam hayapiti.
Inasemekana right moto ungeweka ungeweza unguza wilaya yote y kilwa. Nimeshangaa sana kwa kweli.
=====
UPDATES:
“TANESCO linawataarifu wateja wake kuwa saa 11:20 jioni leo imetokea hitilafu kwenye "valve" na kusababisha kuvuja kwa gesi kwenye kituo cha Somanga Rufiji Mkoani Pwani, hitilafu imetokea wakati Songas wakiendelea na matengenezo kinga kwenye bomba la gesi la Songosongo”- TANESCO.
Taarifa zaidi....
Mamia ya Wasafiri wamekwama kwa saa zaidi ya 3 karibu na eneo la kati ya Songas na Banduka, Wilaya ya Kilwa Lindi baada ya bomba la gesi kwenye mitambo ya umeme kudaiwa kupasuka, Polisi wamezuia magari na vyombo vingine vya moto kupita eneo hilo ili kuepusha madhara.
Gesi hiyo inavuja kwenye kituo hicho kinachomilikiwa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) hivyo kuwashawishi walinzi wa kituo jirani cha kupokea gesi kutoka Madimba Mtwara na Songosongo kilicho chini ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kusaidia kuimarisha ulinzi.
“Ni kweli kuna hitilafu kidogo. Wataalamu wetu wanashughulikia hali hiyo ila hakuna moto wala madhara yoyote kwa binadamu,” amesema Nigel Whittaker mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Songas.
Inasemekana right moto ungeweka ungeweza unguza wilaya yote y kilwa. Nimeshangaa sana kwa kweli.
=====
UPDATES:
“TANESCO linawataarifu wateja wake kuwa saa 11:20 jioni leo imetokea hitilafu kwenye "valve" na kusababisha kuvuja kwa gesi kwenye kituo cha Somanga Rufiji Mkoani Pwani, hitilafu imetokea wakati Songas wakiendelea na matengenezo kinga kwenye bomba la gesi la Songosongo”- TANESCO.
Taarifa zaidi....
Mamia ya Wasafiri wamekwama kwa saa zaidi ya 3 karibu na eneo la kati ya Songas na Banduka, Wilaya ya Kilwa Lindi baada ya bomba la gesi kwenye mitambo ya umeme kudaiwa kupasuka, Polisi wamezuia magari na vyombo vingine vya moto kupita eneo hilo ili kuepusha madhara.
Gesi hiyo inavuja kwenye kituo hicho kinachomilikiwa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) hivyo kuwashawishi walinzi wa kituo jirani cha kupokea gesi kutoka Madimba Mtwara na Songosongo kilicho chini ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kusaidia kuimarisha ulinzi.
“Ni kweli kuna hitilafu kidogo. Wataalamu wetu wanashughulikia hali hiyo ila hakuna moto wala madhara yoyote kwa binadamu,” amesema Nigel Whittaker mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Songas.