Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Bomani ataka mjadala wa Katiba usiwe wa pupa
Imeandikwa na Grace Chilongola, Magu; Tarehe: 10th January 2011 @ 23:50 Imesomwa na watu: 221; Jumla ya maoni: 0
JAJI mstaafu Mark Bomani ametaka mabadiliko ya katiba yafanyike kwa amani na utulivu na kuepuka pupa ambayo inaweza kulitumbukiza Taifa katika vurugu.
Alisema kwa kuwa katiba sio Biblia wala Msaafu kwa kuwa inaweza kubadilishwa, lakini akataka mabadiliko hayo yaepuke vurugu.
Alisema hayo mwishoni mwa wiki katika kijiji cha Mwamanyili wilayani Magu, mkoani Mwanza katika hafla ya kupongezwa kwa familia yake kwa kufanikisha ujenzi wa Kanisa la Wasabato (SDA).
Bomani alitumia nafasi hiyo kuwatahadharisha wanasiasa na Watanzania kwa ujumla, kudai mabadiliko hayo kwa njia ya amani na utulivu, ili kuepusha nchi na machafuko yanayoweza kujitokeza.
Alisema jamii inahitaji katiba mpya lakini madai hayo yasitumiwe kisiasa na kuielekeza nchi katika janga la machafuko na kuwataka wanaodai mabadiliko hayo, kuketi na serikali kujadiliana, ili wafikie makubaliano ya nini kifanyike.
Jaji Bomani alisema njia pekee ya kuepukana na machafuko, ni kukutana mezani na kuzungumza ili muafaka upatikane na kuondoa uwezekano wa kuzuka kwa vurugu.
Katiba mpya inapaswa kupatikana, lakini tuzingatie umoja wetu na tuulinde katika kipindi hiki cha kudai mabadiliko hayo, alisema Bomani.
Kuhusu uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete wa kuunda Tume alisema ni njia ya kufikia mabadiliko ya Katiba na kuongeza kuwa hata mjadala wa bungeni pia ni njia sahihi na kwamba hali hiyo inaonyesha mitazamo tofauti yenye lengo moja.
Alifafanua kwamba njia ya kuunda Tume inaweza kuwa bora zaidi kutokana na ukweli kuwa ndiyo njia pekee inayowashirikisha wananchi wote kwa makundi na vipindi tofauti.
Imeandikwa na Grace Chilongola, Magu; Tarehe: 10th January 2011 @ 23:50 Imesomwa na watu: 221; Jumla ya maoni: 0
JAJI mstaafu Mark Bomani ametaka mabadiliko ya katiba yafanyike kwa amani na utulivu na kuepuka pupa ambayo inaweza kulitumbukiza Taifa katika vurugu.
Alisema kwa kuwa katiba sio Biblia wala Msaafu kwa kuwa inaweza kubadilishwa, lakini akataka mabadiliko hayo yaepuke vurugu.
Alisema hayo mwishoni mwa wiki katika kijiji cha Mwamanyili wilayani Magu, mkoani Mwanza katika hafla ya kupongezwa kwa familia yake kwa kufanikisha ujenzi wa Kanisa la Wasabato (SDA).
Bomani alitumia nafasi hiyo kuwatahadharisha wanasiasa na Watanzania kwa ujumla, kudai mabadiliko hayo kwa njia ya amani na utulivu, ili kuepusha nchi na machafuko yanayoweza kujitokeza.
Alisema jamii inahitaji katiba mpya lakini madai hayo yasitumiwe kisiasa na kuielekeza nchi katika janga la machafuko na kuwataka wanaodai mabadiliko hayo, kuketi na serikali kujadiliana, ili wafikie makubaliano ya nini kifanyike.
Jaji Bomani alisema njia pekee ya kuepukana na machafuko, ni kukutana mezani na kuzungumza ili muafaka upatikane na kuondoa uwezekano wa kuzuka kwa vurugu.
Katiba mpya inapaswa kupatikana, lakini tuzingatie umoja wetu na tuulinde katika kipindi hiki cha kudai mabadiliko hayo, alisema Bomani.
Kuhusu uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete wa kuunda Tume alisema ni njia ya kufikia mabadiliko ya Katiba na kuongeza kuwa hata mjadala wa bungeni pia ni njia sahihi na kwamba hali hiyo inaonyesha mitazamo tofauti yenye lengo moja.
Alifafanua kwamba njia ya kuunda Tume inaweza kuwa bora zaidi kutokana na ukweli kuwa ndiyo njia pekee inayowashirikisha wananchi wote kwa makundi na vipindi tofauti.