Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
MIMI si Muislamu lakini sasa naanza kuamini katika imani hii. Baada ya Tundu Lissu kushambuliwa na watu wasiojulikana Wazee wa Kiislamu Pemba, Unguja, Tanga, Bwagamoyo na Dar es salaam walisoma kinachoitwa "al-badir". Ninaambiwa ikisomwa hii basi aliyetenda jambo la unyama kwa siri wanapatwa na madhara. Wanaweweseka, wanaweza kuongea wenyewe kama vichaa, na wengine wanaweza hata kujiua au kuumbuka. Kwa mbali na karibu naona dalili za matokeo ya "al-badir".
Imenichukua muda kuamini macho yangu na masikio yangu. Nimetafakari na kujiuliza hatimaye nimejiundia majibu kuwa Tundu Lissu amehukumiwa kifo na watu wasiojulikana kwa gharama na namna yoyote. Ninaumia mno! Nashindwa kuamini kama hii ni Tanzania au Rwanda!
Kitendo cha Mawakili wa Serikali kupeleka ombi mahakamani Kisutu ili afutiwe dhamani ili aandikiwe Hati ya Kukamatwa popote alipo chini ya jua ni jaribio la kifo lililoshindwa kama risasi 16. Inaumiza mno. Lissu ameikosea nini nchi hii kiasi cha kumtakia kaburi? Kwa nini tumefikia hatua mbaya namna hii? Imefikia hatua dunia iitazame Tanzania kwa jicho lisilo la kawaida.
Lissu amepigwa risasi 16 mwilini. Mwili wa Lissu aijuaye ni mkewe lakini mwenyewe anasema "umechanwachanwa". Mifupa imevurugwa. Lissu ana maumivu makali. Lissu amesahau hata tendo la ndoa maana nyonga haifai. Lissu amepona kichwa tu. Yuko kitandani Ubelgiji. Mnaitana, mnakaa chini, anakuwepo mwenyekiti, hoja inatolewa, "sasa tunamfanyaji Lissu". Hatimaye mnaafikiana kuwa afutiwe dhamana ili tumkamate mgonjwa huyu, badala ya kulala wodini akalale Segerea kusiko hata na panadoli ya kutuliza maumivu. Hii ni nini kama siyo kutaka Lissu afe?
Ninatamani kuwaona kwa macho mawakili hawa kwa macho yangu. Niwaulize ni dini gani? Wana familia? Wamewahi kuumwa au kuuguza? Ni binadamu kama sisi? Wana nyama na damu kama sisi? Nani aliwatuma kufanya jaribio ovu hili? Walilipwa shilingi ngapi kwa jaribio hili?
Hakimu Simba Mungu akubariki. Mungu akuzungushie fensi ya Moto. Umeongozwa na Mungu kutupilia mbali jaribio hilo la shetani uliposema "HUO SI UBINADAMU". Najua umewaudhi mno waliopanga jaribio hilo. Umejiweka hatarini. Mungu akutetee! Thawabu yako ni kubwa mno!
Inawezekana baada ya jaribio hili kushindwa kikao kitakaa tena kutafuta Lissu afanywe nini? Maana Hakimu Simba amenawa kama Herode kwa Yesu. Lakini bado kuna sauti za asulubiwe?
Natoa wito kila mtu kwa imani yake tumuombee Lissu. Mungu awatie upofu wote wanaopanga "kummaliza". Mungu mtetee maana anakusudi naye!
Tumeshindwa kumdhibiti Lissu kwa hoja sasa tunataka afe gerezani. Mungu shuka! Kama hiyo ndiyo Tanzania mpya, basi siitaki. Mturudishie Tanzania yetu iliyokuwa imejaa watu wenye huruma, upole, upendo, udugu, umoja, amani na raha!
#AchaWoga 2020
Imenichukua muda kuamini macho yangu na masikio yangu. Nimetafakari na kujiuliza hatimaye nimejiundia majibu kuwa Tundu Lissu amehukumiwa kifo na watu wasiojulikana kwa gharama na namna yoyote. Ninaumia mno! Nashindwa kuamini kama hii ni Tanzania au Rwanda!
Kitendo cha Mawakili wa Serikali kupeleka ombi mahakamani Kisutu ili afutiwe dhamani ili aandikiwe Hati ya Kukamatwa popote alipo chini ya jua ni jaribio la kifo lililoshindwa kama risasi 16. Inaumiza mno. Lissu ameikosea nini nchi hii kiasi cha kumtakia kaburi? Kwa nini tumefikia hatua mbaya namna hii? Imefikia hatua dunia iitazame Tanzania kwa jicho lisilo la kawaida.
Lissu amepigwa risasi 16 mwilini. Mwili wa Lissu aijuaye ni mkewe lakini mwenyewe anasema "umechanwachanwa". Mifupa imevurugwa. Lissu ana maumivu makali. Lissu amesahau hata tendo la ndoa maana nyonga haifai. Lissu amepona kichwa tu. Yuko kitandani Ubelgiji. Mnaitana, mnakaa chini, anakuwepo mwenyekiti, hoja inatolewa, "sasa tunamfanyaji Lissu". Hatimaye mnaafikiana kuwa afutiwe dhamana ili tumkamate mgonjwa huyu, badala ya kulala wodini akalale Segerea kusiko hata na panadoli ya kutuliza maumivu. Hii ni nini kama siyo kutaka Lissu afe?
Ninatamani kuwaona kwa macho mawakili hawa kwa macho yangu. Niwaulize ni dini gani? Wana familia? Wamewahi kuumwa au kuuguza? Ni binadamu kama sisi? Wana nyama na damu kama sisi? Nani aliwatuma kufanya jaribio ovu hili? Walilipwa shilingi ngapi kwa jaribio hili?
Hakimu Simba Mungu akubariki. Mungu akuzungushie fensi ya Moto. Umeongozwa na Mungu kutupilia mbali jaribio hilo la shetani uliposema "HUO SI UBINADAMU". Najua umewaudhi mno waliopanga jaribio hilo. Umejiweka hatarini. Mungu akutetee! Thawabu yako ni kubwa mno!
Inawezekana baada ya jaribio hili kushindwa kikao kitakaa tena kutafuta Lissu afanywe nini? Maana Hakimu Simba amenawa kama Herode kwa Yesu. Lakini bado kuna sauti za asulubiwe?
Natoa wito kila mtu kwa imani yake tumuombee Lissu. Mungu awatie upofu wote wanaopanga "kummaliza". Mungu mtetee maana anakusudi naye!
Tumeshindwa kumdhibiti Lissu kwa hoja sasa tunataka afe gerezani. Mungu shuka! Kama hiyo ndiyo Tanzania mpya, basi siitaki. Mturudishie Tanzania yetu iliyokuwa imejaa watu wenye huruma, upole, upendo, udugu, umoja, amani na raha!
#AchaWoga 2020