Bodi Ya Utalii (TTB) ya Tanzania ifumuliwe haraka na inayoingia iwekewe malengo

chotera

JF-Expert Member
May 19, 2016
6,305
15,033
Wakuu salaamu.
Kama ilivyo ada hii bodi yenye jukumu la kutangaza vivutio vinavyopatikana nchini kwetu ili pato la taifa liongezeke imeshindwa kazi kwani ni muda mrefu wakenya waliutangaza mlima Kilimanjaro kama wao na iliandikwa hivyo toka zamani lakini jamaa walikaa kimya kama hawapo na watanzania hata hapa jf wamelalamika sana, Bodi hii haina tija tena ukitembelea hata website zao wako kizamani Leo hii hawana update ya taarifa zao utakuta taarifa za miaka ya nyuma, Bodi imelala na taasisi za kitalii zimelala kifo cha mwafrika kusini juu ya mlima Kilimanjaro uliopo Tanzania kimeonesha uvivu wa hii Bodi mfu, ombi langu hawa wasibakizwe kwani kosa la Olduvai gorge tuluwaacha sasa hili wanatakiwa kuwajibishwa iingie Bodi iliyokisasa zaidi ambayo itakua na Tija zaidi kwa taifa letu.
 
Back
Top Bottom