Bodi ya utalii mnastahili pongezi kwa hili

dittu

Member
Dec 2, 2016
75
53
Kuna siku nilikuwa nasafiri kutoka Dar kuelekea Dodoma tulipofika maeneo ya benzi akasimama jamaa mmoja, alivyosimaa mimi nikajua ni wale wale wa kuuza sabuni na vipidozi.

Alipoanza kuongea ndipo nikagundua jambo tofauti, alikuwa anazungumza kuhusu kutembelea vivutio vya utalii alizungumza mengi sana akiwahamasisha watu watembelee mbuga za Mikumi, Seluo na Udzugwa sababu kwa watu wanaokaa Moro na Dodoma ni rahisi kwako kuzifikia.

Baada ya kuzungumza akatoa nafasi ya maswali yanayohusiana na utalii tu, abiria tukaanza kuuliza na kujibiwa pia watu wakatoa changamoto jamaa akawa anazinoti na kusema kuwa atazifikisha sehemu husika na mwisho kabisa akagawa vipeperushi vyenye taarifa za utalii.

Mara nyingi tumekuwa tukiwalaumu sana bodi ya utalii kuwa hawatangazi, kwa hiki mnachokifanya tunawapongeza maana mtu akifanya vibaya tumkosoe, akifanya vizuri tumpongeze.

Endeleeni kuwa wabunifu maana isije kuwa nguvu ya soda baada ya muda muache.
 
mkuu kwa tanzania bado sana, hata wakienda kutangaza nje mkuu, mie naenda nao sana hawa jamaa, wakifika huko ni watu wa matanuzi tu, leo hii waulize kama wana japo cd tu za kuelezea tanzania watakwambia hawana, kuna vivutio vingi tu kwa kweli, huwa nawatizama naona aibu tupu, niliwahi kwenda ile ya africa kusini indaba, nikaenda desk la lesotho, jamaa wanajielezea vizuri sana kwenye booth yao, inafikia kipindi kampuni za tz zinajiandikisha na kampuni nyingine kama ATA nk. utalii wa ndani wangefanya kama kenya, kenya utalii wa ndani uko juu sana, sasa ni kupandishiana makodi kiasi kwamba mtu yupo arusha anashindwa kwenda porini kuona wanyama japo wikiend, aibu sana mkuu
 
mkuu kwa tanzania bado sana, hata wakienda kutangaza nje mkuu, mie naenda nao sana hawa jamaa, wakifika huko ni watu wa matanuzi tu, leo hii waulize kama wana japo cd tu za kuelezea tanzania watakwambia hawana, kuna vivutio vingi tu kwa kweli, huwa nawatizama naona aibu tupu, niliwahi kwenda ile ya africa kusini indaba, nikaenda desk la lesotho, jamaa wanajielezea vizuri sana kwenye booth yao, inafikia kipindi kampuni za tz zinajiandikisha na kampuni nyingine kama ATA nk. utalii wa ndani wangefanya kama kenya, kenya utalii wa ndani uko juu sana, sasa ni kupandishiana makodi kiasi kwamba mtu yupo arusha anashindwa kwenda porini kuona wanyama japo wikiend, aibu sana mkuu
Ndugu nimewapongeza kwa walivyoanzisha kutangaza kwenye mabasi,unasema gharama za mtanzania zipo juu siyo kweli kaka mtz kuingia mbugani ni hela ya juu ni sh 10000 tu na mbuga nyingine ni sh 5000, mtz kulala hostel za tanapa ni sh 5000 hadi 10000 ghalama ziko wapi wakifanya vizuri wapongezwe,wakihalibu waambiwe pia.
 
mkuu kwa tanzania bado sana, hata wakienda kutangaza nje mkuu, mie naenda nao sana hawa jamaa, wakifika huko ni watu wa matanuzi tu, leo hii waulize kama wana japo cd tu za kuelezea tanzania watakwambia hawana, kuna vivutio vingi tu kwa kweli, huwa nawatizama naona aibu tupu, niliwahi kwenda ile ya africa kusini indaba, nikaenda desk la lesotho, jamaa wanajielezea vizuri sana kwenye booth yao, inafikia kipindi kampuni za tz zinajiandikisha na kampuni nyingine kama ATA nk. utalii wa ndani wangefanya kama kenya, kenya utalii wa ndani uko juu sana, sasa ni kupandishiana makodi kiasi kwamba mtu yupo arusha anashindwa kwenda porini kuona wanyama japo wikiend, aibu sana mkuu
Wamegawa frash za kuhamasisha utalii mabasi yote pale ubungo tukiwa kwenye magari huwa tunaona ikiwekwa mambo mengine ni changamoto ndogo kama hivo wanavyozitatuwa
 
Wamegawa frash za kuhamasisha utalii mabasi yote pale ubungo tukiwa kwenye magari huwa tunaona ikiwekwa mambo mengine ni changamoto ndogo kama hivo wanavyozitatuwa
Ndio wanastuka sasa hivi, mie mkuu nimebarikiwa kwenda show karibia zote hizi nje, lakini bado sana, na hii kuhamasisha wazawa wasipofanya ubahili watanzania tutaamka na kuanza kutembelea, mbuga za wanyama watoto wetu wanazisoma tu shuleni na kuziimba lakini uwezo wa kwenda hakuna, wenzetu wa kenya hili lipo siku nyingi, sasa hapa kila kitu ilikuwa dola, ilikuwa inakera sana, wacha tuone kigwangala akija na mbinu hizo utalii wa ndani utaibuka na tutajua vivutio vingi sana kuhusu tanzania yetu,
 
Ndio wanastuka sasa hivi, mie mkuu nimebarikiwa kwenda show karibia zote hizi nje, lakini bado sana, na hii kuhamasisha wazawa wasipofanya ubahili watanzania tutaamka na kuanza kutembelea, mbuga za wanyama watoto wetu wanazisoma tu shuleni na kuziimba lakini uwezo wa kwenda hakuna, wenzetu wa kenya hili lipo siku nyingi, sasa hapa kila kitu ilikuwa dola, ilikuwa inakera sana, wacha tuone kigwangala akija na mbinu hizo utalii wa ndani utaibuka na tutajua vivutio vingi sana kuhusu tanzania yetu,
Unajuwa watz wengi wanajuwa kutalii mbugani ghalama kubwa lakini siyo kweli kabisa kiingilio cha juu 10000 na chini sh 5000 tu sasa huu uelewa wakijitahidi kuufanya kila mtu akafahamu watu wataenda sana tu.
 
Kuna siku nilikuwa nasafiri kutoka Dar kuelekea Dodoma tulipofika maeneo ya benzi akasimama jamaa mmoja, alivyosimaa mimi nikajua ni wale wale wa kuuza sabuni na vipidozi.

Alipoanza kuongea ndipo nikagundua jambo tofauti, alikuwa anazungumza kuhusu kutembelea vivutio vya utalii alizungumza mengi sana akiwahamasisha watu watembelee mbuga za Mikumi, Seluo na Udzugwa sababu kwa watu wanaokaa Moro na Dodoma ni rahisi kwako kuzifikia.

Baada ya kuzungumza akatoa nafasi ya maswali yanayohusiana na utalii tu, abiria tukaanza kuuliza na kujibiwa pia watu wakatoa changamoto jamaa akawa anazinoti na kusema kuwa atazifikisha sehemu husika na mwisho kabisa akagawa vipeperushi vyenye taarifa za utalii.

Mara nyingi tumekuwa tukiwalaumu sana bodi ya utalii kuwa hawatangazi, kwa hiki mnachokifanya tunawapongeza maana mtu akifanya vibaya tumkosoe, akifanya vizuri tumpongeze.

Endeleeni kuwa wabunifu maana isije kuwa nguvu ya soda baada ya muda muache.
ungewashauri watumie video za kwenye mabasi badala Ya mabasi hayo kuburudisha abiria kwa video zisizo na faida kwa abiria na na taifa
 
TTB wapuuzi wanaacha kuwapa kazi vijana waliosoma utalii wamejazana huku kitaa ,wafanye hiyo kazi ya marketing wao wamekalia majungu na kukaa tu ofisini
 
TTB wapuuzi wanaacha kuwapa kazi vijana waliosoma utalii wamejazana huku kitaa ,wafanye hiyo kazi ya marketing wao wamekalia majungu na kukaa tu ofisini
Kivipi si ndo hiyo wanafanya sasa wanakuwaje wapuuzi tena.
 
Unajuwa watz wengi wanajuwa kutalii mbugani ghalama kubwa lakini siyo kweli kabisa kiingilio cha juu 10000 na chini sh 5000 tu sasa huu uelewa wakijitahidi kuufanya kila mtu akafahamu watu wataenda sana tu.
Kiingilio 5,000-10,000 je unafikaje hapo mbugani? Gari ya aina gani utaingia nayo humo mbugani? Mfano mimi naishi Dar nina kagari kangu ka Passo naweza kuingia nako kule chini ngorongoro crator?
Changamoto sio 5,000 au 10,000 ya kuingia getini.
 
Back
Top Bottom