Bodi ya mkopo tafuteni njia mbadala kuwapata wadaiwa wenu sio mikwara na vitisho

yusuphmarcogaga

Senior Member
Jan 5, 2014
145
161
Bodi ya mikopo ivi karibuni imekuwa habar ya mjini wakijinasibu kuwafatilia waliokopeshwa kwa njia zozote hata kuchapisha picha zao....kwanza nipende tu kuwaarifu kwamba walio katika ajira zisizo rasmi wana kipato kikubwa hata kuliko hao mnaokomaa nao mnaowapata hapa nashauri mjikite katika kampeni ya kushawishi wadaiwa kujitokeza wenyewe kwa hiari ikiwa ni pamoja na hata wakati mwingine kutoa offers mfano watakao jitokeza ndani ya mwezi mmoja ujao watatangazwa kwenye vyombo vya habari kama wazalendo, au hata kuoata punguzo la asilimia kadhaa ndani ya muda flan mnaotoa kufanya kampeni nadhani mnaweza wakajitokeza wengi na mkafikia lengo lenu la makusanyo lakini mkiendelea na iyo mikwara mnazidi kutufanya tutafute chimbo.
 
Hawa jamaa ni viazi sana
Watapita kila ofisi Tanzania nzima kuanzia january.
Huu ni kutaka kupata per diem tu.
Ofisi zote tanzania hawawez kupita.
Watazunguka dsm tu basi then wataita waandishi wa habari na kutangaza waalimu 20 wafanyakazi kwenye kampuni za wahondi 10 basi.

Ukipiga mahesabu hao wafanyakazi kwa mhindi kwenyw kampuni za fummigation wanalipwa laki tano au nne kwa mwezi.
Ukianza tu kumkata mshahara wake ataacha kazi.

Na ndio hutompata tenaa!!! Nasema hutompata tena labda bahati ya Mungu mumuajiri serikalini.
Serikalini napo Magufuli hataki kusikia mtanzania wa kawaida kaajiriwa.
Ana alergy na watz kupata kazi, bora wachina waachriwe ila aio wa tz.
Au bora ateua maprofesa wa vyuo vikuu wote wawe na kazi mbili mbili ila sio mtanzania wa kawaida kupata kazi.
Funny enough hataki mpate elimu ya chuo bure ndio maana ndalichaa anakuja na masharti yasio na kichwa daily ila mradi tu mpungue .
Ni mkakatibwa jamaa hapendi.
Anataka aona kile kitu kimesimama na aogopwe.

Ok turudi kwenye bodi.
Hapa ni trumpet na makelel kwenye media ili jamaa asije akatumbulia anavyoona Makonda na dc Hapi wanazunguka na media GsM na clouds basi huyu badri naye anatamani hata azunguke na tv kwenye kutafuta wadaiwa anaowaita sugu.

Huku akiwa kasahau kuwa wadaiwa sugu wote wapo serikalini na mavyeo makubwa makubwa walisoma bureeee kabisa kabla ya mwaka 94. Na leo hii wanateuan na kupeana vyeo vikunwa vikunwa vijana nendeni mkafanya kazi za wa vietnam haloteli za laki nne.
Huko kwenye hizo kampuni kama huawei wachina wapo kibao wamepewa vibaya. Wataz wamebaki kuendesha magari ya kuwabeba.
Sera mbovu.
Povu langu liishie hapa
 
Hawa jamaa waacheni tu waendelee kukurupuka. Wana majina ya watu Ambao wanadaiwa na hawajawahi kukopa na pia wengine wamemaliza kulipa lakini bado wanadaiwa hata kama wamepewa cheti na bodi yenyewe kuthibitisha wamemaliza deni. Wakati umefika wa kuwachukulia hatua stahiki. Na tusubiri majina na picha.
 
Back
Top Bottom