Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 872
Wakuu wa jukwaa la Elimu habari,
Ningependa kuwasilisha matatizo yaliyowakumba wanafunzi wa St Joseph college tawi la Songea kwa kukatwa fedha yao ya kujikimu, jambo lililoleta mgogoro mkubwa na uongozi hadi kufikia hatua ya kugoma. Kiwango kilicholipwa kwa mwaka huu wa fedha ni kile cha zamani kabla serikali haijapandisha.
Hivi sasa bodi imetoa shilingi 367500/= tu kwa miezi miwili ya kwanza badala ya kiwango kipya cha shilingi 472000/= kilicholipwa baada ya serikali kupandisha viwango.
Uongozi wa chuo ulipoulizwa walisema suala hilo ni la bodi na si lao.Waulizwe bodi. Sasa hapa panahitajika kuapata maelezo toka kwa uongozi wa bodi kujua kwanini imeshusha kiwango hiki?Je vyuo vyote vimepata viwango hivi au ni hiki tu?Kama ni tofauti kwanini iwe hivyo kwao tu?
Nina amini kama tatizo hili lingetokea kwa UDSM basi mgomo ungetokea na maelezo yangepatikana haraka.Lakini chuo hiki cha wahindi ni kama wanajifanyia mambo wanavyotaka.
Naomba kuwasilisha ndugu zangu
Ningependa kuwasilisha matatizo yaliyowakumba wanafunzi wa St Joseph college tawi la Songea kwa kukatwa fedha yao ya kujikimu, jambo lililoleta mgogoro mkubwa na uongozi hadi kufikia hatua ya kugoma. Kiwango kilicholipwa kwa mwaka huu wa fedha ni kile cha zamani kabla serikali haijapandisha.
Hivi sasa bodi imetoa shilingi 367500/= tu kwa miezi miwili ya kwanza badala ya kiwango kipya cha shilingi 472000/= kilicholipwa baada ya serikali kupandisha viwango.
Uongozi wa chuo ulipoulizwa walisema suala hilo ni la bodi na si lao.Waulizwe bodi. Sasa hapa panahitajika kuapata maelezo toka kwa uongozi wa bodi kujua kwanini imeshusha kiwango hiki?Je vyuo vyote vimepata viwango hivi au ni hiki tu?Kama ni tofauti kwanini iwe hivyo kwao tu?
Nina amini kama tatizo hili lingetokea kwa UDSM basi mgomo ungetokea na maelezo yangepatikana haraka.Lakini chuo hiki cha wahindi ni kama wanajifanyia mambo wanavyotaka.
Naomba kuwasilisha ndugu zangu